Baada ya Miaka 2, natamani Ndoa yangu ivunjike

Baada ya Miaka 2, natamani Ndoa yangu ivunjike

Ndoa ina miaka miwili, vipi kuhusu uchumba wenu kabla ya ndoa ulikuwa na muda gani?
Uchumba Sio ndoa unaweza kaa hata miaka 10 uchumbani ndoa ukaa mwezi.
Uchumba ni maisha feki ndoa ni maisha halisi huwezi feki thus ndoa nyingi chali.
Sababu kwenye ndoa hakunaga maigizo kama ulikua unaazima magari,nguo,bata, itajulikana.
Huwezi ijua tabia ya mtu bila kuishi nae.
 
Uchumba Sio ndoa unaweza kaa hata miaka 10 uchumbani ndoa ukaa mwezi.
Uchumba ni maisha feki ndoa ni maisha halisi huwezi feki thus ndoa nyingi chali.
Sababu kwenye ndoa hakunaga maigizo kama ulikua unaazima magari,nguo,bata, itajulikana.
Sawa mkuu
 
Tulia wewe, mwanaume akiingia kwenye ndoa ndio hupata zaidi vishawishi unakuta mke ndio ametoka uzazi amejiachia balaa hapo unaandika ila ukute umevaa mikanga tupu na minywele umeiachia tu.

Tulia nawe jikague vizuri, haiwezekani ndoa ya miaka miwili unaanza kulalamika mtu anakucheat. Mpe mambo jipake poda nukia oga osha mashuka, nyumba ing'ae acha kumsemesha upuuzi kila saa na acha kumkaguakagua simu yake na kumdadisi alikuwa wapi instead anza kumpa pole kwa kazi na kumwambia maneno mazuri.

Ongea nae mambo yanayokuudhi kwa upendo na upole na mfanye ajisikie aibu kwa anayoyafanya pia uasiache kumkumbusha viapo vyenu kanisani na usiache pia kumuombea kwa Mungu.

Pia ongea nae kwa upole kuhusu hisia zako kwake jinsi unavyompenda na namna anavyokuumiza kwa matendo yake. Mfahamishe kwamba wewe ni mwanadamu haupendi kujuta kuolewa nae na haupendi ifike pahala muachane au mvunje ndoa sababu ambazo anaweza kuzuia yeye mwanaume wako.

Tell him your feelings dewply kwa upole. Tafuta sehemu mtoe out na umwambie unataka kukaa nae faragha ya dinner. Mjadili bila yeye kunywa pombe ili aelewe maana akilewa atakuchukulia poa.

Jaribu kumuelezea namna ambavyo pombe inamzidi pia angalia kama inasababishwa na stress za kazi au nini? Ongea nae acha kukimbilia kutafuta ushauri mwingi maisha ni yako wewe.

Pambana ndoa sio Big Brother House. Fikiria mwanao je ataishi na wababa wangapi? Unamuacha huyu utakutana na malaika? Wanaume ndio sisi sisi tu hatuna tofauti sana we just sin differently.

Komaa na ndoa we tafuta jamaa akuliwaze kimyakimya huku unatunza ndoa kwa maana kuishi pamoja ili mtoto akue mazingira salama.
Duuu,ushauri wako nibora sana mkuu,afuate huu ushauri,unaweza msaidia sana,
 
