The Khoisan
Platinum Member
- Jun 5, 2007
- 18,258
- 17,454
Mtasingizia wazungu kwa mengi.Tatizo wamesababisha wenyewe nchi za kiarabu za Afrika kaskazini na mashariki ya kati zilikuwa nchi za amani zilizotulia ambazo raia wake waliishi vizuri mno na wengi hawakuwa na mpango wa kwenda ulaya kama wakimbizi au wahamiaji.
Wazungu wakaanzisha vurumai za mapinduzi ya Arab spring kisingizio kikiwa ooh hakuna demokrasia!!!! kwenye nchi hizo!!! wakazibomoa na mabomu barabara .Chumi zikaporomoka chini sasa wakazi wa nchi hizo wanaona maisha magumu wanaona waende huko huko kwenye nchi za washambuliaji wakakae huko sababu kwao hakukaliki maisha mazuri waliyozoea hayapo tena.
Sasa wazungu waliojitia wana huruma, huruma ya kuwapokea wakimbizi imekatika.Walitakiwa wasiziingilie nchi hizo za kiarabu mambo yao ya ndani ulaya kungekuwa kimya na kusingekuwa na ugaidi duniani.Wao wakiona nchi imetulia wanachotakiwa kufanya ni kuiacha iendelee kutulia kwani ikilipuka hata kwao kutakuwa si salama.Sasa hivi Wakimbizi ni agenda ya kisiasa ujerumani wakati kabla ya hapo haikuwepo.Waliposhambulia miinchi kama Iraq ndio ukaanza kuzaliwa ugaidi mbaya kabisa.
Nchi kama Somalia ilitawaliwa na dikteta Siad barre kwa miaka kibao lakini Somalia ilikuwa taifa moja na lililotulia.Marekani na Ulaya wakajitia na videmokrasia vyao kuwa somalia inatakiwa itawaliwe kidemokrasia ya nchi za Magharbi wakaondoa mzee wa watu hawakujua aina ya watu kama wasomali wanatakiwa kutawaliwa kidikteta.Mwarabu na msomali utawala unaomfaa ni wa kidikteta au kifalme ndio panatulia.Mpaka leo marekani na ulaya hawajui nini kifanyike somalia.Nchi haikuwa na magaidi imezalisha magaidi wa ALSHABAB baada ya SIAD BARRE kuondolewa.Wanajuta kuingilia Somalia.Kila nchi ina aina ya watu na staili za kuwatawala na kuifanya itulie hawa wamarekani na ulaya wanajifanya wana solution ya utawala ya aina moja kwa dunia nzima.They are wrong.Hiyo miundo na mifumo yao ya kidemokrasia,ushoga,usagaji na ndoa za jnsia moja inafaa huko kwao sio muarobaini wa kila nchi!!!!!Ulaya Na marekani zamani walikuwa Na watu wenye akili sana kwenye mambo ya utawala wa ndani na wa kimataifa sasa hivi hawana watu.Very sad
Hilo tatizo wamelitengeneza wenyewe hiyo miji waijenge huko huko kwao
Wazungu hawakuanzisha hayo mapinduzi bali waliyaunga mkono. Waarabu walitakiwa wake na uwezo wa kumanage mambo Yao. Period. Kama kisingekuwa tamaa ya madaraka wangeweza kutransform na manage situation.
Hayo matatizo yatakuwa kutokea kwenye hadhi ya nchi za kiafrika including Tanzania. Kwa Tanzania hii tabia ya wao kujidai kuwa wana uwezo na akili ya kuongoza nchi kwa sababu wako ndani ya chama flani kuna siku itaback fire tu.