Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 11,866
- 4,252
Ukweli mchungu. Hata Chipando mwenyewe anajua sasa, kuwa hali si shwari tena na sio mteremko baada ya kusikia kauli ya mgombea urais ccm. Kote kwingine alikuwa akisema anataka mafiga matatu ila alipofika Kigoma kauli yake ilibadilika. Kwamba wanakigoma wataamua. Huo ni ujumbe kwako Chipando kuwa jimbo lina wenyewe.
Wenyewe hao kwanza ni wazoefu wa siasa. Wasomi. Hazina ya Taifa pia maana Bungeni pawapo na mijadala ya kitaifa na kimkakati, hoja zake huwa zina nafasi ya kufanya maamuzi.
Nakumbuka ulibananishwa na Kipotoshi na ulionyesha udhaifu mkubwa sana kuhusu uelewa wa masuala ya kibunge. Sasa kweli Samia amuache Zitto ambaye atakuwa msaada kwake mbeleni halafu akuchukue wewe mzee wa vibe? Hapana.
Asante kwa kushiriki. Ulitumika tu kumuweka benchi Kilumbe ili wenye jimbo warudi. Na amesharudi. Ushauri wangu kwako tu kwa sasa ni uwe na akiba ya maneno. Usimzodoe sana kaka yako from another father kwani baada ya October huwezi kujua kitatokea nini. Suala kwamba zilikuwa ni kampeni tu zile, sio kwa Zitto.
Hapo nimezungumzia upande mmoja tu nikiacha mengine yawe constant.
Wenyewe hao kwanza ni wazoefu wa siasa. Wasomi. Hazina ya Taifa pia maana Bungeni pawapo na mijadala ya kitaifa na kimkakati, hoja zake huwa zina nafasi ya kufanya maamuzi.
Nakumbuka ulibananishwa na Kipotoshi na ulionyesha udhaifu mkubwa sana kuhusu uelewa wa masuala ya kibunge. Sasa kweli Samia amuache Zitto ambaye atakuwa msaada kwake mbeleni halafu akuchukue wewe mzee wa vibe? Hapana.
Asante kwa kushiriki. Ulitumika tu kumuweka benchi Kilumbe ili wenye jimbo warudi. Na amesharudi. Ushauri wangu kwako tu kwa sasa ni uwe na akiba ya maneno. Usimzodoe sana kaka yako from another father kwani baada ya October huwezi kujua kitatokea nini. Suala kwamba zilikuwa ni kampeni tu zile, sio kwa Zitto.
Hapo nimezungumzia upande mmoja tu nikiacha mengine yawe constant.