Avatar na jina lako, ulifikiria nini?

Avatar na jina lako, ulifikiria nini?

MIE NI MZALENDO,AVTR,,,NI FUTURE TRUCKS,,,WAZALENDO TUONE MBALI:A S thumbs_up::drum:
 
Avatar yangu ni sawa na jina langu in sketch drawing. Nilichagua jina hili kuienzi maskani yangu ya enzi hizo,
pale kwenye junction ya Samora avenue na Mkwepu street. Watu wa katikati ya jiji la Dar wananielewa vizuri
hapa.
 
Wale wazuri wote wanapelekwa kwa mfalme Mswat
 
mim ninawakilisha matatizo ya watu wa chini,watu wa wAsosikika,watu wanao kandamizwa .mimi ndio nkaamua nijiite sauti yako SAUTI YAKO
 
umefanya nikuogope, mwanamke hakuumbwa kuwa katili kiasi hicho.
mwanamke ameumwa kuwa vp?
mwanamke ameumwa kuwa na upendo sana uvumilivu sana, ujasiri sana na mengine mengi. lakini hizi sana ndio tatizo lenyewe. kwa sababu hata ukigeuza upande mwingine upendo hugeuka kuwa chuki sana, na vingine vyote katika sana hiyo hiyo. ndio maana watu husema mwanamke ni mzuri sana lakini akiamua kuwa mbaya ni mbaya sanaaaaaaaa.
ana huruma sana na akishatendwa akaikosa huruma huikosa sana.

mkuu usinishangae ni mambo ya kawaida. sipendi uonevu napenda amani utulivu na kuwapenda wengine na kuwatetea. itapobidi I CAN DO ANYTHING TO ANYBODY WHO DESERVE IT.
 
Nimekuwa nikiangalia na kushangaa kwa muda mrefu, avatar na majina tunayoyachagua yanatokana na nini hasa? unakuta mtu kaweka avatar ya jicho moja au kichwa nazi, mara avatar ina pengo, huwa najiuliza hivi leo Mungu anasema kuanzia leo uwe kama avatar yako sijui utafanya nini.

Watapona walioweka avatar za warembo, sijui itakuwaje aliyeweka avatar ya kike na yeye ni mwanaume.

Hebu tufunguke ilikuwaje ukachagua avatar na jina hilo.

Binafsi nilichagua jina la JEKI likiwa na maana nakuja katika JF kuwapiga jeki wasiojiweza kama vile jeki inavyomsaidia mtu aliyeharibikiwa na gari lake, avatar nayo ikawa jeki yenyewe.

Wewe je?

Niliwaza kama avatar na jina vinavyojieleza....
 
Hili ni jina langu la ukoo, Avatar ni tofauti za maisha kutoka eneo1 la jiji letu na eneo jingine, hasa kiuchumi
 
Id yangu ni jina langu kwa kifupi, wanavyoniita mtaani. No comment on my avatar!
 
Aliimba wimbo wa mukhomboti, ni wa kutoka hukooo kwa madiba JEKI

Mimi avatar yangu ni kama inavyojionesha, ram ni kifupi cha majina ya watoto wangu na baba yao

Oooh, nimetia aibu kwa kutokumjua huyu dada wakati ni maarufu sana. Anhaa, avatar yako ni wewe mwenyewe au na wewe ni mwanamke unayefata nyayo zake ram?
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom