Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,900
- 944
Mbunge wa Jimbo la Kiteto, Mhe. Edward Ole Lekaita ameendelea na ziara yake Kata ya Partimbo kutembelea eneo la ujenzi wa Chuo cha VETA kukagua maendeleo yake. Amewapongeza wasimamizi na mkandarasi wa mradi huo kwa kazi kubwa inayoendelea
Mhe. Edward Lekaita amezungumza na Wananchi wa Kata ya Matui na kuchangia 150,000 kati ya 200,000 zilizokuwa zinahitajika kununua uwanja wa mpira Ifukuza na kusikiliza kero zao huku Wananchi hao wakimshukuru kwa miradi na kumuomba kutatua kero za Maji, Umeme na Barabara.
Aidha, Mhe. Edward Ole Lekaita amesema kuwa kiasi cha Shilingi Milioni 580 zimetumika kujenga Shule mpya ya Msingi na kuwasisitiza wazazi kuhakikisha wanawapeleka watoto Shule pindi itakapokamilika.
Vilevile, Mhe. Edward Ole Lekaita amekagua maendeleo ya ujenzi wa daraja la Shilingi Milioni 118 linalojengwa ili kupunguza kero ya kushindwa kupita kuelekea Matui wakati wa kipindi cha mvua.
Attachments
-
WhatsApp Image 2023-09-11 at 11.43.35.jpeg1 MB · Views: 2
-
WhatsApp Image 2023-09-11 at 11.43.35(1).jpeg900.1 KB · Views: 2
-
WhatsApp Image 2023-09-11 at 11.43.36.jpeg825.5 KB · Views: 2
-
WhatsApp Image 2023-09-11 at 11.43.36(1).jpeg708.1 KB · Views: 2
-
WhatsApp Image 2023-09-11 at 11.43.36(2).jpeg1.1 MB · Views: 2
-
WhatsApp Image 2023-09-11 at 11.43.37.jpeg957.7 KB · Views: 2
-
WhatsApp Image 2023-09-11 at 11.43.37(1).jpeg902.3 KB · Views: 2
-
WhatsApp Image 2023-09-11 at 11.43.38.jpeg818 KB · Views: 2
-
WhatsApp Image 2023-09-11 at 11.43.38(1).jpeg730.1 KB · Views: 2