Madame S
JF-Expert Member
- Mar 4, 2015
- 17,172
- 34,277
ERIC SHIGONGO
MZIMU UNAOTABASAMU-01
Mchungaji wa kimataifa wa Kanisa la Revelation lililopo jijini New York nchini Marekani, Gideon Matimya alishtuka kutoka usingizini mara baada ya kusikia mlio wa simu ya mezani iliyokuwa ikiita kwa fujo sebuleni. Alishangaa, kitu cha kwanza kabla ya kuteremka kutoka kitandani ni kumwangalia mkewe, Lucy ambaye naye alishtuka kutoka usingizi na kumwangalia mumewe huyo.
Haikuwa kawaida kwa simu hiyo kuita, ulipita mwezi mzima hawakuwa wameitumia, ilikuwa mbovu na hawakuwa na muda wa kuitengeneza kwa kuwa walikuwa wakitumia simu za mikononi. Kitendo cha simu hiyo kuanza kuita, walishangaa, kitu cha kwanza kabisa ambacho walijiuliza ni siku ambayo waliitengeneza simu hiyo.
Mchungaji Gideon akateremka kutoka kitandani, akatoka chumbani na kuanza kuteremka ngazi. Lucy hakubaki chumbani mule, naye akateremka na kumfuata mkewe huku wote wawili wakionekana kuwa na hofu nzito. Hatua zao zilikuwa za taratibu, walikuwa wakitembea huku wakionekana kuhofia kitu fulani, macho yao hayakutulia chumbani, walikuwa wakiangalia huku na kule kwani walihisi kwamba mbali na wao ndani ya nyumba hiyo, pia kulikuwa na mtu mwingine aliyekuwa akiwatazama.
“Ngriii...ngriii..ngriii...” simu ilindelea kuita mfululizo.
Usingizi wote waliokuwa nao ukakatika, macho yakawa makavu na woga kujaa mioyoni mwao. Walipoifikia simu ile, Mchungaji Gideon akauchukua mkonga wake na kuupeleka sikioni huku akitetemeka kwani alihisi kabisa simu ile haikuwa ya kawaida, ilikuwa ni simu ya hatari, simu iliyotoka kwa mtu hatari.
“Halo...” aliita kwa sauti ndogo iliyosikika kama mtu aliyekuwa na hofu moyoni mwake.
“Halo!” sauti ya upande wa pili ikasikika.
“To whom Am I speaking?” (nazungumza na nani?) aliuliza kwa sauti ya taratibu sana.
“The Smilling Ghost you created.” (mzimu unaotabasamu ulioutengeneza) sauti ya upande wa pili ilijibu.
Mchungaji Gideon akanyamaza, akazidi kutetemeka huku akimwangalia mke wake. Jibu la mtu huyo aliyepiga simu lilimtisha. Hakumjua mpigaji, hakukumbuka kama aliwahi kumtengeneza mtu na kuwa kiumbe kibaya. Katika maisha yake alimwamini Mungu, alimwabudu usiku na mchana na kujitolea katika maisha yake kwamba atamuabudu kwa moyo wake wote mpaka kifo chake.
Aliwawahubiria watu kuhusu kumjua Mungu, aliwaombea na wengine kuokoka na mwisho wa siku kuwabatiza kwa maji mengi. Mtu aliyekuwa amepiga simu alikuwa nani? Na alikuwa akihitaji nini kutoka kwake? Kila alichokuwa akijiuliza, alikosa jibu.
“Unahitaji nini?” aliuliza, kipindi hiki kidogo akatoa sauti iliyokuwa na ujasiri.
“Nilitaka nikwambie kitu kimoja tu kwamba nipo hai, nimeishi maisha ya tabu mpaka kuwa hapa, niliteseka, nililia usiku na mchana, niliumia kwa ajili yako. Jua kwamba sikufa, nipo hai, ninapumua kama unavyopumua,” alisema mtu aliyesikika upande wa pili maneno ambayo yalimchanganya kabisa Mchungaji Gideon.
“Wewe ni nani?”
“Mzimu Unaotabasamu. Mzimu unaotafutwa kila kona katika dunia hii,” alijibu mwanaume huyo.
