Baada ya Kumalizana na CCM, Shigongo kaibuka na hii

Baada ya Kumalizana na CCM, Shigongo kaibuka na hii

Mimi mwananchi ambaye ni mlipa Kodi mwaminifu na ambaye nahitaji kodi inayokusanywa kwangu na kwa baadhi ya ndugu zangu watanzania,ningependa rais wa hii nchi afanye vitu ambavyo tunaweza kunufaika moja kwa moja na kwa kiwango kikubwa.Ndege ambazo ananunua zinawasaidia watu wachache moja kwa moja kuliko watu wengi ambao nauli tu ni shida.Fedha hizo zingetumika kununua dawa mahospitalini,kuboresha Huduma mbalimbali amb mtu wa chini na wa juu wanaweza kufaidika.Tuache unafiki,akiondoka Magufuli akaingia rais mwingine na akaanza kuponda mambo mabaya anayoyatenda raid,bado tena watu watasema tumepata mkombozi,ila kwasasa anashangiliwa.
 
Kutoka mtaa wa pili kwenye ukurasa wa FB nimekutana na hii promo, Kwa mtazamo wangu tu hii hali ya kutuambia tuvumilie mpaka leo hii ni miaka 50.Sio fair kabisa! Yaani mtu kazaliwa babako anavumilia, unazaliwa wewe unaendelea kuambiwa Vumilia! Huu uvumilivu utaisha lini!??

6b3fa130a25805f68fb8f63ab720ecdf.jpg
"Hapa bombardier tu"
 
Mwizi mwizi Tu hata avae suti atabaki kuwa mwizi

Sent from Microsoft Lumia 950xl Lte
 
Wakati mwingi si kupinga kila kitu, hoja ni muhimu sana... Ndege ni biashara, faida inayopatikana kupitia biashara hii ya ndege inaweza kujenga kituo cha afya na babu yako akatibiwa, pia hiyo faida inaweza kununua ambulance na kumchukua babu yako kwa haraka kwenda kituo cha afya cha karibu.. Sio lazima babu yako apande hiyo dream liner....
well said
 
Hapo hamna kosa kabisa.Kaeleza Tanzania tulikuwa tunaziona hizo ndege za kimataifa Sasa tunaiona yetu.Kwa upande mwingine hizo kampuni za ndege zinafurahi kutangazwa bure.Huwezi huwa Labda tutakuwa nao ubiya.

zipi hizo za kimataifa zile za kukodi au zipi hizo , tanzania hatujawahi kuwa na ndege za kimataifa mkuu zile hazikuwa za kwetu zilikuwa za watu
 
Tatizo la baadhi ya sisi watanzania ni kuamua kujitoa ufahamu na kuona kila kitu kinachofanywa na serikali kwa nia njema na yenye malengo ya muda mfupi au hata mrefu hakifai. Tulikuwa na awamu iliyokuwa haichukui hatua kwa wakati tukaongea sana... imekuja inayochukua hatua papo hapo tunaongea vile vile....hivi tunataka nini kifanyike ndipo tupongeze? Uamuzi wa kununua hizi ndege bila ya kujali kama mimi na wewe tutazipanda au hapana sio kigezo cha kusababisha kubeza hata kidogo. Kama hatuelewi manufaa ya moja kwa moja au hata yatokanayo na hizo ndege ni vizuri tuombe kujulishwa na sio kuponda tuuu bila kujua tunachokiponda ni kipi. Serikali imekuwa kwa muda mrefu ikikosa mapato yatokanayo na biashara ya usafirishaji kwa njia ya anga kwa kutokuwa na ndege zake zenye uwezo wa kutua viwanja mbalimbali ndani na nje ya Tanzania ili kuweza kushawishi watalii wakizipanda wawe na uhakika watafika Tanzania na kutuingizia fedha za kigeni, ambazo sasa iwe ulimudu kuzipanda hizo ndege kwenda kwenu au hukumudu lakini mapato yake yataiwezesha serikali kukutimizia wewe mambo mengi mengi tu unayoyahitaji serikali ikufanyie kama vile kujenga miundo mbinu, huduma za kijamii, ruzuku za pembejeo, kilimo, mifugo, mikopo kwa vikundi mbalimbali n.k Bravoo serikali ya awamu ya tano.
 
Dah...acha uboya bana...umesikia watu wanapanda bure?....ile nauli inayolipwa pale...serikali inachukua sehemu..kisha Babu yako anunuliwa dawa[emoji13] [emoji13] [emoji13]
Ni hospitali ipi inatoa dawa bure,ukiachaARVs za msaada?
 
Jibu swali Kwa point na siyo kupayuka kilumumba Lumumba, Hizo ndege zimenunuliwa Kwa jasho letu watanzania, sasa hujajibu sisi tuliopo huku porini tutafaidikaje?

Piga huduma kwa wateja namba 112 ikulu usaidiwe
 
Jibu swali Kwa point na siyo kupayuka kilumumba Lumumba, Hizo ndege zimenunuliwa Kwa jasho letu watanzania, sasa hujajibu sisi tuliopo huku porini tutafaidikaje?
Kama upo porini lima upate hela uje upande ndege kwani umezuiliwa? ?
 
Hivi unafikiri kunufaika na hizo ndege ni lazima uzipande ndio iwe umefaidika nazo? shughulisha kichwa japo kidogo tu mkuu.
Mkuu ungeanza kukishughulisha kwanza wewe ndo unishauri na mimi...ungekuwa unakishughulisha usingekuwa kijana wa lumumba
 
Back
Top Bottom