AY arudi shule; kujiunga na chuo fake?

Ndugu yangu umegonga kwenyewe, nilipoangalia hiyo website ya hao jamaa wa Learn IT nikakuta kuna elimu inaitwa International Diploma, kweli nilichoka kweli kweli, kwa sababu katika Marekani diploma ni cheti unachopata baada ya kuhitimu elimu fulani. Kuna high school diploma, Associate degree Diploma, College Degree Diploma, Graduate degree diploma, n.k.

Hakuna hakuna kitu kama international degree, international diploma au international certificate. Ukitambulisha digrii yako, lazima vile vile uonyeshe uliitoa chuo gani. Angalia, watu wanatambulisha elimu ya Obama kuwa "a graduate of Columbia University and Harvard Law School"

Kichuguu,

Mambo mengine yanatokana na mifumo yetu ambayo imekazania sana kutoa vyeti.

Mtu anafanya juhudi zote hili afaulu kwenda A level. Na akipata nafasi ya A level anafanya juhudi zote ili aende mbele.

Hivyo vyeti vinakuwa motivation na sio process yenyewe ya kupata elimu.

Kama process ya kupata elimu ingekuwa ni juhudi yetu, elimu ya A level ni sawa na elimu mwaka wa kwanza au wa pili katika vyuo vikuu vya nchi nyingi.
 
Hii system mpya basi bongo......nijuavyo hakuna diploma ya mwaka 1 na adv diploma tanzania......diploma ni miaka miwiloi na adv diploma ni miaka mitatu.....

sasa iweje wewe usome miezi 12 upate diploma? hivi ndio tunaita vyuo vya mtaani....kwanza umeangalia qualification ya kuingia kwenye diploma kwanza?


nenda hata CBE leo na o level ya division one uone kama utakubaliwa ku join diploma....hapo unaanza na certicate mwaka 1 then ndio unaenda diploma miaka miwili.....muulize Ally mayai alianzia wapi....au Bonny pawasa..wale woote walikuwa form 4...

wewe kusoma pale na kupata kazi nzuri siahangai kwa system ya tanzania.....washangaa nini kama jabir kigoda form 4 feliya alikuwa "kizito' BOT.....

Wewe nawe umezidi, yani lazima udondoshe jina au picha kila baada ya posts kadhaa.
 
Kuna mtu mmoja amezungumzia kuwa vyuo hivyo vya mitaani vinatoa MSCE kwa hiyo vinafundisha vizuri.
Lakini anashindwa kufahamu kwa MSCE siyo elimu ya juu bali ni ujuzi wa kutumia Windows Server za Microsoft tu. Microfost wenyewe wanaonyesha kuwa unachotakiwa ni experience ya kutumia windows server kwa miaka miwili: angalia kwenye linki hii hapa. Unaweza kukaa nyumbani kwako ukachezea windows server yako kwa miaka miwili hadi ukaielewa kiundani, na hivyo kujipatia MSCE bila kuwekwa darasani na mtu yeyote.
mkuu hii imeniacha hoi....sasa iweje watanzania washindwe kuchezea window server 2003 wachina,wahindi,wamalaya waweze? si kiasi cha kukaa nayo tu miaka miwili mkuu? kisha unalamba certificate.....watalaam wa it watanisaidia sijui kama ni rahisi kihivyo....
Angefanya utafiti wa kutosha angegudnua kuwa kuna MSCE certificate nyingi zinazotolewa mitaani lakini hazitambuliwi na Microsoft; kwa mfano, angalia kwenye link hii hapa.

suala la u fake wa vyeti ni blobal issue.....from PhD kushuka chini zipo fake zake.....so MCSE pekee.....
 
Hapa kaazi kwel kwel yaani mtu alikosa credit hata za kuendlea na advance levell kapasi vizuri, huyo dogo alifeli Ifunda na ana D mbili tu kwenye cheti chake, hata alipokwenda Forest morogoro hakudumu hata mwezi mmoja alishindwa masomo, kifupi vyuo hivyo va mitaani ndio mahala pake hana ruhusa hata ya kufanya shoo Nkrumah hall nyambaf..

Mkuu Burn
Hii comment nimeizimia
 
ni sawa tuseme wachaga wanajua biashara.....mkuu haipingiki india wako juu kwa IT,business na fani za kitabibu.....sidhani kamaa kuna nchi barani africa na nyingi ulaya unaweza kulinganisha development ya IT n india.....hta majuu mkuu tunaona n kusikia kule silicon vllley wameja a wahindi na wachina.....na ni majuu kule.....

ukiangalia software engineer wengi ni wahindi....ila ndio wananunuliwa na wazungu...founder wa hotmail ni muhindi na wengine wengi...hata mshauri wa Obama wa IT ni muhindi.....ni ukweli usiopingika wenzetu wako juu.....apart ya chap labour huko india microsoft,IBM,DELL na kampuni kubwa za software wamehamia India....kwanini wasifungue matawi Holland,Poland au saudia Arabia?....



