Arusha: Mgomo wa daladala na pikipiki

Arusha: Mgomo wa daladala na pikipiki

Mimi ni mwanachama wa CDM..sipendi kusikia tunavyichukuliwa na other parties. kwanini tuendelee kuitwa watu wa vurugu, mambumbumbu, tulioishiwa sera?
Tubadilike..hata kama tuna machungu sana na nchi yetu, its better tutumie means nzuri na zenye manufaa kuleta ukombozi. Mbona Malawi wameweza, kwanini sisi tushindwe?

kwaio unashauri chadema watende yale ya kuifurahisha ccm,alafu iweje?kama unataka kuifurahisha ccm hamia kwa wenzi wao cuf
 
Mtu kajipeleka mwenyewe mahakamani halaf watu vihelehele ati wanagoma.sasa wanamgomea nani?.Tuzungumze ukweli tukiambiwa chagueni wabungë wa CCM tunakuwa na viburi,sasa hawa wehu tunaona madhara yake.tangu tumchague huyu jamaa hapa Arusha amekuwa kituko.hajafanya lolote la kutuletea maendeleo zaidi ya migogoro na vifo.tunamshukuru AFANDE ZUBERI kumdhibit la sivyo wizi wa magari ungekua umetamalaki hapa Arusha.

Mtu mpumbavu utamjua tu kwa maneno yake,pia utumwa ni mzigo
 
Ilikuonyesha kumuunga mkono kamanda Godbless Lema, madereva wa daladala na Toyo kesho wataanza mgomo hapa Arusha....

=======


Yale yale ya IGunga , vyombo vya habari viliongeza chumvi sana kuhusu hali a Igunga wakati wa uchaguzi, wakati wakazi wa huko wenyewe wanaendelea na kazi zao kama kamwaida. Arusha nao watakuwa wanashangaa tulivyokosa kazi humu JF yaani kweli daladala na pikipiki zigome kisa mtu kajipeleka mwenyewe jela. Kma mimi ndiyo SUMATRA hakika magari yenu hao mtauza scrapers
 
Last edited by a moderator:
Mtu kajipeleka mwenyewe mahakamani halaf watu vihelehele ati wanagoma.sasa wanamgomea nani?.Tuzungumze ukweli tukiambiwa chagueni wabungë wa CCM tunakuwa na viburi,sasa hawa wehu tunaona madhara yake.tangu tumchague huyu jamaa hapa Arusha amekuwa kituko.hajafanya lolote la kutuletea maendeleo zaidi ya migogoro na vifo.tunamshukuru AFANDE ZUBERI kumdhibit la sivyo wizi wa magari ungekua umetamalaki hapa Arusha.

Hatishiwi mtu nyau, huyo Zuberi kajidai kumtisha sasa mwanaume mzima (Lema) kaenda mwenyewe Kisongo. Na kila siku anayolala huko gerezani ndio hali ya Benghazi inazidi kuwa tete. Mtajuta!
 
Miaka 50 ya uhuru wa bendera Wananchi Tumechoshwa na;
1. Umaskini wa kuletewa na CCM,
2. Ufukara uliokithiri wa kuletewa na MAGAMBA,
3. Manyanyaso kutoka kwa WALOWEZI na MAKUPE wa CCM,
4. Utu wetu kutothaminiwa kwa Kuitwa PANYA, wadanganyika wa kanga na vitenge, Wavivu wa Kufikiri tusio kuwa na taaluma ya utawala kama NET GROUP SOLUTION, RITES, TANZANITE ONE, AFRICAN BARRICK GOLD, SYMBION, KAGODA, RICHMOND, AGRECO, DO ONCE, EPA, GGM, UPUNGUZAJI WA RAIA MV BUKOBA, SPICE ISLANDER, DISCO TOTOs, MBAGALA & GONGOLAMBOTO, INFLATION MGT, TCCC, TBL, KIWIRA ANNABEN...
5. Wanyama wetu na kuporwa
6. Kukosa Huduma bora za Afya
7. Kukosa maji safi na salama
8. Kukosa ajira
9. Kuwa Gizani kwa kukosa umeme badala yake waporaji wa madini kupatiwa umeme unaotokana na kodi zetu wananchi.
10. Kuibiwa kura wakati wa uchaguzi
11. Askari polisi kuamua ku ua wananchi Arusha,Mara, Igunga, Buzwagi, Mererani...
12. Sera za CCM za sisi wananchi Kuwekezewa madude kwenye Ardhi yetu wenyewe
13. Mafisadi wa MAGAMBA ku-ua viongozi wetu wazalendo kama Mwl Nyerere, Hayati Karume, Sokoine, Kombe, Kolimba, Prof Chachage, Wangwe, Mbatia, Prof. Shaba ...
14. kukosa sukari na bidhaa muhimu
15. sera za kueneza njaa za CCM
16. kitengo cha usalama kuwekwa mfukoni na MAFISADI...
17. Kupanda sana kwa gharama za maisha
18. Tanzania yetu Kutokuwa na sera wala mfumo wa maendeleo kwa wananchi
19. Bunge lenye kutetea Mafisadi chini ya CCM
20. Mahakama kutokuwa huru
.... Kesho itakuwa ni Mwanzo tu wa mapambano ya muda mfupi na hawa magamba, tutafunga barabara kuu zote kesho, then tutaendelea keshokutwa ambapo mgomo utajumuisha mkoa wa kilimanjaro na Manyara. kisha itafuata Tanga, Mara, Mwanza, Shinyanga, Dar, Mbeya, Then Nchi Nzima kwa muda usiokuwa na kikomo. Tutasitisha kwa muda biashara ya Utalii ...
 
