Kwani Pengo ninani hata asikemewe?
.....ni mfanyakazi wa serikali, mnufaika wa mgao wa Escrow.
Kwani Pengo ninani hata asikemewe?
Ile clip ina mengi ya kutafakari.......tuendako pabaya.Tusomeni alama za nyakati.Linaanza la wakiristo kwa wakiristo.
.....ni mfanyakazi wa serikali, mnufaika wa mgao wa Escrow.
Acha uwongo wewe jamaa kasema yuko Arusha...Pengo mtu wa system kitambo sana lazima aheshimiwe! Alikua mshauri wa bwn Nkapa!
Leo asubuhi nilibahatika kusikia matamshi ya Gwajima kupitia Redioni!! Kwakweli ni aibu sana kuwa na watu wa aina hii ya Gwajima katika Kanisa, inawezekana kweli alikerwa na hicho Kadinari Pengo alichokisema lakini namna alivyo panikc na kutoa mahubiri ya kumkashifu Kadinari sio sawa, Sina uhakika kuwa kweli huyu ni mtu wa Mungu maana Bwana Yesu katika mafundisho yake alifundisha faida ya kuwa wapole na wanyenyekevu machoni pa watu hata Mbele za Mungu, Nadhani wafuasi wa haya Makanisa ya aina ya Gwajima ifike wakati wajiulize na wamuulize roho mtakatifu awafunulie kilichoko nyuma ya pazia kwa watumishi wanaowaongoza. Ni aibu sana kwa kanisa
Ndo maana anaitwa mnafiki, toka lini yesu alikuwa mshauri wa mfalme herode, au pilato
Gwajima ni kama komandoo flani,amewachenga vizuri sana,maana hapo polisi walikuwa wamesha jiandaa mabomu,risasi na maji ya kuwasha ili walipe kisasi kwa waumini wake, yaani kawachenga vzr sana
Nakupa big like mkuu tatuzo kuna watu wanacoment vitu wasivyovifahamu kwa sheria ya uvunjifu wa amani Gwajima hana pa kutokeaUle uwanja si kanisa ni public open space kama uwanja wa jangwani.Si jengo la kanisa lile.Kamtukana pengo kwenye uwanja wa wazi mbele ya watu wenye dini na wasio na dini kwenye eneo lisilokuwa la kidini la viwanja vya Tanganyika Packers visivyokuwa vya kidini.Pale hakuna madhabahu pana jukwaa mbele ya sheria.Ambapo alitumia hilo jukwaa kumtukana Pengo akijua fika kuwa pengo si muumini wa kanisa lake wala si kiongozi aliye chini yake akaamua kumporomoshea matusi ya nguoni wakati akjijua pengo hakuwemo humo kanisani kujitetea dhidi ya matusi aliyomporomoshea.
Si kesi zote za jinai lazima mtu aliyekashifiwa akashtaki.Mfano wewe ni askofu ukatukana waislamu hadharani kuwa mohamed alikuwa anakula nguruwe Waislamu wakaja juu.Polisi wanaweza kukufungulia mashtaka ya kutoa matamshi yanayoletelea uvunjifu wa amani bila mwislamu yeyote kupeleka mashtaka.
Kutukana pengo ni kuletelea uvunjifu wa amani kwa waumini wanaomheshimu Pengo.Hivyo Polisi kumfungulia mashtaka Gwajima ni sahihi.Pengo wala hahitaji kwenda polisi.
Gwajima ashikiliwe hadi jumatatu ili asizidi kuzua na kuporomosha matusi na tuhuma zitto.Ikumbukwe kuwa pamoja na kutafutwa ameendelea kutoa Audio za matusi kwa viopngozi ikiwemo aliyoweka leo.Kwa hiyo ili asiendelee na hayo ashilkiliwe hadi jumatatu
Wampime na DNA ili tuwe na uhakika mtoto wa Flora ni wake
Usibwabwajebwabwaje tu mdomo ! Kuna civil and criminal law...hii kesi ni sawa na ya kubaka mtoto. Mwenye mtoto akifungua kesi au asipofungua kesi, SERIKALI itafungua tu upende usipende.
Tuacheni maneno ya kanga na ngonjera hapa. Alichokifanya hata shetani anamshangaaa
Pengo na Kilaini ni waganga njaa
sasa pampaz ni tusi
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Uzima na Ufufuo, Josephat Gwajima amejisalimisha kituo cha polisi kati kuhojiwa juu ya kutoa lugha chafu dhidi ya Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Muadhama Polycarp Kardinali Pengo.
Akiongea kabla ya kuhojiwa na polisi Mchungaji Gwajima amejitetea kuwa alichofanya ni kutumia fursa ya kumuonya kiongozi mwenzake wa kiroho kutokana na kuwageuka wenzake katika makubaliano waliofikia katika tamko la kuipigia kura ya hapana Katiba inayopendekezwa.
![]()
Pole Gwajima japo lugha uliyoitumia ilikuwa na ukakasi sana ila ujumbe umemfika askofu wangu pengo
mchochezi mkubwa...akamatwe tu na afungwe mpaka kieleweke. hawezi kuwa anatukana watu kwa makusudi akaachwa bila kushtakiwa na kufungwa jela.