Nimemsikiliza kwa makini jana Askofu wa Kanisa la Ufufuko na Uzima, Josephat Gwajima akitoa utetezi wake juu ya kile kilichoelezwa na Dr Slaa kuwa ni Ushenga baina ya ndoa ya Lowasa na CHADEMA. Kimsingi amekubaliana na yale yaliyoelezwa na Dr Slaa na kujitetea eti alikuwa anafanya hivyo kama wajibu wake wa msingi kwa wanasiasa. Eti kwamba wanasiasa wengi wanapotaka kugombea wanaenda kwa waganga wa kienyeji hivyo yeye alitaka kumuandaa Lowasa kiroho.
Jambo lililonishtua zaidi ni pale aliposema kuwa kama Dr Slaa ataendelea kuwatukana Maaskofu wa Kanisa Katoliki, Anglikana, Lutherani, TAG, Masheikh na Maimamu nk, hatakaa kimya bali atajitokeza kuwatetea. Kwamba Masheikh na Maaskofu wasijisumbue kumjibu Dr Slaa bali yeye ataifanya kazi hiyo.
Binafsi nimetafakari sana juu ya msimamo huu wa Gwajima. Nimejiuliza, ni wapi Dr Slaa kawatukana Masheikh na Maaskofu? Au kuwaambia kuwa baadhi yao wamepokea hongo toka kwa Lowasa jambo ambalo ni kweli ni matusi? Ni lini Gwajima amekuwa na urafiki na Maaskofu wa Kanisa Katoliki? Ni lini Gwajima amekuwa na Urafiki na Masheikh na Maimamu?
1. Gwajima aliwahi kumtukana Askofu Pengo wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam
2. Gwajima huyo huyo aliwahi kumtukana Askofu Balina wa Kanisa Katoliki jimbo la Shinyanga ambaye kwa sasa ni marehemu.
3. Gwajima pia aliwahi kumtukana Askofu Norbert Mtega wa Kanisa Katoliki, Jimbo kuu la Songea.
4. Gwajima pia aliwahi kuwatukana Masheikh na Maimamu wakati wanadai haki ya Waislam ya kuwa na Mahakama ya Kadhi ndani ya Katiba Mpya.
Kimsingi Mchungaji Gwajima katika hili hana moral authority ya kumnyooshea kidole Dr Slaa ambaye hajatukana. Yeye ndiye alipaswa kujikanya mwenyewe kwa matusi ambayo amekuwa akiporomosha kila siku kwa mahasimu wake kiroho na kisiasa.