Hapo ndipo Mchungaji Gideon akamfahamu mtu huyo. Alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa wakitafutwa kwa nguvu kubwa duniani kote huku maofisa wa Kijasusi wa CIA wakiwa mstari wa mbele kabisa. Katika orodha ya watu mia moja waliokuwa wakitafutwa kwa udi na uvumba wa kwanza kabisa alikuwa mwanaume huyo. Hakujulikana, hakukuwa na mtu aliyejua sura yake ilifananaje lakini ndiye mtu aliyekuwa akiua watu wengi kila siku duniani.
Alijulikana kama The Smilling Ghost kwa maana ya Mzimu Unaotabasamu, na kwa kuwa hakuwa akijulikana jina lake, hata kwenye orodha hiyo ya CIA waliliandika jina hivyohivyo japokuwa hawakujua mwanaume huyo alifananaje na hakukuwa na mtu aliyejua sababu iliyompelekea kufanya mauaji katika siku ya Jumapili.
“Leo ni Jumapili, huu ni usiku wa kuamkia Jumapili, ina maana unataka kuniua?” aliuliza Mchungaji Gideon huku akianza kuingiwa na hofu kwa mara nyingine.
“Hapana. Nimekupigia simu kukwambia kwamba leo ndiyo siku maalumu ya Mzimu Unaotabasamu kukamatwa. Nahisi baada ya kukamatwa, hakutokuwa tena na mauaji kwa Jumapili ya leo,” alisema mwanaume huyo maneno yaliyozidi kumchanganya zaidi Mchungaji Gideon.
“Unamaanisha nini?”
“Umeangalia stoo?”
“Hapana! Kuna nini?”
“Umeangalia bafuni?” aliendelea kuuliza.
“Hapana. Kuna nini?”
“Hata hukujiuliza kwa nini mbwa wako leo habweki?” aliuliza mwanaume huyo.
Swali hilo lilimfanya Mchungaji Gideon kujiuliza kuhusu mbwa huyo. Hakujua ni kitu gani kilikuwa kimetokea, kila siku usiku mbwa wake aliyempa jina la Bobby alikuwa akibweka mno kuhakikisha nyumba yake inakuwa salama mbali na kamera ndogo za CCTV alizokuwa amezifunga ndani ya nyumba yake.
Siku hiyo alikuwa kimya kabisa, alishangaa, alijiuliza maswali yasiyokuwa na majibu lakini alikuwa na uhakika kwamba mwanaume aliyekuwa akizungumza naye alifahamu kila kitu. Baada ya kujiuliza kuhusu mbwa huyo, akajiuliza kuhusu huko stoo na bafuni alipokuwa ameambiwa, alihisi kulikuwa na kitu, alihisi kabisa kwamba mwanaume alikuwa amefanya jambo.
“Unataka nini?” aliuliza kwa ukali kidogo.
“Polisi wanaingia hapo dakika chache zijazo. Hakutokuwa na kitu chochote watakachokijua zaidi ya kufahamu kwamba wewe ndiye Mzimu waliyekuwa wakimtafuta kwa miaka kumi na tano, dunia itajua kwamba wewe ndiye mwanaume aliyekuwa akiua kila Jumapili, itajua kwamba wewe ndiye uliyemuua waziri mkuu wa Uingereza, mwanamitindo, Amanda Posh, Mwanamuziki Michael Turner, kwa kifupi, dunia nzima itajua kwamba wewe ndiyo mimi,” alisema mwanaume huyo na kukata simu.
“Halo..halo..halo..” aliita Mchungaji Gideon lakini simu ilikuwa imekatwa.
Mwili mzima ulikuwa ukitoka jasho, hakutaka kuchelewa, ilikuwa ni lazima kwenda bafuni na chooni kuona ni kitu gani kilikuwa kimetokea huko. Yeye na mkewe, kwa kasi ya ajabu wakaanza kuelekea bafuni, walipoufikia mlango na kuufungua, hawakuamini walichokiona, maiti ya mwanamke ilikuwa sakafuni, ilichomwa visu vinne kifuani, damu zilikuwa zikitoka huku kwenye paji la uso kukiwa na alama ya msalaba, yalikuwa ni aina ya mauaji yaleyale aliyokuwa akiua mtu huyo aliyekuwa akitafutwa.
