Baada ya njia za giza kugonga mwamba kwenye kusaka utajiri, nimeamua kufanya hivi

Baada ya siku nyingi kupita leo nimemkumbuka rafiki yangu kipenzi ambaye alipatwa na matatizo makubwa katika safari yake yakusaka maisha miaka kama 5 iliyopita tukiwa kidato cha sita yaani kila nikikumbuka nabaki kulia tu.

Wakati naripoti shuleni nilikuwa nimechelewa kidogo baada ya kufika pale kutokana na jitihada zangu za masomo darasani nilitokea kuelewana na jamaa mmoja alikuwa anaitwa agustino yeye alikuwa anasoma hge mimi nilikuwa egm masomo mengi tulikuwa tunaendana tukawa tunadiscuss pamoja

Kumbe jamaa huyo agustino alikuwa amejisajili kama private candidate so alikuwa anatokea kitaa kuja shuleni baada ya urafiki kuzidi nikawa natoroka mara kwa mara tunaenda kukaa getto na kupiga story pamoja na masela wengine

Kifupi wakati ule nilikuwa na kama miaka 18 lakini kutokana na mwili wangu tulikuwa tukitembea nae unaona kama mimi nimkubwa maana alikuwa anamwili mdogo mdogo sana

Wakati natoka nyumbani nilikuwa bado sina mawazo kichwani ya kuwa na pesa nyingi nilichokuwa naona mbele yangu ni namna gani nitafaulu kidato cha sita michongo ya pesa niliowahi kufanya ilikuwa ni vibarua vya kawaida kitaa

Lakini jamaa yangu alikuwa ni mtu wa mishe mishe nyingi kila akikaa lazima apigiwe simu, tukiwa tunaongea lazima apige story za maswala ya pesa. Wallet yake akitoa hela unaona imejaa misimbazi nikawa najiuliza jamaa hizi hela anatoa wapi nikabaki kusema labda kwao watakuwa wanajiweza sana, japo ukimuangalia vizuri haonekani kama katokea kwenye rich family.

Getto alipokuwa amepanga lilikuwa limesheheni kila kitu,
Mtaani pale alikuwa amezoeleka na watu wengi chocho nyingi akawa ananionyesha sasa kuna siku weekend kaniambia nimsindikize akachukue pesa yake kwa jamaa yake mmoja.

Alinipitia pale shuleni tukaondoka kuelekea kwa huyo jamaa shule tuliokuwa tunasoma iko maeneo ya kijijini so tulukuwa tunapita njia za vichakani chakani kuna mashamba wanalima nyanya, na matikiti maji nyumba ziko mbali mbali sana.

Baada ya kuvuka kamto tufika kwa yule jamaa mimi ikabidi ni baki njee halafu jamaa mwenyewe kumuona umri ulikuwa kama umeenda hivi ,alikuwa na zaidi ya 50 year tulisalimiana wenyewe wakaingia ndani lakini kwa njee nilisikia kama mabishano ambayo sikujua wanazungumzia nini....

Sent using Jamii Forums mobile app
Ilikendelea unistue aseee
 
Tuendelee.
Ilipita siku kadhaa safari ya kwenda kwa yule mganga ikawadia.
Hapo shule tushalegeza maana nilianza kufikiria pesa. Ukichangay a na bangi tulikuwa tunavuta ikawa ndio basi tena.

Kufika kwa mkongo anatueleza shida yetu kabla hatuja mweleza.
Na masharti yake ikawa ni kulala chini na kutoosha kichwa.

Kweli yale masharti niliyaweza na nikaanza biashara ya vitenge.

Asikuambie mtu mambo yalinyooka sana.
Nilianza na mtaji wa laki 6 Augustino alinipa ndani ya miezi mitatu nilikuwa na mtaji wa milioni 5.
Biashara ikachangamka sana na shule tukaacha.
Mara nikaanza kuona mambo ambayo siyaelewi jamaa akaniambia turudi kwa mkongo....kufika kule mganga kasema nilikosea sharti.
Inatakiwa nisafishe kwa damu ya mwanadamu.

Hapo nikawaza sina mke wala mtoto.
Nina mama na baba na ndugu zangu wa chache nikianza kutoa kafara itakuwaje....

Nikaamua rasmi acha nifilisike watu wawe salama.


Wazoefu wa biashara bila uchawi nipeni uzoefu nisimane tena.

NB:-HII STORY HATA SIO YANGU ,NIMEIKAMILISHIA TUU.
Wewe ni mkali aiseee...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shule ipo mashambani, vichakani
Huko hukohuko kijijini kuna tax
We na Muddy mlitembea umbali gani kwenda kumpokea boss wa Bangi?

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu ningekuwa na uwezo ningekutajia jina la shule lakini siwezi, shule iko njee ya mji barabara kuu zinapita mpaka kwenye mashamba ya watu.

Shule yetu ilikuwa karibu na centre unakuta vijana wamejaa wanapiga boda mazingira yaliyobaki ni nyumba moja moja na mashamba

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Story kali na ni nzuri sana tunaisubiria tujue jinsi gan ulikuwa drag dealer na kukimbizana na cops
Mkuu sikuwahi kuwa drug dealer au kukimbizana na polisi kisa hiyo mishe ndomaana kunajamaa hapo juu anadhani ni hadithi ya alinacha akaamua aweke muendelezo wake mimi nasimulia nilichokiona na macho yangu na wala sii story ya kutunga

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Njia yenyewe tayari ina giza, iweje uone uone/ upate mali kwa njia hiyo?
 
Mkuu ningekuwa na uwezo ningekutajia jina la shule lakini siwezi, shule iko njee ya mji barabara kuu zinapita mpaka kwenye mashamba ya watu. Shule yetu ilikuwa karibu na centre unakuta vijana wamejaa wanapiga boda mazingira yaliyobaki ni nyumba moja moja na mashamba

Sent using Jamii Forums mobile app
Aiseeeee leta Leta mkuuu
 
Back
Top Bottom