Hii kitu inakata stimu yakuishi na mwanamke ,kelele ndani ya ndoa hasa kwa wanawake kujidai ndio wenye haki sana nakutendewa mema wao tuu huathiri akili ya mwanaume ktk ndoa,jct imagine kila kukicha mwanmke anahitaji kutendewa mazuri yy tu,hajawahi kuwaza hata kukununulia kitu chochote kutokana namapato yake,hawazi kukutendea mambo yanayoweza kuimarisha mahusiano wala hafanyi jitihada zozote kujenga mahusiano bora bali yy anajiweka upande wa hakimu/wakili kukosoa utendaji wako ktk kuendesha familia,daima anakudai matumizi nakukupigia makelel hujatimiza hili mara hujakamilisha lile..daahh hayo yote nichanzo cha msongo wamawazo kwa mme hivyo kutafuta furaha ktk ulevi.
Hakuna mwanaume anaeweza ishi na mwanamke anaerapu.
Wao wakirap wanatoa sumu zile sumu ni hatari sana kwa afya ya akili ya mwanaume.
Wanaume wote wasio na nuru study wote ndani moto.
Hapa ni ishu ya nyota kutobalance yaani kukosea kuoa.
Ukioa mwanamke Simba au moto wewe ni baridii au kondoo usipotoka nduki utawahi kufa kwa stress,kisukari, pressure,sononona sababu zile toxins toka kwa mwanamke mrapaji.
Mwanaume yeyeto ili apate pesa anahitaji mwanamke asiyerapu.
Kelele ufukuza malaika wa pesa ndani.
 
Mkuu hivi unaelewa maumivu ya kusalitiwa ukiwa kwenye ndoa?
Utaweza uke wenza kweli? Watu wanaolewa hadi wa 4.
Athumani alioa wake 3, pembeni anamchepuko naye ana mimba licha ya hivyo. Ana wanawake wengine na wote wanajuana.
Fuatilia interview ya Athuman na wake zake kwenye channel ya Youtube
 
"Familia anahudumia vizuri tu" SIMAMIA hapa.

Ukiondoka utamtafuta na hutampata tena
analewa usiku kucha analala na ma bar maid, most likely bila mipira
akimpa ukimwi ?
 
Kuna watu humu (ke) watawahi kukaba nafasi kama wakijua ameshatoka kwenye ndoa! Watapeleleza hadi wampate!! Sikubaliani na ulevi wake, lakini nampongeza kwa kuhudumia vizuri familia yake pamoja na ulevi wake!!
Yaani uambukizwe magonjwa kisa unaogopa ukiondoka atachukuliwa na mwingine??? hii akili ya wapi...
 
Mtengeneze mumeo uyo ndo uliemridhia kama huwezi katafute mwingine Alibaba au Ebay
 
Mpe uroda asubuhi mchana na jioni halafu mpe Kama vile sio unalala Kama gogo halafu utegemee asichepuke.
Mpe hicho kitu afaidi. Kumbania bania ndio maana anakwenda kwa hao ma bitch wanaompa yote.
Halafu epuka kua argumentative and fault finding.
Anzisha topic anazopenda atakaa akusikilize. Sio kulalamika 24/7
Wanaume tunapenda peace and uroda.
Ushauri mwingine wakufata nihuu.
 
Ukisha achana nae akipata atakae mueka sawa itakuaje?
Wewe bado mdogo jaribu kumuelewesha vizuri, kama familia anahudumia vizuri hakuna shida.
Nenda kanisani kwa padre aliewafungisha ndoa muelezee yanayokusibu nadhani ataitwa na wazee wa kanisa tu.
Akishindwa na hapo achana nae tunawahitaji single mother mtaani sana tu.
Yaani,familia anahudumia vizuri. Af tena, anatamani kuivunja ndoa. Kbla ya kulaumu mwanaume,inaonekana we mwanamke hujafundwa,af pengine malezi ya mama huna.
 
Uliomba mungu upate wa kufanana nae au ulijisemea kuwa 'utambadilisha pole pole'?. BTW pole. Hii ndio sababu inanifanya nisioe maana nikiangalia mienendo yangu ya kuondoka ijumaa na kurudi jpili sijui ni binti gani atafanikiwa kunibadili.
 
Tuambie na wewe mabaya yako.

Tuanzie hapa kwanza, maana huwenda wewe ndo chanzo a.k.a vuvuzela jamaa anaona michosho kukaa ndani na wewe bora akeshe bar!

