Baada ya Dkt. Salim, Dkt.Tulia atairudisha nchi katika unguli wa diplomasia ya kimataifa. Tumuombee, anaweza kuwa Katibu mkuu ajaye wa UN

KARLO MWILAPWA

JF-Expert Member
Apr 10, 2019
2,590
4,601
Kwanza, ninampongeza sana Spika Dkt.Tulia kwa ushindi wa kishindo kama Rais wa IPU, kama Taifa linajivunia juhudi na jitihada zake za kuitangaza nchi kimataifa.

Spika Tulia au tumuite Rais wa IPU ni jasiri na mpambanaji na historia yake inajieleza vema. Kwa ufupi ni mwanamke wa shoka na yuko "very determined" maana sio rahisi kufika alipofika kama ni mtu wa kukata tamaa na kukubali kushindwa kabla hujaanza shindano.

Safari yake ya ujasiri inaanza pale jimboni Mbeya kwenye kiti Cha Ubunge kwenye uchaguzi mkuu wa 2020. Jimbo la Mbeya ni Moja ya majimbo yaliyokuwa na ushindani mkubwa sana lakini alijitoa na akafanikiwa kushinda na mpaka sasa hakuna mwanaume wala mwanamke wa kumtia Tulia kwenye Ubunge wa Mbeya. Amefanya mengi makubwa Kwa kipindi kifupi.

Na hili la kugombea Urais wa IPU Kwa Imani na matumaini ya kushinda na kufanikiwa kushinda ni kielelezo Cha kuthibitisha uwepo wake ni baraka kubwa Kwa nchi yetu Kwa siku za mbeleni.

Hapa ndipo ishara kuu zinaonekana mbeleni kwamba huyu si mtu wa kawaida hata kama sisi watanzania tuna tabia ya kuwachukulia watu kawaida. Spika Tulia ana roho ya kufanikiwa na kushinda kwa kila anachofanya. Roho hii itaendelea kufanya kazi kwa mengine mengi juu yake.

Wakati Mhe.Rais akifungua tovuti ya historia ya Dkt.Salim alisema tumerudi nyuma kwenye diplomasia uwe unguli tuliokuwa nao miaka ya 2000 kurudi nyuma haupo tena,tunahitaji kulibadili hili.

Unguli unaosemwa na Rais Samia ni kupitia Kwa Dkt.Salim, mtanzania aliyekuwa na historia ya kusisimua ambaye kama sio fitna basi angeukwaa ukatibu mkuu wa Umoja wa Mataifa.

Namtazama Spika Tulia kama Dkt.Salim wa leo ambaye atabeba jukumu la kuipaisha diplomasia ya nchi yetu kimataifa. Namtazama Spika Tulia mtu sahihi Kwa kizazi Cha Sasa kuturejeshea unguli wetu kwenye diplomasia ya kimataifa.

Zaidi, namtazama kwenye nafasi kubwa zaidi za kimataifa. Alishindwa Dkt.Salim kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa naamini njia ipo wazi Kwa Dkt.Tulia kuja kuwa Katibu mkuu wa umoja wa Mataifa Kwa uwezo wake Mwenyezi Mungu. Tunakuombea na Taifa linajivunia wewe.

Sasa, Taifa linakutazama kama nguli wa diplomasia za kimataifa wa kizazi cha leo na lina matarajio makubwa kutoka kwako.
 
Kwanza, ninampongeza sana Spika Dkt.Tulia kwa ushindi wa kishindo kama Rais wa IPU, kama Taifa linajivunia juhudi na jitihada zake za kuitangaza nchi kimataifa...
Dr Tulia ni ushuhuda wa matendo makuu ya Mwenyezi Mungu
Huyo ni jizi la kura kama majizi mengine, na hicho cheo hakina maana yoyote. Wangalau kwake ni cheo Cha maana, maana ameweza kukipata bila wizi wa kura. Lakini ni cheo kisicho na tija yoyote. Kingekuwa Cha maana asingeweza kukipata.
 
