Waungwana,
Mimi naomba kuwauliza tatizo nini katiba mbovu au wabunge kukosa uchungu na taifa? Nauliza hivi kwa sababu wengi wetu tulisikitika saana EL jina lake lilipopendekezwa kuwa PM lakini kwa maajabu makubwa kwa watanzania walio wengi EL akapita kwa kishindo bungeni.
Sasa hata leo hii mkisema rais akiteu watendaji wakuu lazima wapitishwe na bunge mimi bado yatatupata haya haya ya EL.
Labda niombe tena kuuliza hizo kura za kumpitisha PM huwa za kunyoosha mkono au kura za siri?
Watanzania tuna safari ndefu mno, waliyoyafanya wabunge wa Niger kumpinga rais wao uteuzi wa PM itachukua muda mrefu kutokea Tanzania, wabunge wetu ni wanafiki wanastahiri kupigwa bakora majimboni kwao.