mkuu kwani quality ya elimu bora wewe unaipima kwa fee kuwa juu? au? kwa mujibu wako rafiki yako kasema fee ni $700 ambayo ni chini ya udsm na vyuo vingi vya tz so ina maana quality ya elimu tz iko juu mara dufu zaidi ya india au malaysia,sio? ulizia hapo learn It wanalimwa shilingi ngapi?btw elimu bora haipo UK,USA au canada.....kw sababu tu fee yao ni ghali


mkuu tafuta data za wahindi kukimbilia majuu....pia angalia je kimbilio kubw majuu ni undergraduate au post.....wamarekani wako china na south korea kwa tarifa yako wanalishwa shule ya IT.....ulizia mtu alieko Seoul atakuambia....alafu ujue kukimbiliaa majuu wengi wanafataa pay kama beijing,Soel au newdelhi wangewalipa vizuri wasingekuja majuuu
ni katika kuweka sawa

Mkuu ulipita huko nini teh teh teh teh.....

Anyway jokes aside..mimi naweza kuamini kwamba India wanajitahidi kwenye hayo maeneo uliyoniambia..lakini ukweli hawa jamaa wanatuchukulia for granted!

Anyway long story short..Mimi wahindi siwaamini kabisa. Wakiwa ulaya na Amerika wanaplay by the rules..wakiwa kwingineko hata kwao..wanakuwa longo longo sana..


Kama nina hela mwanangu ntampeleka asome shule ya "maana" kunako.. kama sina atabanana Sikinde na watanzania wengine hapa hapa....hii longo longo ya kwenda kusoma India sijui China...hapana...tutaanza kwenda kwao baadaye..siyo sasa hivi..
 
Kama nina hela mwanangu ntampeleka asome shule ya "maana" kunako.. kama sina atabanana Sikinde na watanzania wengine hapa hapa....hii longo longo ya kwenda kusoma India sijui China...hapana...tutaanza kwenda kwao baadaye..siyo sasa hivi..
tehe tehe sijapitia huko mkuu.....si unajua mambo ya ku google....kuna member humu anaitwa KILONGWE anakula shule uchinani labda atatueleza mengi zaidi...
 
shem masanja......angalia kule uchina ambapo elimu yake huiamini huyu mkulima kaweza kutengeneza ka ATC kake...
[ame="http://www.youtube.com/watch?v=SqrAA0xDKmE&feature=related"]YouTube - Broadcast Yourself.[/ame]
 
Hakuna chuo kibaya bali kuna wanafunzi wabaya au hata walimu.....kokote msuli unatoka, ud ni chuo kizuri? Watu wanakaa chini hadi juu ya mti kusikiliza leacture?

kuna tofauti kubwa sana kati ya vyuo vibaya na vizuri asikudanganye mtu

tofauti kati ya vyuo vibaya na vizuri ni kama ardhi na mbigu ndugu

elimu ya juu ni gharama sana ndugu yangu, kuna vitu vingi sana vinahitajika kulipiwa na kama chuo ni kidogo basi akiwezi ku meet gharama matokeo yake kinafundisha kufaulu mitihani tu..
mwanafunzi akimaliza unakuta creativity yake ndogo na kufikiria nje ya box hawezi

halafu university kama za uk zina displine sana katika kufundisha na kusahihisha (mtihani mmoja unasahihishwa na watu watatu mwalimu wako, second marker na external examiner na kila mtu ana copy yake).
ukifanya assignment huwezi kutumia google/au copy n paste/kucopy ya mtu mwingine, kwa ajili wakati wa ku hand-in assignment yako inapitia kwenye plagiarism software (vyuo vidogo haviwezi ku afford software)
research nyingi latest muhimu zinauzwa kwa hiyo kama chuo kidogo unakuta hakiwezi ku afford kulipia databases kwa hiyo wanafunzi wake hawana access ya material
vyuo vya mitaani havipati makampuni ya kuja kuwekeza kwenye research zao

hao waindi/wachina mnaowaongelea wewe wamejaa kibao kwenye vyuo vikuu vya uk kwa nini wasibaki kwao???? katika foreign students wa uk wachina na wahindi ndio wanaongoza
 
shem masanja......angalia kule uchina ambapo elimu yake huiamini huyu mkulima kaweza kutengeneza ka ATC kake...
YouTube - Broadcast Yourself.

Hahaha.... shem wewe endelea kuwaamini hawa jamaa wanatuliza tuu hawana lolote! Mi nilishawakataa kabisa wana longo longo kibao...

Unajua kama alivyosema Semilong..hawa jamaa hawako serious na sisi. Hivi unajua wakija Africa wanajua sisi hatujui kitu..Hivi shem..njoo bongo..bidhaa zao wanazozileta huku ni tofauti na wanazozipeleka huko majuu kwenyewe...

Na ukiwakuta wapo bongo...wanakuwa na chuo kina affiliation na jina la majuu..Hivi ulishawahi kusikia chuo cha wadosi bongo kina affiliation na Hyderabad au Bangalore au Kelara University? wanatafuta huko kwenyewe harafu wakija ndo wanatulia pesa.