Hawezi kufikia hata robo ya Dr. Salim AS... Tulia ni jinga fulani hivi... Akiongea ni kama anatukana
 
Kwanza aishukuru Simba sc kwakuwa ndio imemfikisha kujulikana kimataifa kwani waliompigia kura ndio wale mashabiki wa kimataifa wanaoipenda Simba sc(akili za wkend night)
 
Kwanza, ninampongeza sana Spika Dkt.Tulia kwa ushindi wa kishindo kama Rais wa IPU, kama Taifa linajivunia juhudi na jitihada zake za kuitangaza nchi kimataifa.

Hapa ndipo ishara kuu zinaonekana mbeleni kwamba huyu si mtu wa kawaida hata kama sisi watanzania tuna tabia ya kuwachukulia watu kawaida. Spika Tulia ana roho ya kufanikiwa na kushinda kwa kila anachofanya. Roho hii itaendelea kufanya kazi kwa mengine mengi juu yake.
Naunga mkono hoja, Dr. Tulia sio mtu wa kawaida!, angalia tarehe ya bandiko hili, uone sisi watu wa Sauti za Ndani, tuliambiwa nini na lini kumhusu Dr. Tulia Akson. Voices from within: Nimesikia sauti, Dr. Tulia Ackson ndiye Spika ajaye! Sauti hiyo imenieleza Ndugai, japo atatamani aendelee lakini...

Angalia hapa uone Dr. Tulia anakokwenda
Ujumbe wangu kwa Rais Samia- Naona umemuona Tulia. Kusema kweli mwanamke mwenzako anaweza. Mjenge vizuri, mpe exposure, mjenge aendeleze haya mazuri yote unayoyafanya sana hasa katika kujenga uchumi imara kupitia sekta binafsi pale utakapomaliza uongozi wako. Mpe exposure apate kujifunza vizuri geopolitics. Na mwisho ikikupendeza chama chako kimpe kijiti akapeperushe bendera ya chama 2030.

Asanteni
Lord Denning
Kigali
Mkuu Lord denning , kwanza naunga mkono hoja Dr. Tulia awe mgombea wa urais wa CCM mwaka 2030.

Pili kwa vile Rais Samia alishauri 2025, twende na mgombea Mwanamke, japo wengi wanadhani Mwanamke huyo wa 2025 ni lazima awe Mama Samia, kwasababu ndio awamu yake ya pili, mimi pia Watanzania, tuunge mkono 2025 ni zamu ya Mwanamke, ila sio lazima awe yeye bali yule aliyepangiwa na 'YEYE', kama ni yeye aliyepangiwa, then ni yeye!, hii maana yake 2025 Rais Samia is most likely but not necessarily ni lazima, yeye!, sio lazima, Mwanamke huyo, anaweza kuwa mwanamke mwingine yeyote, ila ukimuondoa Rais Samia as the No. 1 top lady in Tanzania, Dr. Tulia is the second!, hivyo 2025 anaweza kuwa ni Dr. Tulia!.

Kisha tembelea uzi huu, Voices From Within: Japo 2025 Tumepanga Twende na Mwanamke, 2025 Mama Akabidhi Kwanza Mwanamume, Kisha 2030 Ndipo Aje Mwanamke angalia nilichosema kumhusu Dr. Tulia na uchaguzi wa 2030
Na kipindi hicho cha 2025- 2030 ndipo sasa sasa tufanye grooming ya Mwanamke atakaye kuja kugombea urais wa JMT kwa 2030, na kwa maoni yangu, Mwanamke huyu sii mwingine yeyote zaidi ya Dr. Tulia Akson Mwansasu, Spika wa sasa wa Bunge la JMT.
Hivyo kwa hoja yako hii ya Dr. Tulia kuwa mgombea urais wa JMT kwa tiketi ya CCM mwaka 2030, tunafanana!.

P
 
Pongezi Dr Tulia, nina hakika utatufaharisha watanzania kwenye wsdhifa wako wa kimataifa.
 
Back
Top Bottom