Bushmamy
JF-Expert Member
- Aug 18, 2019
- 8,848
- 15,253
Machinga mmoja ambae hadi sasa hajafahamika jina lake amepigwa vibaya na mgambo wa jiji la Arusha na hali yake inasemekana ni mbaya.
Adha hiyo imetokea mida hii ya usiku baada ya kutokea mabishano kati ya Mgambo Na machinga na hivyo Kupelekea machinga huyo kupata kipigo Kikali kutoka kwa mgambo wa jiji hali iliyopelekea kujeruhiwa vibaya na hivyo kukimbizwa kwenye Hospitali ya Ngarenaro iliyopo jijini hapa.
Wananchi wamejazana nje ya geti la Hospital wakilia na wengine wakitaka kuwaua mgambo hao ambao wamefichwa ndani ya jengo la Hospital hiyo.
Hali hiyo imepelekea polisi kuja kutuliza ghasia usiku huu.
Adha hiyo imetokea mida hii ya usiku baada ya kutokea mabishano kati ya Mgambo Na machinga na hivyo Kupelekea machinga huyo kupata kipigo Kikali kutoka kwa mgambo wa jiji hali iliyopelekea kujeruhiwa vibaya na hivyo kukimbizwa kwenye Hospitali ya Ngarenaro iliyopo jijini hapa.
Wananchi wamejazana nje ya geti la Hospital wakilia na wengine wakitaka kuwaua mgambo hao ambao wamefichwa ndani ya jengo la Hospital hiyo.
Hali hiyo imepelekea polisi kuja kutuliza ghasia usiku huu.