Mkewe akaanza kupiga kelele kwa woga, hakuamini alichokuwa akikiona, moyo wake ulikufa ganzi na mwili kumtetemeka. Mchungaji Gideon akachanganyikiwa, hakujua ni kitu gani kilikuwa kimetokea mpaka maiti ile kuletwa ndani ya nyumba yake.
Akatoka na kueleka stoo, alipoufikia mlango na kuufungua, akakutana na maiti nyingine ya mtoto iliyokuwa sakafuni. Nayo ilichomwa visu viwili kifuani na kwenye paji la uso kulikuwa na alama ya msalaba, ilikuwa ni aina ya mauaji yaleyale aliyokuwa akiyafanya Mzimu.
“Mungu wangu! Kwa nini mimi?” alijiuliza na kutoka ndani.
Akaelekea katika banda la mbwa, alichokikuta huko ni maiti ya mbwa wake ikiwa chini. Aliuawa kwa kuchomwa visu mfululizo.
Machozi yakaanza kumtoka, hakuamini. Hata kabla hajafikiria ni kitu gani kilikuwa kimetokea, akaanza kusikia mlio ving’ora vya polisi wakija kule ilipokuwa nyumba yake, akazidi kuogopa.
Haraka sana akarudi ndani ya nyumba yake, akamkuta mkewe akiendelea kulia, hakujua ni kitu gani alitakiwa kufanya. Wakati akimchukua mkewe kwa ajili ya kumpeleka chumbani, polisi nao wakapiga teke geti kubwa na kuingia ndani huku wakiwa na bunduki mikononi mwao, tena wengine walikuwa wale polisi waliokuwa na silaha nzito ambao walikuja na gari lao lililoandikwa kwa maandishi makubwa yaliyosomeka S.W.A.T.
Hawakuingia kistaarabu, wakavunja mlango wa sebuleni na kuingia ndani. Walipofika, wakamkuta Mchungaji Gideon akiwa na mkewe, walikuwa wamekumbatiana chini huku wote wakilia kama watu waliokuwa wamefiwa.
“Mpo chini ya ulinzi! Nyanyueni mikono juu,” alisema polisi mmoja huku wakiwanyoonyeshea bunduki, wakatii na kufanya hivyo.
Kabla ya kufungwa pingu, polisi wale wakaanza kuangalia ndani ya nyumba hiyo, tena moja kwa moja wakaelekea stoo na bafuni na kuzikuta maiti hizo, yaani walikuwa kama watu ambao walijua maiti zilipokuwa. Wakawafunga pingu na kutoka nao ndani ya nyumba ile.
“Hatukuua! Hatukumuua mtu yeyote! Mimi ni mchungaji, mnanijua, mimi ni mpaka mafuta wa Bwana, sikumuua mtu yeyote yule,” alijitetea Mchungaji Gideon huku akiwaangalia polisi hao.
“Tumekutafuta sana. Kumbe mchungaji anayeaminika duniani, mpaka mafuta wa Bwana, anayewahubiria watu Neno la Mungu ndiye Mzimu Unaotabasamu tunayemtafuta! Mungu wangu! Kweli dunia imekwisha,” alisema polisi mmoja huku akionekana kushangaa.
Hakukuwa na mtu aliyemsikiliza, wakawachukua na kuwapeleka katika kituo cha polisi hapo kilichokuwa Manhattan jijini New York na kuwatuliza huko huku wakitakiwa kusubiri mpaka asubuhi itakapofika na mambo mengine ya kimahakama kuendelea.
Kukamatwa kwake haikuwa siri hata kidogo, usiku huohuo taarifa zikaanza kupelekwa sehemu mbalimbali kwamba hatimaye Mzimu Unaotabasamu alikuwa amekamatwa. Watu wengi walishtuka na kushangaa baada ya kupewa taarifa kwamba Mzimu wenyewe alikuwa mchungaji Gideon aliyekuwa na kanisa kubwa lililokuwa na washirika zaidi ya milioni moja duniani kote.
Ilipofika majira ya saa 10:15 alfajiri, Mchungaji Gideon akatolewa kutoka katika chumba alichokuwemo na kupelekwa katika chumba kingine kwa ajili ya kufanyiwa mahojiano. Muda wote alikuwa akilia huku akisisitiza kwamba hakuwa muuaji bali kulikuwa na mtu aliyekuwa ameua na kuzipeleka maiti katika nyumba yake.
Hilo halikusikilizwa. Alipofikishwa ndani ya chumba cha mahojiano, akakalishwa kwenye kiti na kuanza kuhojiwa. Muda wote alikuwa akilia, aliikunja mikono yake kama mtu aliyekuwa akisali, mara kwa mara alikuwa akifanya ishara ya msalaba lakini yote hayo yalionekana kama unafiki machoni mwa polisi waliokuwa ndani ya chumba hicho.
Wakaanza kumuuliza maswali kadhaa. Kila swali alilokuwa akiulizwa, Mchungaji Gideon aliwaambia kwamba hakuwa ameua na hakumfahamu mtu aliyekuwa amezileta maiti zile nyumbani kwake kwani alipigiwa simu na mtu aliyejitambulisha kwa jina la Mzimu Unaotabasamu na kuzipeleka maiti zile nyumbani kwake lakini si yeye aliyekuwa amefanya mauaji hayo.
“Fungua hiyo bahasha,” alisema mwanaume aliyekuwa akimuhoji huku akimpa bahasha kubwa ya kaki na kumwambia afungue.
Haraka sana akaifungua. Humo akakutana na picha mbili zikimuonyesha yeye akiwa amesimama nje ya nyumba moja huku mkononi akiwa ameshika kisu kilichokuwa na damu, na ndani ya nyumba hiyo kulikutwa maiti mbili za wanawake ambazo zilichomwa visu vifuani na kuwekewa alama ya msalaba katika paji la uso la kila mmoja.
“Huyu ni nani?” aliuliza polisi yule swali ambalo Mchungaji Gideon alishindwa kabisa kulijibu kwani kila alipokuwa akiiangalia sura ile, alikuwa yeye ila hakukumbuka kama kulikuwa na siku aliwahi kwenda kufanya mauaji yoyote yale.
“Huyu ni nani?” aliuliza polisi kwa sauti ya juu. Badala ya kujibu, Mchugaji Gideon akaanza kulia kwa sauti kama mtoto mdogo huku akisisitiza kwamba hakuua.
MZIMU UNAOTABASAMU-01
Mchungaji wa kimataifa wa Kanisa la Revelation lililopo jijini New York nchini Marekani, Gideon Matimya alishtuka kutoka usingizini mara baada ya kusikia mlio wa simu ya mezani iliyokuwa ikiita kwa fujo sebuleni. Alishangaa, kitu cha kwanza kabla ya kuteremka kutoka kitandani ni kumwangalia mkewe, Lucy ambaye naye alishtuka kutoka usingizi na kumwangalia mumewe huyo.
Haikuwa kawaida kwa simu hiyo kuita, ulipita mwezi mzima hawakuwa wameitumia, ilikuwa mbovu na hawakuwa na muda wa kuitengeneza kwa kuwa walikuwa wakitumia simu za mikononi. Kitendo cha simu hiyo kuanza kuita, walishangaa, kitu cha kwanza kabisa ambacho walijiuliza ni siku ambayo waliitengeneza simu hiyo.
Mchungaji Gideon akateremka kutoka kitandani, akatoka chumbani na kuanza kuteremka ngazi. Lucy hakubaki chumbani mule, naye akateremka na kumfuata mkewe huku wote wawili wakionekana kuwa na hofu nzito. Hatua zao zilikuwa za taratibu, walikuwa wakitembea huku wakionekana kuhofia kitu fulani, macho yao hayakutulia chumbani, walikuwa wakiangalia huku na kule kwani walihisi kwamba mbali na wao ndani ya nyumba hiyo, pia kulikuwa na mtu mwingine aliyekuwa akiwatazama.
“Ngriii...ngriii..ngriii...” simu ilindelea kuita mfululizo.
Usingizi wote waliokuwa nao ukakatika, macho yakawa makavu na woga kujaa mioyoni mwao. Walipoifikia simu ile, Mchungaji Gideon akauchukua mkonga wake na kuupeleka sikioni huku akitetemeka kwani alihisi kabisa simu ile haikuwa ya kawaida, ilikuwa ni simu ya hatari, simu iliyotoka kwa mtu hatari.
