Shixi889
JF-Expert Member
- Jun 1, 2012
- 338
- 208
Wakuu Mimi nakwenda Mbali zaidi, katika kuyajadili maneno ya huyu anayejiita Askofu Gwajima aliyoyatoa jana tar 08.09 katika ukumbi wa Landmark Hotel, kama majibu kwa Dr. Slaa kufuatia Dr. Slaa kumwita yeye (Gwajima} mshenga wa kukaribishwa kwa Mh. Edward Lowasa ndani ya CHEDEMA.
Ndugu zangu maneno ya Askofu Gwajima si tu yanashusha tu credibility ya Ukawa Ila Gwajima hanashusha hata credibility ya Maaskofu wenzake.
Gwajima anavyosema mambo ambayo yalikuwa siri kati yake na mtumishi wake wa dini Dr. Slaa ama Bi Mashumbushi, anadharirisha uaskofu wake, kwasababu kama baba wa kiroho unaanza kuropoka mambo ya siri ya kondoo zako, hivi ni nani? Leo mwenye akili timamu ataweza kukufuata na kukuambia jambo lake la siri.
Gwajima amejisifu kuwa yeye anakakitu kakurecordia, hivyo maongezi yote anayoyafanya huya-record yaani ni mtaalamu wa kurecord, sasa embu, Jiulize, muumini wake yupi Leo, mwenye akili timamu, atakaye weza kumfuata Askofu Huyu na kumweleza mambo yake ya siri ya kiroho yanayoitaji msaada wa kiroho, kama mtumishi huyu amekuwa mropokaji kwa kiwango hichi.
Mimi ni mkatoliki sisi kwetu tunakitu tunaita sacrament ya kitubio, Ambapo Mlei umfuata Padri nakukiri dhambi zake\kuungama Dhambi/Maungamo, hapo kwenye Maungamo mnakuwa na padri tu, na unamueleza dhambi ulizozitenda, kisha padri utamka maneno Fulani kisha dhambi zile kwa imani yetu tunaamini huondoka, sasa kinachofanyika pale huwa ni siri yako wewe unayetubu Padri, na Mungu wenu pekee,
Katika mazingira hayo watu uungama na kutaja dhambi mabalimblali, wengine unakuta alishawahi kuua na kuiba, unamkuta mtu anataja kuwa alishawahi kuzini na Mke Wa katekista pengine, sasa japo huyu padri anamjua Mke Wa katekista na katekista mwenyewe kama msaidizi wake ila hawezi kumfuata na kumwambia lolote Yale yanabaki kuwa siri na kwavile ni maungamo tunaamini yanakuwa yamekwisha lakini haimaanishi Bw. Huyo Mlei ameacha ama kukoma kutenda dhambi.
Huo ni mfano tu wa padri wa kanisa katoliki, haya sasa mfananishe huyu Gwajima kama angelikuwa Padri, si angekuja Jana kutuambia yote Ambayo Mama Mashumbushi. Mke Wa Dr Slaa aliyatubu kwake? Hakika huu ni mfano wa Upuuzi wa kiwango cha PHD.
Lakini mbali na hapo Gwajima ni Muhuni, kwasababu yeye mwenyewe alishawahi kumtolea maneno ya kashfa sana Kiongozi wangu Wa kanisa, Aliyenipa Kipaimara, Askofu Polycop Kardinali Pengo alimwita majina ya hovyoovyo na ni wazi kabisa kuwa yalikuwa matusi. Embu sasa tazama mambo yake Alafu Leo mtu yule yule Muhuni aliyemtukana kiongozi Mkuu wa kanisa katoliki nchini, anarudi kwetu kuwakemea watu wengine tena walei wake mwenyewe wanapowatukana Maaskofu. Kwani si yeye aliyewafunza?
Pengine Dr. Slaa alikuwa sahihi aliposema Maaskofu wananunuliwa kwa kumchukulia mfano wa Askofu mmoja tu, Askofu Gwajima ambaye ameonekana wazi wazi kabisa kununuliwa na Mh. Edward Lowasa.
Gwajima amejiaibisha na kuwaaibisha Maaskofu wenzake wa Madhehebu mengine, wala asijibaraguze yeye hawezi hata siku moja kafanana na Askofu Pengo, kwasababu yeye mwenyewe hana maadili wala hana utakatifu ni Muhuni tu kama wahuni wengine walioko kule Tandale kwa mtogole ama Manzese.
[h=1]Mithali 26[/h]1 Kama theluji wakati wa joto, na mvua wakati wa mavuno; Kadhalika heshima haimpasi mpumbavu.
2 Kama shomoro katika kutanga-tanga kwake, Na kama mbayuwayu katika kuruka kwake; Kadhalika laana isiyo na sababu haimpigi mtu.
3 Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda, Na fimbo kwa mgongo wa mpumbavu.
4 Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake; Usije ukafanana naye.
5 Umjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake; Asije akawa mwenye hekima machoni pake.
6 Apelekaye ujumbe kwa mkono wa mpumbavu Hujikata miguu, na kunywa hasara.
7 Miguu yake achechemeaye huwa dhaifu; Kadhalika mithali katika kinywa cha mpumbavu.
8 Kama mfuko wa vito katika chungu ya mawe; Kadhalika mtu amheshimuye mpumbavu.
9 Kama mwiba uingiao katika mkono wa mlevi; Kadhalika mithali katika kinywa cha mpumbavu.
10 Fundi stadi hufanyiza vitu vyote; Bali amwajiriye mpumbavu ni kama awaajiriye watu wapitao.
11 Kama vile mbwa arudiavyo matapiko yake; Kadhalika mpumbavu afanya upumbavu tena.
12 Je! Wamwona mtu mwenye hekima machoni pake mwenyewe? Afadhali kumtumaini mpumbavu kuliko yeye
Gwajama arudie tena kusoma vizuri hiyo Methali.....!!!!!