Vyombo husika vya kiserekali vizikilize ushauri huu. Kajadilianeni na Lema sasa hivi , muelewane naye atoke kule aliko ili kuvunja NGUVU amabayo mkifanya mzaha kidogo Mtamkabidhi mikononi, jmabo ambalo mtalijutia kwa muda mrefu ujao. MSICHEZE NA NGUVU YA UTU ANAYOILALAMIKIA KWENYE WARAKA WAKE ... UTU NDIO CHIMBUKO LA TAIFA HILI ... NI MEBGU YA KUMWAGILIA MAJI KIDOGO NA ITAFUMUKA KWA NGUVU KUBWA.

Kwa kuwa hamko kwenye nafasi ya kusikilizana nyie wenyewe ni kweli PIA hmna nafasi ya kusikiliza kinachoshauriwa hapa. HIVYO tarajieni kile ambacho hamtatamani kukiona , kile ambacho BURE kabisa Mtampatia kama USHINDI kwenye kisahani cha ALMASI Mheshimiwa Lema. NARUDIA Tena ... Kama hamtaki kumpa Lema ushindi wa BURE kabisa ..MFUNGULIENI SASA HIVI ...!!

Lakini Nyie wabishiiiiii!!! Kwahiyo ...Subirini kimchezo mchezo nchi nzima ijipange ... Hamjaona kitu kama hiki ..karibuni .... Lema ameweka mitego yake in a purely PSYCHOLOGICAL WAR FAIR ...!!! You will poorly react and you will terribly going to loooseee!!

Na ikiwa wataenda kujadiliana na LEMA basi hapo nitaaminini kwamba kweli serikali ya JK ni serikali legelege!!! Yaani mtu ajipeleke mwenyewe selo halafu ukambembeleze atoke?!!! kumbe alijipeleka makusudi ili achochee ghasia zitakazowaumiza waliomo na wasiokuwemo?! Mnataka kumchezea simba sharubu kwa kumuona amelala!
 
Watanzania wenzangu,

Ni kwa nia njema kabisa naomba kueleweka kwamba ni hekima na busara kuweka U-tanzania kwanza kabla ya Chama. Hapa napenda kuongea kama mtanzania na wala si mwana CCM ama mwana CDM.


Ni vyema tukajua asili, lengo, nia ya kitu kabla ya kukifanya ama kukishabikia. Kama watanzania wapenda amani tunajua nini maana ya mgomo huo unaotarajiwa kufanywa kesho?, kwa faida ya nani?.

Ndugu zangu tuwe makini sana na tutafute ukweli kwa mapana na marefu kabla ya kushabikia mambo. Kwa upande wangu nisingependa hayo yatokee kwani kuna njia mbadala ya kutatua hili tatizo. Na nikiangalia kwa undani zaidi naona Watanzania tunasukumwa kuanza vita ya wenyewe kwa wenyewe kwa faida ya watu wachache wenye uchu na uroho wa madaraka kwa kupata msaada wa mataifa makubwa ya magharibi.
Tuwe makini ndugu zangu, tuelewe nini lengo na nia ya chama unachoshabikia, nani anatoa fedha za kukiendesha chama hicho na kwa sababu gani. Tuna madini lukuki ndani ya nchi yetu, nchi za magharibi zinayatamani sana hivyo tusipokuwa makini tutajikuta tunapiganishwa wenyewe kwa wenyewe kwa faida ya hayo mataifa makubwa ya magharibi yanayotoa hayo mapesa kwa lengo la kuleta machafuko ndani ya Tanzania.
Kama hujui lengo na faida ya mgomo wa kesho sasa ushauri wako utatusaidia nini nyamaza waache wanaojua malengo yake.
 