“Halo...” aliita kwa sauti ndogo iliyosikika kama mtu aliyekuwa na hofu moyoni mwake.
“Halo!” sauti ya upande wa pili ikasikika.
“To whom Am I speaking?” (nazungumza na nani?) aliuliza kwa sauti ya taratibu sana.
“The Smilling Ghost you created.” (mzimu unaotabasamu ulioutengeneza) sauti ya upande wa pili ilijibu.
Mchungaji Gideon akanyamaza, akazidi kutetemeka huku akimwangalia mke wake. Jibu la mtu huyo aliyepiga simu lilimtisha. Hakumjua mpigaji, hakukumbuka kama aliwahi kumtengeneza mtu na kuwa kiumbe kibaya. Katika maisha yake alimwamini Mungu, alimwabudu usiku na mchana na kujitolea katika maisha yake kwamba atamuabudu kwa moyo wake wote mpaka kifo chake.
Aliwawahubiria watu kuhusu kumjua Mungu, aliwaombea na wengine kuokoka na mwisho wa siku kuwabatiza kwa maji mengi. Mtu aliyekuwa amepiga simu alikuwa nani? Na alikuwa akihitaji nini kutoka kwake? Kila alichokuwa akijiuliza, alikosa jibu.
“Unahitaji nini?” aliuliza, kipindi hiki kidogo akatoa sauti iliyokuwa na ujasiri.
“Nilitaka nikwambie kitu kimoja tu kwamba nipo hai, nimeishi maisha ya tabu mpaka kuwa hapa, niliteseka, nililia usiku na mchana, niliumia kwa ajili yako. Jua kwamba sikufa, nipo hai, ninapumua kama unavyopumua,” alisema mtu aliyesikika upande wa pili maneno ambayo yalimchanganya kabisa Mchungaji Gideon.
“Wewe ni nani?”
“Mzimu Unaotabasamu. Mzimu unaotafutwa kila kona katika dunia hii,” alijibu mwanaume huyo.
Hapo ndipo Mchungaji Gideon akamfahamu mtu huyo. Alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa wakitafutwa kwa nguvu kubwa duniani kote huku maofisa wa Kijasusi wa CIA wakiwa mstari wa mbele kabisa. Katika orodha ya watu mia moja waliokuwa wakitafutwa kwa udi na uvumba wa kwanza kabisa alikuwa mwanaume huyo. Hakujulikana, hakukuwa na mtu aliyejua sura yake ilifananaje lakini ndiye mtu aliyekuwa akiua watu wengi kila siku duniani.
Alijulikana kama The Smilling Ghost kwa maana ya Mzimu Unaotabasamu, na kwa kuwa hakuwa akijulikana jina lake, hata kwenye orodha hiyo ya CIA waliliandika jina hivyohivyo japokuwa hawakujua mwanaume huyo alifananaje na hakukuwa na mtu aliyejua sababu iliyompelekea kufanya mauaji katika siku ya Jumapili.
“Leo ni Jumapili, huu ni usiku wa kuamkia Jumapili, ina maana unataka kuniua?” aliuliza Mchungaji Gideon huku akianza kuingiwa na hofu kwa mara nyingine.
“Hapana. Nimekupigia simu kukwambia kwamba leo ndiyo siku maalumu ya Mzimu Unaotabasamu kukamatwa. Nahisi baada ya kukamatwa, hakutokuwa tena na mauaji kwa Jumapili ya leo,” alisema mwanaume huyo maneno yaliyozidi kumchanganya zaidi Mchungaji Gideon.
“Unamaanisha nini?”
“Umeangalia stoo?”
“Hapana! Kuna nini?”
“Umeangalia bafuni?” aliendelea kuuliza.
“Hapana. Kuna nini?”
“Hata hukujiuliza kwa nini mbwa wako leo habweki?” aliuliza mwanaume huyo.
Swali hilo lilimfanya Mchungaji Gideon kujiuliza kuhusu mbwa huyo. Hakujua ni kitu gani kilikuwa kimetokea, kila siku usiku mbwa wake aliyempa jina la Bobby alikuwa akibweka mno kuhakikisha nyumba yake inakuwa salama mbali na kamera ndogo za CCTV alizokuwa amezifunga ndani ya nyumba yake.
