Azam TV Limited yaingia mkataba wa kuonesha Matangazo ya Ligi Kuu kwa miaka 10. Mshindi misimu mitatu ijayo kulamba bonus Tsh 500m

Tunaongelea Full Package 225 billion bila kuangalia hiyo miaka 10 yenyewe tutakuwa wapi katika Ramani ya Soka na Mtazamo wa Soka lenyewe kwa Mapana yake.
Kama zabuni ilitangazwa, na yeye ndo akashinda kwa nn tusimpongeze?

Ukwel n kwamba wamejitahid kwa kiasi chao, tusubir iishe tuone tutakuwa wapi, na hii inaweza kuwa n chachu ya kuipandisha thamni ligi ili kuvutia wawekezaji wengine wenye pesa ndefu.
Kwangu mm namuona kama ametake risk kubwa kwa ninavouona mpira wetu.
 
Merchant za klabu Pekee kwa Yanga na Simba Tayari ni Pesa kubwa Sana..
Angalia Simba Day.....
Mwananchi Day .........
Viingilio + Mauzo ya Product zao + Wauze haki yakuonyesha tu hizi Tamasha kwa Tv wanazo zitaka watapa Fedha kiasi Gani.??
Na jiulize tofauti na Simba na yanga ipi event kubwa na kuingiza pesa kwa soka la hapa kwetu?.
Kuna timu zinasubir mechi za Simba na yanga kama chanzo kikubwa cha mapato.
Sasa kwa mantiki hiyo ni kwamba bado hatuna fan base ya kutosha kwa vilabu vidogo ambavyo hata mishahara tuu n tataizo.
 
Kama zabuni ilitangazwa, na yeye ndo akashinda kwa nn tusimpongeze?

Ukwel n kwamba wamejitahid kwa kiasi chao, tusubir iishe tuone tutakuwa wapi, na hii inaweza kuwa n chachu ya kuipandisha thamni ligi ili kuvutia wawekezaji wengine wenye pesa ndefu.
Kwangu mm namuona kama ametake risk kubwa kwa ninavouona mpira wetu.
Kuna Haja Gani ya Kuingia miaka10, kwa nn wasiingie kwa term ya 5yrs then 5yrs Tena? Je thaman ya Fedha ikipolomoka au kukiwa na fiscal cliff Unanilaumu Nani?
 
Kwa nature ya hii biashara (Haki za kuonesha mpira) ilivyo ni ngumu sana investors wawili kuexist kwa pamoja..Lazima mmoja afe..kwasababu

Market bado ni dogo sana kuhitaji two suppliers...Gharama za kuendesha biashara zinakuwa juu kuliko faida mtakayogawana..chukulia mfano kwenye soko la ving'amuzi tu..kuna kampuni zingine naamini zinapata faida ndogo sana au inawezekana zinapata loss kwasababu tayari soko ni dogo halitoshi watu wawili..Kuna aina za ving'amuzi huwa nazisikia tu redioni ila hadi leo sijawahi kuviona vinatumika majumbani..vipo ila wateja ni wachache sana.

sasa Ukimuweka AZAM na DSTV kwa ligi moja ya bongo na ambayo market 99.5% ipo bongo lazima wagawane faida na mmoja lazima aanguke maana cost of production ni kubwa kuliko market share.

Najua utakuwa unajiuliza kwanini kuna TIGO, VODA, AIRTEL, HALOTEL, ZANTEL n.k at the same time na wote wanapata faida...Jibu ni rahisi tu kuwa market ni kubwa (zaidi ya watu 30m wanatumia simu) na unakuta mtu mmoja anamiliki line zote...ila watu wanaomiliki ving'amuzi viwili kwa pamoja ni wachache sana kutokana na per capital income za raia.

So, kwa hii biashara ya kuonesha mpira wa ligi ya bongo (taking into consideration the current situation) ni ngumu sana sana sana DSTV na AZAM kuonesha kwa pamoja...Kwanza kati yao hakuna atakaekubali...Kitu pekee ambacho watakubali kufanya ni kugombania tender tu ila sio kuonesha kwa pamoja..