Mnazinguwa sana nyie sometimes. Kesi zenu zinasikilizwa sana lakini mna matatizo mengi sana wengi wenu.

Najuwa kwa nini umetaja umri wako.....unadhani huo umri utapata mme mwingine kwamba hujazeeka, WANAUME WOTE TUKO HIVYO utofauti ni madhambi tuu.

Achana nae apate mke mtulivu halafu usikie jamaa ametulia hata wewkend hatoki ananywea bia nyumbani ndo utaanza kulalama.

Mrekebishe kwa kujirekebisha wewe,alikuoenda ndo maana akakuoa, bila shaka ulijuwa anakunywa,ukakubali lakini umekosa mbinu za kumfanya anywe kistarabu unavyotaka wewe.
 
Ni sababu ndogo sana mleta mada,
Hazitoshi kabisa kuvunja ndoa.

Ni bahati mbaya sisi vijana tumekua wepesi sana tofauti na baba na bibi zetu, wao walipitia mengi hayo ya kwako ni madogo mno!
Lakini walistahili kipindi cha mpito kikapita, sasa wewe miaka miwili ndio una fika hitimisho la namna hiyo?
Tafakari.
 
Kuna jamaa yetu ni mlevi kupindukia,
Alishajua kuwa tunamsema vibaya kwa ulevi wake,

Kuna siku tuko na shemej yetu jamaa alifunguka mazima kuhusu tabia ya mkewe,
Mkewe aliwai toka na shem wake wa tumbo moja,

Jamaa akamgeuka mkewake unakataa!?

Dah yule shem akainamia chini kimya,

Jamaa akaturudia na sisi akatuuliza ni nani anaweza vumilia hili tukio?

Tukabaki midomo wazi,

Mambo ya ndoa bana usikilize pande zote, ila hii ya upande 1, ni kuchangamsha genge,

Mlianza vizur iweje sasa?
Tena huenda huyo shemejie kashakula mara kibao
 
Ndoa sio gereza hapo unatafuta ukimwi ili uishi na Sonona?

Ndoa ni vita kwani?
 
Natamani kuvunja ndoa yangu.

Habari zenu wakuu, natumai mko poa. Nimekuja na nia ya dhati kutafuta ushauri kuhusu jambo langu ambalo linanitatiza.

Mimi ni msichana mwenye umri chini ya miaka 30. Nina mtoto mmoja wa kiume. Nimekuwa katika ndoa na mume wangu kwa takriban miaka miwili sasa.

Sababu za maamuzi yangu ni kama ifuatavyo:

1. Uchepukaji uliokithiri: Huyu mume wangu amekuwa akinihadaa sana. Sijawahi kuona kitu kilichoniumiza zaidi ya kugundua kuwa anatoka na wanawake wengine. Ameomba msamaha kila mara ninapomfumania, lakini bado anarudia tabia hiyo. Kesi zetu zimekuwa nyingi kwa wazazi na nadhani wamechoka kutusuluhisha.

2. Ulevi uliopitiliza: Mume wangu ni mlevi sana. Kurudi nyumbani asubuhi ni jambo la kawaida kwake. Nimeshazungumza naye na kumweleza jinsi ninavyojisikia kuhusu tabia yake ya kunywa kupindukia, ingawa anahudumia familia vizuri. Lakini, hupati muda na familia kabisa. Inanidhalilisha sana kwa sababu tunakaa na mdogo wake nyumbani, hivyo najihisi vibaya sana anaporudi asubuhi.

Ndoa yetu imefungwa kanisani na tumekuwa tukiishi pamoja kwa miaka miwili tu. Nashauriwa nifanye nini kuhusu maamuzi yangu haya, maana sijisikii furaha kabisa katika ndoa hii. Na mimi ni mchanga sana kuishi kama hivi hadi kifo kitutenganishe.
yaani kuchepuka na kunywa pombe tu?

be serious wewe!
 
Back
Top Bottom