Siku hiyo alikuwa kimya kabisa, alishangaa, alijiuliza maswali yasiyokuwa na majibu lakini alikuwa na uhakika kwamba mwanaume aliyekuwa akizungumza naye alifahamu kila kitu. Baada ya kujiuliza kuhusu mbwa huyo, akajiuliza kuhusu huko stoo na bafuni alipokuwa ameambiwa, alihisi kulikuwa na kitu, alihisi kabisa kwamba mwanaume alikuwa amefanya jambo.
“Unataka nini?” aliuliza kwa ukali kidogo.
“Polisi wanaingia hapo dakika chache zijazo. Hakutokuwa na kitu chochote watakachokijua zaidi ya kufahamu kwamba wewe ndiye Mzimu waliyekuwa wakimtafuta kwa miaka kumi na tano, dunia itajua kwamba wewe ndiye mwanaume aliyekuwa akiua kila Jumapili, itajua kwamba wewe ndiye uliyemuua waziri mkuu wa Uingereza, mwanamitindo, Amanda Posh, Mwanamuziki Michael Turner, kwa kifupi, dunia nzima itajua kwamba wewe ndiyo mimi,” alisema mwanaume huyo na kukata simu.
“Halo..halo..halo..” aliita Mchungaji Gideon lakini simu ilikuwa imekatwa.
Mwili mzima ulikuwa ukitoka jasho, hakutaka kuchelewa, ilikuwa ni lazima kwenda bafuni na chooni kuona ni kitu gani kilikuwa kimetokea huko. Yeye na mkewe, kwa kasi ya ajabu wakaanza kuelekea bafuni, walipoufikia mlango na kuufungua, hawakuamini walichokiona, maiti ya mwanamke ilikuwa sakafuni, ilichomwa visu vinne kifuani, damu zilikuwa zikitoka huku kwenye paji la uso kukiwa na alama ya msalaba, yalikuwa ni aina ya mauaji yaleyale aliyokuwa akiua mtu huyo aliyekuwa akitafutwa.
Mkewe akaanza kupiga kelele kwa woga, hakuamini alichokuwa akikiona, moyo wake ulikufa ganzi na mwili kumtetemeka. Mchungaji Gideon akachanganyikiwa, hakujua ni kitu gani kilikuwa kimetokea mpaka maiti ile kuletwa ndani ya nyumba yake.
Akatoka na kueleka stoo, alipoufikia mlango na kuufungua, akakutana na maiti nyingine ya mtoto iliyokuwa sakafuni. Nayo ilichomwa visu viwili kifuani na kwenye paji la uso kulikuwa na alama ya msalaba, ilikuwa ni aina ya mauaji yaleyale aliyokuwa akiyafanya Mzimu.
“Mungu wangu! Kwa nini mimi?” alijiuliza na kutoka ndani.
Akaelekea katika banda la mbwa, alichokikuta huko ni maiti ya mbwa wake ikiwa chini. Aliuawa kwa kuchomwa visu mfululizo.
Machozi yakaanza kumtoka, hakuamini. Hata kabla hajafikiria ni kitu gani kilikuwa kimetokea, akaanza kusikia mlio ving’ora vya polisi wakija kule ilipokuwa nyumba yake, akazidi kuogopa.
Haraka sana akarudi ndani ya nyumba yake, akamkuta mkewe akiendelea kulia, hakujua ni kitu gani alitakiwa kufanya. Wakati akimchukua mkewe kwa ajili ya kumpeleka chumbani, polisi nao wakapiga teke geti kubwa na kuingia ndani huku wakiwa na bunduki mikononi mwao, tena wengine walikuwa wale polisi waliokuwa na silaha nzito ambao walikuja na gari lao lililoandikwa kwa maandishi makubwa yaliyosomeka S.W.A.T.
Hawakuingia kistaarabu, wakavunja mlango wa sebuleni na kuingia ndani. Walipofika, wakamkuta Mchungaji Gideon akiwa na mkewe, walikuwa wamekumbatiana chini huku wote wakilia kama watu waliokuwa wamefiwa.
“Mpo chini ya ulinzi! Nyanyueni mikono juu,” alisema polisi mmoja huku wakiwanyoonyeshea bunduki, wakatii na kufanya hivyo.
