Baada ya Serikali kutenga Tsh. Bilioni 1.4 kwa ajili ya Chuo cha VETA Rorya, awamu ya kwanza ya ujenzi yaanza

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,813
11,991
f910ab6f-20dd-46a5-a5a3-dd92b7038743.jpg

Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imetenga kiasi cha Shilingi Bilioni 1.4 kwa ajili ya ujenzi wa Chuo cha Ufundi (VETA) cha kwanza kitakachojengwa Wilaya ya Rorya.

Chuo hicho kitajengwa kwa awamu mbili ambapo kwa awamu ya kwanza ni ujenzi wa majengo 9.

Mkuu wa Wilaya ya Rorya, Juma Chikoka amesema "Tunamshukuru Rais kwa kuwa mkombozi wa jamii ya Wanarorya kwani watapata ujuzi na ufundi utakaowasaidia kuajiriwa na kujiajiri, ndio maana nimeongoza mamia ya Wanarorya kushiriki shughuli za maendeleo kwa kuanza kuchimba misingi."

Aidha, DC Chikoka pia amempongeza Mbunge wa Jimbo la Rorya, Jafari Chege kwa kuendelea kusimamia ahadi zake kwa vitendo.
50a2f318-d6fe-4a2a-bb89-a7651ff7ed8f.jpg

a46273f4-8b5c-46ff-8e11-9187b455d139.jpg

57e09479-8617-4aa3-a89b-8c6cfb46b938.jpg
 
Back
Top Bottom