Baba Majirani mbona wanatuchukia?

Baba Majirani mbona wanatuchukia?

Asante sana ila mapungufu ya baba ni mengi na hayavumiliki tena
Hahahahaaa Elli you are so creative! Big up! Hii lugha iliyotumika hata jirani hawezi kuistukia kw urahisi! Manake tunamueleza baba mapungufu yake bila kumuadhiri kwa majirani! Na hata wachangiaji wote wamezingatia.....
 
Hivi mara baada ya babu kufa, hakutuachia mrithi? nakumbuka marehemu babu alikua na wazee wenzie waliokuwa na maono kama yake, twaweza kwenda kuwaona hao?
Baba familia yako tu umeshindwa kuitunza, ona tunavyo chukiana ndani ya hii nyumba, unashindwa hata kumzuia kaka kunichomea kibanda changu cha wana kondoo...?
Baba boma lako limechafuka Baba, hebu ona na bamdogo nae anavyo Pinda na kushadadia tupigwe wakati tukiwa kwenye arakati ya kutafuta uongozi bora wenye amani na maendeleo katika familia yetu...!
Baba hebu toa lile tabasamu nililolizoea na uweke ndita usoni kama marehemu Babu labda naweza kuhisi kweli uko serious na hii familia, maana nahisi kama unataka kututoa kafara!!!!!!!
 
Hivi mara baada ya babu kufa, hakutuachia mrithi? nakumbuka marehemu babu alikua na wazee wenzie waliokuwa na maono kama yake, twaweza kwenda kuwaona hao?

hata tukiwaona haitasaidia maana Baba kamwe hatosikia ushauri kutoka kwa rafiki zake Babu.... yeye huwaamini sana wale nduguze wenye nembo ya uoto wa asili!!!!!!!
Kaka, mwenzio natamani sana kwenda kupaza sauti pale kwenye ule MBUYU wa matambiko, labda Baba anaweza akanielewa......!
 
Hivi ni kunapotokea frictions na majirani ni lazima vita vitokee? kwa nini tunatengeneza hofu isiyo na msingi?
 
majirani walipoambiwa shamba letu (ardhi) haliwahusu, ndio chuki hizi unazoziona zikaanza.
Walizidisha chuki siku yule mbuni mkubwa (air force one) alipotua uani kwetu. Wivu ukawazidi eti kwa nini hakutua kwao.
Tujijue na kujitegemea sasa, majirani wa karibu hatuna.

umenena mkuu.natamani jk asome hapa.kimsingi majirani hatuna.waliopo ni manyangau.mmoja anaitangazia dunia mlima kilimanjaro na mbuga zetu ziko kwake.wengine wanajenga bahima empire wakiwa na lengo la kuchukua ardhi yetu na kutawala.hawa nao wanaitangazia dunia kuwa wanatawala tanzania.tulipowashtukia wanaleta za kuleta.sio ajabu wakaanzisha vita.mburula kweli hawa!!!!!TUMEWAKENULIA VYA KUTOSHA NA KWA MUDA MREFU.
 
Mbaya zaidi nilimsikia jirani anakuteta, anasema eti kwamba wewe na mama siyo wazazi wetu na hustahili kuitwa baba kwa sababu wewe ni "unfit", lakini mimi siamini hayo maneno ya majirani zetu.
 
Baba kwa kutambua kuwa hutaweza kupatana na majirani ndio maana umetuletea wazo tuwe na nyumba mbili kwa atakayetaka, ukiwasingizia wanao walioondoka kwenda kuishi ughaibuni? Au ni janja yako baba ya kutaka kutukimbia ukiona kumechafuka ukaishi na wanao waliokukimbia ukisikilizia machungu uliyoyaacha kama yatatumaliza, na machungu hayo yakishindwa kutumaliza urudi tena ukijifanya ulienda kusalimia wanao wa kule. tukiisha ubaki huko huko ukila raha na hao.
 
Sasa naanza kumuelewa babu aliposema mwanae huyu alikuwa bado hajakuwa kuweza kuilea familia

na nadhan babu asingefariki bado baba asingekua kiongoz wa hii familia labda yule baba mdogo aliyekataa kuwa msaidiz wa familia yetu.
 
Ni kweli ardhi inawauma sasa je tungekubali ingekuwaje? Na ujio wa obama iliwauma sana tena wakome tujitoe eac choooonde
 
Mbaya zaidi nilimsikia jirani anakuteta, anasema eti kwamba wewe na mama siyo wazazi wetu na hustahili kuitwa baba kwa sababu wewe ni "unfit", lakini mimi siamini hayo maneno ya majirani zetu.

Majirani walikwenda mbali zaidi kuwa wewe na mama sio biological parents wetu na ndio maana hamtujali; baada ya wazazi wetu kufa nyie ndio mlikuja kwa babu kumuomba eti mtulee ingawa yeye hakupendelea kabisa lakini kwa kutumia mtandao wenu wa kiharamia mkatuchukua!!
 
hii mbona sikuiskia Mkuu? hivi kumbe wazazi wetu sio halisi? Imeniuma sana hii, how come tusiwe na wazazi halisi? Maskini weee kumbe ndio maana anatuacha tunateseka na kusimangwa hivi??
Majirani walikwenda mbali zaidi kuwa wewe na mama sio biological parents wetu na ndio maana hamtujali; baada ya wazazi wetu kufa nyie ndio mlikuja kwa babu kumuomba eti mtulee ingawa yeye hakupendelea kabisa lakini kwa kutumia mtandao wenu wa kiharamia mkatuchukua!!
 
hii bona sikuiskia Mkuu? hivi kumbe wazazi wetu sio halisi? Imeniuma sana hii, how come tusiwe na wazazi halisi? Maskini weee kumbe ndio maana anatuacha tunateseka na kusimangwa hivi??

Daah,inauma kwa kweli. Babu tuonyeshe njia huko uliko.
 
MamaYooo !! BabaEeee !! bora watundikie na uninginize mkungu wa ndizi hao majirani watakuja kutuomba msamaha na kukupigia magoti watuombe radhi....! Ujirani Mwema urudi kama zamani kwani waTZ hatukuzoea uhasama na mashemeji zetu !! Elli safari njema na urejee salama.
 
Majirani walipoambiwa shamba letu (ardhi) haliwahusu, ndio chuki hizi unazoziona zikaanza.
Walizidisha chuki siku yule mbuni mkubwa (air force one) alipotua uani kwetu. Wivu ukawazidi eti kwa nini hakutua kwao.
Tujijue na kujitegemea sasa, majirani wa karibu hatuna.
shida ilianzia hapo kwenye bold, mengine yote ni kusherehesha tu bifu
 
Back
Top Bottom