Kabla ya kufungwa pingu, polisi wale wakaanza kuangalia ndani ya nyumba hiyo, tena moja kwa moja wakaelekea stoo na bafuni na kuzikuta maiti hizo, yaani walikuwa kama watu ambao walijua maiti zilipokuwa. Wakawafunga pingu na kutoka nao ndani ya nyumba ile.
“Hatukuua! Hatukumuua mtu yeyote! Mimi ni mchungaji, mnanijua, mimi ni mpaka mafuta wa Bwana, sikumuua mtu yeyote yule,” alijitetea Mchungaji Gideon huku akiwaangalia polisi hao.
“Tumekutafuta sana. Kumbe mchungaji anayeaminika duniani, mpaka mafuta wa Bwana, anayewahubiria watu Neno la Mungu ndiye Mzimu Unaotabasamu tunayemtafuta! Mungu wangu! Kweli dunia imekwisha,” alisema polisi mmoja huku akionekana kushangaa.
Hakukuwa na mtu aliyemsikiliza, wakawachukua na kuwapeleka katika kituo cha polisi hapo kilichokuwa Manhattan jijini New York na kuwatuliza huko huku wakitakiwa kusubiri mpaka asubuhi itakapofika na mambo mengine ya kimahakama kuendelea.
Kukamatwa kwake haikuwa siri hata kidogo, usiku huohuo taarifa zikaanza kupelekwa sehemu mbalimbali kwamba hatimaye Mzimu Unaotabasamu alikuwa amekamatwa. Watu wengi walishtuka na kushangaa baada ya kupewa taarifa kwamba Mzimu wenyewe alikuwa mchungaji Gideon aliyekuwa na kanisa kubwa lililokuwa na washirika zaidi ya milioni moja duniani kote.
Ilipofika majira ya saa 10:15 alfajiri, Mchungaji Gideon akatolewa kutoka katika chumba alichokuwemo na kupelekwa katika chumba kingine kwa ajili ya kufanyiwa mahojiano. Muda wote alikuwa akilia huku akisisitiza kwamba hakuwa muuaji bali kulikuwa na mtu aliyekuwa ameua na kuzipeleka maiti katika nyumba yake.
Hilo halikusikilizwa. Alipofikishwa ndani ya chumba cha mahojiano, akakalishwa kwenye kiti na kuanza kuhojiwa. Muda wote alikuwa akilia, aliikunja mikono yake kama mtu aliyekuwa akisali, mara kwa mara alikuwa akifanya ishara ya msalaba lakini yote hayo yalionekana kama unafiki machoni mwa polisi waliokuwa ndani ya chumba hicho.
Wakaanza kumuuliza maswali kadhaa. Kila swali alilokuwa akiulizwa, Mchungaji Gideon aliwaambia kwamba hakuwa ameua na hakumfahamu mtu aliyekuwa amezileta maiti zile nyumbani kwake kwani alipigiwa simu na mtu aliyejitambulisha kwa jina la Mzimu Unaotabasamu na kuzipeleka maiti zile nyumbani kwake lakini si yeye aliyekuwa amefanya mauaji hayo.
“Fungua hiyo bahasha,” alisema mwanaume aliyekuwa akimuhoji huku akimpa bahasha kubwa ya kaki na kumwambia afungue.
Haraka sana akaifungua. Humo akakutana na picha mbili zikimuonyesha yeye akiwa amesimama nje ya nyumba moja huku mkononi akiwa ameshika kisu kilichokuwa na damu, na ndani ya nyumba hiyo kulikutwa maiti mbili za wanawake ambazo zilichomwa visu vifuani na kuwekewa alama ya msalaba katika paji la uso la kila mmoja.
“Huyu ni nani?” aliuliza polisi yule swali ambalo Mchungaji Gideon alishindwa kabisa kulijibu kwani kila alipokuwa akiiangalia sura ile, alikuwa yeye ila hakukumbuka kama kulikuwa na siku aliwahi kwenda kufanya mauaji yoyote yale.
“Huyu ni nani?” aliuliza polisi kwa sauti ya juu. Badala ya kujibu, Mchugaji Gideon akaanza kulia kwa sauti kama mtoto mdogo huku akisisitiza kwamba hakuua.