Ndio maana watu wanalalamika miaka 10 ni mingi sana ilibidi iwe michache ili kutoa nafasi kwa bidders kugombania tenda na TFF pamoja na vilabu kuzidi kupata masilahi mazuri. Hii ya mtu mmoja kumiliki soko kwa 10yrs inaua ubunifu.

swali fikirishi kidogo kwako mkuu:

Yule MO kama mjasiriamali, unadhani hajaiona fursa kwenye kuonesha soka?, unadhani anashindwa kuanzisha channel yake ili aoneshe?..Anaweza 100% ila tatizo soko automatically haliruhusu more than one supplier/producer...

Otherwise angekuwa tayari kuanzisha TV ili agombee tender lakini ndo hivo miaka 10 inabidi abaki na idea + ubunifu kichwani.....TFF wamefeli sana.
Kudos kwa hii analysis
 
Kuna Haja Gani ya Kuingia miaka10, kwa nn wasiingie kwa term ya 5yrs then 5yrs Tena? Je thaman ya Fedha ikipolomoka au kukiwa na fiscal cliff Unanilaumu Nani?
Mm sio mtaalamu wa mambo ya uchumi. Lakin nadhani viongozi wa TFF wametumia uzoefu wao katika thamani ya ligi yetu.
Kama mdhamin mkuu anatoa bonasi ambayo haizid mil. 100. Na anagharamia gharama za usafir kwa kila timu. Hatuoni kama Azam kaja kuwa dawa ya kulipa mishahara kwa ile bil 8 kwa vilabu?
Lakin pia wamesema pesa itapanda, kutoka mil 500 kwa mshindi had mil 700.

Jambo la thamani ya pesa kushuka Hilo linahitaji wataalamu wa uchumi pengine wanaweza kulielezea kwa uzuri zaidi.
 
Kuongezea je kulifanyika mchakato wa kushindanisha wazabuni? Maana hata Rioba TBC wangeweza kuifanya. DSTV wanaweza kuleta upinzani sana. Ni pesa ndogo sana hii. TAKUKURU watie miguu.
Mkuu hivi unajitoa ufahamu au? hukuona biders wengine wametajwa? kwa taarifa yako dstv hakubid kabisaa, nikuulize swali, ikiwa wewe ndio muamuzi wa mwisho kwenye tenda, azam kabid kwa 1b na tbc kabid kwa 1.5b utampa nani?
 
Tunaongelea Full Package 225 billion bila kuangalia hiyo miaka 10 yenyewe tutakuwa wapi katika Ramani ya Soka na Mtazamo wa Soka lenyewe kwa Mapana yake.
Kwani kuna mwingine aliyetoa pesa pungufu ya hiyo na akataka mkataba wa miaka mitatu?
 
Hujui kitu wew. Just imagine nafas ya tano atapokea 65ml. Yan iyo hela hata kwa sas iv kwa nauli ya nusu msimu haitoshi alaf TFF wamekubal ilo dili kwa mda wa 10yrs.
Azam amefany mambo makubwa kwasbb lig yetu ilkuwa haijulikan. Lakn ki uhalisia tuko nyuma ya mda.
mzee unachanganya madesa, mshindi wa 5 kupewa milioni 65 ni bonus tu kama vile watakavyompa mshindi wa kwanza mil500, hivi unavyosikia vodacom wanampa bingwa 80m unajua ndio hizo hizo?
 
Kaka hata kwa hesabu ndogo kiasi gani hio sio pesa ndogo imagine simba ndio club yenye mkataba mnono kwa sasa na ana mkataba wa billion 2.5 per year toka vunja bei sasa chukua bilion 225 gawanya kwa mwaka unapata bilion 22.5.

Zigawe kwa vilabu 16 vitavyocheza ligi kuu msimu ujao unapata karibia billion 1.5 kwa club sasa unakuaje mkataba mdogo tena wenye kuwa na muda wa miaka 10 na ukizingatia ligi yetu kiuhalisia ni chenga na utopolo mtupu.

