Leo asubuhi nilibahatika kusikia matamshi ya Gwajima kupitia Redioni!! Kwakweli ni aibu sana kuwa na watu wa aina hii ya Gwajima katika Kanisa, inawezekana kweli alikerwa na hicho Kadinari Pengo alichokisema lakini namna alivyo panikc na kutoa mahubiri ya kumkashifu Kadinari sio sawa, Sina uhakika kuwa kweli huyu ni mtu wa Mungu maana Bwana Yesu katika mafundisho yake alifundisha faida ya kuwa wapole na wanyenyekevu machoni pa watu hata Mbele za Mungu, Nadhani wafuasi wa haya Makanisa ya aina ya Gwajima ifike wakati wajiulize na wamuulize roho mtakatifu awafunulie kilichoko nyuma ya pazia kwa watumishi wanaowaongoza. Ni aibu sana kwa kanisa