Mpango mzuri na hivi saizi sina ajira naingia barabarani kesho bango nshaandaa tayari.
 
Na ikiwa wataenda kujadiliana na LEMA basi hapo nitaaminini kwamba kweli serikali ya JK ni serikali legelege!!! Yaani mtu ajipeleke mwenyewe selo halafu ukambembeleze atoke?!!! kumbe alijipeleka makusudi ili achochee ghasia zitakazowaumiza waliomo na wasiokuwemo?! Mnataka kumchezea simba sharubu kwa kumuona amelala!
Muna simba gani Tanzania kuzidi simba baba yenu wa Afrika aliyetolewa kwenye shimo la majitaka juzi.
 
Yale yale ya IGunga , vyombo vya habari viliongeza chumvi sana kuhusu hali a Igunga wakati wa uchaguzi, wakati wakazi wa huko wenyewe wanaendelea na kazi zao kama kamwaida. Arusha nao watakuwa wanashangaa tulivyokosa kazi humu JF yaani kweli daladala na pikipiki zigome kisa mtu kajipeleka mwenyewe jela. Kma mimi ndiyo SUMATRA hakika magari yenu hao mtauza scrapers

Wewe binuka vyovyote lakini sikio halizidi kichwa.
 
Dr Slaa nae nasikia anataka ajipeleke Gerezani kuchuana umaarufu na Lema!
 
Umechelewa sana kutoa ushauri ndugu,labda ukiweza upite na gari yenye spika Arusha nzima usiku huu..yatayotokea kesho mtajuta
Watanzania wenzangu,

Ni kwa nia njema kabisa naomba kueleweka kwamba ni hekima na busara kuweka U-tanzania kwanza kabla ya Chama. Hapa napenda kuongea kama mtanzania na wala si mwana CCM ama mwana CDM.


Ni vyema tukajua asili, lengo, nia ya kitu kabla ya kukifanya ama kukishabikia. Kama watanzania wapenda amani tunajua nini maana ya mgomo huo unaotarajiwa kufanywa kesho?, kwa faida ya nani?.

Ndugu zangu tuwe makini sana na tutafute ukweli kwa mapana na marefu kabla ya kushabikia mambo. Kwa upande wangu nisingependa hayo yatokee kwani kuna njia mbadala ya kutatua hili tatizo. Na nikiangalia kwa undani zaidi naona Watanzania tunasukumwa kuanza vita ya wenyewe kwa wenyewe kwa faida ya watu wachache wenye uchu na uroho wa madaraka kwa kupata msaada wa mataifa makubwa ya magharibi.
Tuwe makini ndugu zangu, tuelewe nini lengo na nia ya chama unachoshabikia, nani anatoa fedha za kukiendesha chama hicho na kwa sababu gani. Tuna madini lukuki ndani ya nchi yetu, nchi za magharibi zinayatamani sana hivyo tusipokuwa makini tutajikuta tunapiganishwa wenyewe kwa wenyewe kwa faida ya hayo mataifa makubwa ya magharibi yanayotoa hayo mapesa kwa lengo la kuleta machafuko ndani ya Tanzania.
 
Hapa ukishakuwa under the influence of Bacard and the likes na muda huu ban inamhusu mtu...nimemfuatilia kilaza facebook naona ntaishia kupigwa ban ila wacha nikupe hili tusi maana nimeshindwa kuvumilia@facebook BUJIBUJI wewe
 
haya....nimependa ushauri wako.....

Mohamed Boaziz alikuwa mtu mdogo sana Tunisia, mmachinga hasiye julikana na wengi zaidi ya familia yake, lakin tendo lake la "kijinga" ni historia, si ya Ben Ali pekee bali ulimwengu mzima.
 
ndugu yetu Ngongo unaambiwa kuna maandamano halafu unataka kutembea na gari? Kweli hulitakii mema hilo gari lako litachomwa moto au litavunjwa vioo n.k,tembea kwa miguu ikiwezekana ungana nao. Nalog off
 
Yale yale ya IGunga , vyombo vya habari viliongeza chumvi sana kuhusu hali a Igunga wakati wa uchaguzi, wakati wakazi wa huko wenyewe wanaendelea na kazi zao kama kamwaida. Arusha nao watakuwa wanashangaa tulivyokosa kazi humu JF yaani kweli daladala na pikipiki zigome kisa mtu kajipeleka mwenyewe jela. Kma mimi ndiyo SUMATRA hakika magari yenu hao mtauza scrapers

utaishia kusema "kama"
 
Back
Top Bottom