Kuhusu China namsubiri jamaa yako aje atupe kapriensi yake! Sisemi lolote...


Anyway kwa vile tuna njaa..basi hatuna budi kupokea lolote..
 
hii thread imelata balaa bwa ha ha ha .....AY tafuta chuo cha maana usome.....hivyo vyuo vya degree ya mwaka mmoja achana navyo....
 
hii thread imelata balaa bwa ha ha ha .....AY tafuta chuo cha maana usome.....hivyo vyuo vya degree ya mwaka mmoja achana navyo....
Mukulu YoYo mbona umeongea ukweli tu kwenye hii thread? sidhani kama hii ndio imeleta lile balaa kule mitaa mingine.
 
Nilikuwa sitaki kusema kitu hapa lakini mmh!

hebu angalieni sehemu ya tutors..kawaida chuo chenye kutoa hadi degree wanakuwa wamesema waalimu wao wamesoma wapi na wana qualification gani..lakini kwa hapa naona wameorodheswa tu na longo longo kibao!

kama walivosema wengine ni kwa nini serikali minafumbia macho uwepo wa vyuo kama hivi? kwa nini kama NACTE wanajua kuwa hawa jamaa ni feki wasiwafungie?

http://www.learnit.co.tz/tutors.htm
 
Hii imenikumbushia tangazo flani hivi uchwara huwa naliona kwenye bango za matangazo hapa Dar. Wanasema eti, kuna njia mbili za mtu kuweza kupata sijui ni kazi/mafanikio hapa Tanzania; the hard way; primary education, o level, A level, university degree, interviews 100 kisha ndio unapata kazi. The easiest way; primary education, o level, A level, na hiyo program yao (something like ICCA-am not sure though maana huwaga naliona nikiwa mbio mbio kwa usafiri), one interview then unapata kazi. Mimi nafsi yangu huwa nikiliona najiskia kichefu chefu, impliedly wanajitangaza na kuwaambia vijana kuwa elimu kama tulivyozoea haina maana yoyote, yale yale, kuna ki short cut cha kuweza kukupatia kazi kwa njia rahisi. Imagine mtu ana degrade 'degree' kabisa kwa sababu ya ki course hicho, na bila aibu wanatangaza!

Kazi bado tunayo Watanzania.
 
Hawa jana kweli ni fast track. Course:Bachelor of science in Computing and Information duration: 12Months - 3 hours / day?
 
Ila jamaa wapo PRACTICAL kweli sio theories na kusoma masomo mengi husiyohitaji kama UDSM
 
would you suggest this college to your son, daughter or close relative?

Not son or daughter, but to be fair, to those who struggle endlessly for a Diploma or Advanced Diploma, YES. Maana wengine hat ufanyeje hiyo credit ya kwenda form 6 mhh, so let them be.
 
hii thread imelata balaa bwa ha ha ha .....AY tafuta chuo cha maana usome.....hivyo vyuo vya degree ya mwaka mmoja achana navyo....

Hivi ile thread kuhusu huu umbeya na ushankupe wako imeishia wapi?

Au nihakikishie kuwa na wewe ni MOD siku hizi na ndio maana watu makini wanazidi kutoweka siku hadi siku.
 
Hivi ni lazima tufate series ya mtaala wa kimasomo tanzania,kwamba mtoto lazima asome chekechea,Shule ya msingi 7yrs,Secondary 6yrs then Chuo miaka 3-5yrs ili aweza kukubalika kuwa kasoma?Kama kila mtu atakuwa na degree engineer atamtuma Engineer mwenzie...mwajua kuwa IIT,LEART IT,NewHorizon inatoa Second Level baada ya degree i mean technical people..kwa mfano DIT,Madini Dodoma ndio inatoa hawa mafundi walioko mitaani na kwenye maofisi?

Hawa ndio wanawasaidi watu wenye degree kwenye kazi zao za kila siku,wakati wao wanafanya managment?Go out there and see diploma kibao zinafanya mambo uko town kazi zinakwenda...kwani hawa ndio wanajituma sana.Degree hizi zinawafanya watu wanabweteka sana...wanachagua kazi sana...na kuhisi wamemaliza kila kitu.
 
would you suggest this college to your son, daughter or close relative?


Hivi kusoma ni nini hasa ???

Mimi nimesoma hizo degree zenu za UDSM, lakini niamini ninavyokwambia huku TZ wasomi wa hizo degree hawaoni ndani kwa jamaa hawa wa mitaani.

Mtu anamaliza Bsc Cumputer science miaka mitatu unakuta computa katumia kwa average ya siku 60 tu labda tena kwa masaa.

Utamlinganisha na huyu anayeichezea kila siku?, pia kumbuka hizi centre ni consultancy centres hivyo zina mifano hai za matatizo mengi sana, hawa wanatoa Internet wanauza softwares. Kwa ufupi wana first hand experience kwenye field wanazofundisha.

Wakati ma Dr wetu wa UDSM ni researchs tu..practical zero.
 
Back
Top Bottom