Arusha: Polisi, Walimu na Wanafunzi kuanzisha club za kupambana na uhalifu shuleni

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,989
3ed9c227-e0cb-4851-afaf-e38ede98facb.jpeg
Mkaguzi wa kata ya Mkundi Mkoani Morogoro Mkaguzi msaidizi wa Polisi A/INSP Anna Manumbu amebainisha kuwa Jeshi hilo kwa kushirikiana walimu na wanafunzi wanaunda club za kupambana na uhalifu mashuleni ambazo zitaongeza kasi ya kupambana na uhalifu na vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia.

Mkaguzi huyo amebainisha endapo club za kupambana ana uhalifu mashule zikiimarishwa mashuleni zitaibua taarifa nyingi za uhalifu wanaofanyiwa baadhi ya wanafunzi katika kata hiyo.
0c77d18b-ce77-4fa1-9f5f-a8737998efe6.jpeg

4aec826d-0ac8-48dd-83c1-07e329553562.jpeg

3c0859aa-75b3-441a-bacd-3452bb163e0d.jpeg
Pia amesema kwa kufanya hivyo itasaidia kuondoa changamoto ya kupata taarifa sahihi pindi changamoto inapotokea ya uhalifu na unyanyasaji wa kijinsia wanaofanyiwa baadhi ya wanafunzi katika eneo hilo la kata ya Mkundi wilaya Morogoro Mjini Mkoani Morogoro.

Mbali na hilo amewataka walimu kutengenezea mahusiano mazuri na kubadilishana taarifa kutoka kwa wananfunzi, wazazi na walezi wa wanafunzi hao ili kupata taarifa sahihi pindi wanafunzi hao wanapopata changamoto.
 
Back
Top Bottom