Tuwape hongera Azam kwa kutufikisha Hapa mwaka 2011 kurudi ulikuwa huwezi hata kuona mechi yoyote bongo labda Simba na Yanga tena kwa low quality na nina uhakika tulikua hatuoni madudu ya marefa na ubovu wa team za ligi ilikuwa ni ukanjanja mtupu kabla.

Azam media group wamefanya makubwa hata kuwa na team nzuri hata huo ubora simba na yanga wanajisifu nao Azam wamechangia pakubwa mno.
Hii ni point ya msingi sana mkuu kwa uwekezaji walioufanya azam kiukwel ni mageuz katika soka letu
 
TFF na Bodi ya Ligi wameingizwa choo cha kike, huwezi kuingia mkataba muda mrefu namna hiyo lakini kitu kingine sidhani kama walipokuwa wanatangaza tenda walitangaza utakuwa mkataba wa miaka 10. Ilitakiwa angalau uwe mkataba wa miaka mitano ili kusudi wanapotaka kungia mkataba mwingine wafanye evaluation ya mkataba uliopita.

Pia nimeona vilabu ambao ni wanufaika watapata asilimia 67 na vilabu vinachekelea bila kuangalia vilabu ndio vinabeba gharama kubwa kuliko wadau wengine.
Nchi inaingia mikataba ya miaka 50 watu kimyaa ya Azam mapovu mimi na uhakika leo hii Azam anune tu sitaki tena nakuhakikisha million 500 hawapati nani wa kuwalipa? leo league imekuwa na thamani tu baada ya Azam kuibeba walikuwa wapi kabla ya Azam? Hebu watutajie kampuni moja tu hapa TZ ya kushindana na Azam, watu wako DSTV, hawa DSTV wana miaka mingapi nchi hii walikuwepo kabla hata ya kuzaliwa Azam walichangia nini katika mpira wa TZ, wao wamejikita na soko lao la ndani SA. Leo hii tumevishwa kidogo na Azam tunapendeza katika TV tumeshajiona tuko EPL. Hii league ya humu humu ndani tu tusidanganyane ni kama chips mayai iko Tanzania tu tusione sababu tunapenda sana chips mayai basi Africa nzima wanakula chips mayai. Hii league iko hapa sababu ya Azam siku wakizira tunarudi kule tulikotoka.
 
Ishu sio udogo wala ukubwa
Ishu miaka 10?
DStv akija na ofa mara tatu ya hiyo baaada ya miaka 5 hawawezi vunja mkataba?
Dstv wapo miaka yote waliweka sh ngapi tz harafu hao makaburu hata hatuwataki wanyonyaji tu. Azam waacheni wanafanya kazi nzuri. Wabongo kwa kulinga bila sbb tunapenda sana hv nyie mnaona rahisi kurusha mechi live nchi nzimaaaa
 
Hatua nzuri lakini 10yrs ni mingi sana kwa hii mikataba.

Premier League wanafanya kwa mnada na ni kwa miaka 3. Halafu wanarudi tena kwenye mnada, kufunga mkataba wa miaka 10, labda kama wameweka vifungu vya kulinda pia thamani ya fedha. Hiyo hela baada ya miaka 10 inaweza kushuka thamani by 50%.
Sasa ndugu yangu unataka kufananisha EPL na VPL, ndio wanafanya mnada kwa sababu wahitaji wengi ile ni international brand yaani EPL wanaringa wakifanya mnada na sio wanauza mechi zote wanauza kwa mafungu ikija international wanafanya mnada tena ila mwaka huu wana renew bila bidding sababu ya corona. Huku kwetu unataka mnada kama hajatokea Azam tu na ukifanya mnada Azam si atajua mpinzani ana offer ngapi atapandisha kidogo tu. Hii ni deal kubwa kwa vilabu hakuna yoyote wakuwapa hiyo Simba tu imeuza maisha kwa Billion 20 tu bado ya mkopo Azam analipa kwa mwaka hiyo.
 
Back
Top Bottom