Kibunago
JF-Expert Member
- Jan 11, 2008
- 300
- 122
Hatuwezi kukimbilia kuwa ana matatizo ya kiafya (kichaa) hadi jopo la Madaktari wa magonjwa ya akili watakapothibitisha.
Kwa vile kasema mwenyewe kuwa aliwahi kuuwa. Polisi inatakiwa kumuhifadhi mahala kwa usalama wake sasa, kisha kuchukuwa maelezo yake kwa kina na kuyachunguza. Ikithibitisha kuwa ana kesi ya kujibu iihusuyo mauaji na kujihusisha na imani za kichawi asogezwe Mahakamani mara moja kwa mujibu wa sheria za nchi yetu.
Kwamba alitumwa kuuwa akiwa Msukule na Waziri, hilo la (UCHAWI) ni gumu sana kulithibitisha (beyond reasonable doubt) mahakamani. Hata hivyo maelezo hayo nayo yatafanyiwa kazi kwa kina akiulizwa kuonyesha jinsi alivyokuwa anakutana na huyo Waziri na kupewa maelezo na faida aliyokuwa anaipata huyo Waziri katika kuuwa au hata uthibitisho wowote kuwa huyo Waziri anahusika na hayo Mauaji.
Nasikitika kuwa ikishindikana kuoneka kuhusika kwa Waziri, mtajwa hapa, atakabiliwa na kesi nyingine ya kujibu ya slander per se ambayo itaonekana kuwa anakusudia kumchafua Mh. Waziri kwa sababu anazozifahamu yeye.
Kwa vile kasema mwenyewe kuwa aliwahi kuuwa. Polisi inatakiwa kumuhifadhi mahala kwa usalama wake sasa, kisha kuchukuwa maelezo yake kwa kina na kuyachunguza. Ikithibitisha kuwa ana kesi ya kujibu iihusuyo mauaji na kujihusisha na imani za kichawi asogezwe Mahakamani mara moja kwa mujibu wa sheria za nchi yetu.
Kwamba alitumwa kuuwa akiwa Msukule na Waziri, hilo la (UCHAWI) ni gumu sana kulithibitisha (beyond reasonable doubt) mahakamani. Hata hivyo maelezo hayo nayo yatafanyiwa kazi kwa kina akiulizwa kuonyesha jinsi alivyokuwa anakutana na huyo Waziri na kupewa maelezo na faida aliyokuwa anaipata huyo Waziri katika kuuwa au hata uthibitisho wowote kuwa huyo Waziri anahusika na hayo Mauaji.
Nasikitika kuwa ikishindikana kuoneka kuhusika kwa Waziri, mtajwa hapa, atakabiliwa na kesi nyingine ya kujibu ya slander per se ambayo itaonekana kuwa anakusudia kumchafua Mh. Waziri kwa sababu anazozifahamu yeye.