Askofu Mwamakula sio mhuni, wahuni ni nyie mnaotetea maovu. Watanzania tunataka Katiba Mpya

Nyankurungu2020

JF-Expert Member
Oct 2, 2020
4,086
6,568
1613650666713.png

Watanzania wanahitaji katiba mpya maana wanajua fika mwarobaini wa matatizo yao.

Katiba mpya ndio itayokata mzizi wa fitina wa kila shida inayowakabili Watanzania.

Mfano tunataka Katiba ambayo itaruhusu kila mtanzania kuwa na mamlaka ya kusimamia haki za binadamu wenzake,mathalani mtu akiuliwa na vyombo vya dola katiri visivyojali haki za binadamu, ndugu au jamaa za marehemu wawe na uwezo kufungua kesi na kushitaki sio mpaka Jamhuri ifungue kesi.

Tunataka Katiba itayolinda uhuru wa raia wa Tanzania. Raia wawe huru, sio kuwa wanakamatwa hovyo na vyombo vya dola bila sababu. Sio kuwa wanateswa na kuumizwa kisa tu ni watuhumiwa. Tunataka katiba ambayo itamfanya kila mtanzania aache uharifu. Kama ni mharifu apewe adhabu kwa mujibu wa sheria za nchi.

Kwa muktadha huu sioni sababu ya kufanya unafiki na kumuita Askofu Mwamakula muhuni wakati anapambana watanzania kupata katiba itayowasaidia.

Ni wapi aliwahamasisha watanzania kuleta vurugu wakati wanaandamana? Alihamasisha watu wabebe siraha?
 
Mi policcm inamuonea tu Mtumishi wa Mungu. Hoja zake zina mashiko. Watanzania tunahitaji Katiba yetu Mpya tuliyo ipendekeza!

Lakini pia tunahitaji Tume Huru ya Uchaguzi ili kuondokana na huu uhuni tunaofanyiwa na CCM wakati wa uchaguzi.
 
Je, ni vitu hivyo tu abavyo mnataka katiba mpya ifanye? Inaonekana wengi hamjui maana ya katiba! Kufuatana na katiba ya sasa, vipengele vyote ulivyo vitaja ni uhalifu na kama ukimshitaki aliye tenda makosa hayo - kama una ushahidi wa kutosha, ataadhibiwa.
Hivyo kama unatetea kuwepo kwa katiba mpya jaribu kujua faida zake - ni nini ambazo mtanzania wa kawaida atapata.
 
Wala hata huelewi katiba ni kitu gani. Unafikiri katiba ndio itamaliza rushwa au kuingiza upinzani madarakani? Kama huoni katiba sio tatizo tanzania wewe ni sawa kasuku unaimbishwa tu wimbo na adui wa nchi yetu.
 
Chadema ni wajinga sana! Yani ukiwauliza mnataka katiba mpya ili iweje wanakwambia ili tuitoe ccm madarakani

Jamani katiba ni karatasi tu, hazipigi kura wala kutangaza matokeo. Hivi kule ambako vyama tawala vimeondolewa kulianza na katiba mpya?
 
Chadema ni wajinga sana! Yani ukiwauliza mnataka katiba mpya ili iweje wanakwambia ili tuitoe ccm madarakani

Jamani katiba ni karatasi tu, hazipigi kura wala kutangaza matokeo. Hivi kule ambako vyama tawala vimeondolewa kulianza na katiba mpya?
Yani wewe ilibidi uitwe INYEGENDA....

Unanyegeka sana.
 
Je! Ni vitu hivyo tu abavyo mnataka katiba mpya ifanye? Inaonekana wengi hamjui maana ya katiba! Kufuatana na katiba ya sasa, vipengele vyote ulivyo vitaja ni uhalifu na kama ukimshitaki aliye tenda makosa hayo - kama una ushahidi wa kutosha, ataadhibiwa.
Hivyo kama unatetea kuwepo kwa katiba mpya jaribu kujua faida zake - ni nini ambazo mtanzania wa kawaida atapata.
Unafahamu kusoma? Hapo nimeweka mifano tu. Hujui kuwa tunataka tuwe na haki ya kumwajibisha mbunge anayeshindwa kutekeleza majukumu yake?
 
Back
Top Bottom