benzemah
JF-Expert Member
- Nov 19, 2014
- 1,503
- 2,977
Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Felician Mtehengerwa, amesema hali ya ushoga katika jiji la Arusha ni mbaya kwa sababu inakadiriwa zaidi ya vijana 400 wanajihusisha na vitendo hivyo na kuwataka madiwani kuvikemea katika maeneo yao.
Aidha, amesema kuanzia hivi sasa nyumba za starehe zikiwemo baa na 'pub' zinazoruhusu wateja wa aina hiyo kukaa katika maeneo yao, wamifiki watachukuliwa hatua kali za kisheria. Mtahengerwa alisema hayo jana katika kikao cha robo ya tatu cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya jiji la Arusha na kuwataka madiwani kushirikiana na jamil, haswa walezi na wazazi katika vita hiyo.
"Niwaombe sana madiwani tushirikiane na jamii katika maeneoyetu kwa kuhakikisha tunapinga vitendo vya mapenzi ya jinsia moja kwa sababu hali ni mbaya mo taarifa nilizonazo ni vijana zaidi ya 400 katika jiji la Arusha wanajihusisha na mapenzi ya jinsia moja. Hii ni hatari tushirikiane kukemea vitendo hivi viovu," alisisitiza.
Mtahengerwa alisema kwa mujibu wa taarifa alizonazo, mashirika mengine yasiyo ya kiserikali yanakuja kwa mgongo wa kutoa elimu kwa wananchi kumbe malengo yake kuratibu masuala ya ushoga kupitia shule za awali na vituo vya taasisi zao.
Alisema Jeshi la Polisi linamshikilia mtu mmoja, ambaye alisajili shirika lisilo la kiserikali kwa nia ya kutoa elimu, lakini likawa linafundisha mapenzi ya jinsia moja.
Kwa mujibu wa Mtahengerwa, kuna fedha nyingí zinatolewa kwa shule binafsi na taasisi za kijamii kuratibu na kufundisha mapenzi ya jinsia moja kwa madai ya kuwaelimisha watu hao kutambua hali zao.
"Juzi kuna mtu moja alibainika kusaiili taasisi va kijamii tulipoifuatilia tumegundua kibali amedanganya, pia taasisi hivo inajihusisha na vitendo vya kuwafundisha vijana mapenzi ya jinsia moja," alisema.
Aidha, aliwaomba wazazi na walezi kutambua jukumu la malezi ni la kwao hivyo wana wajibu wa kufuatilia mienendo ya watoto kwa njia ya kuzungumza nao athari za mapenzi ya jinsia moja.
"Niwaombe wazazi fuatilieni mienendo ya watoto wenu wa kike na wa kiume na ikibidi muwakague hali ni mbaya haiwezekani mtoto anatoka hovyo bila kuaga na kurudi mzazi hujui mienendo yake hili hata sisi katika makuzi hatukulelewa hivyo," alionya.
Aliongeza: Wazazi wetu kipindi tunakua walikuwa wanafuatilia sana mienendo yetu ndiyo maana vitendo viovu havikuwepo kwa kasi, lakini hivi sasa malezi tumewaachia wasaidizi wetu wa nyumbani na kibaya zaidi kila siku tunapata ripoti ya watoto wawil kulawitiwa katika jiji la Arusha na wengine kubakwa." Alisema serikali wilayani.
Arusha imetangaza vita dhidi ya vitendo hivyo na kuwataka madiwani kutoa ushirikiano kwa sababu kuna taasisi nyingi zina fedha kwa lengo la kuhamasisha ukiukaji wa maadili.
Aidha, amesema kuanzia hivi sasa nyumba za starehe zikiwemo baa na 'pub' zinazoruhusu wateja wa aina hiyo kukaa katika maeneo yao, wamifiki watachukuliwa hatua kali za kisheria. Mtahengerwa alisema hayo jana katika kikao cha robo ya tatu cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya jiji la Arusha na kuwataka madiwani kushirikiana na jamil, haswa walezi na wazazi katika vita hiyo.
"Niwaombe sana madiwani tushirikiane na jamii katika maeneoyetu kwa kuhakikisha tunapinga vitendo vya mapenzi ya jinsia moja kwa sababu hali ni mbaya mo taarifa nilizonazo ni vijana zaidi ya 400 katika jiji la Arusha wanajihusisha na mapenzi ya jinsia moja. Hii ni hatari tushirikiane kukemea vitendo hivi viovu," alisisitiza.
Mtahengerwa alisema kwa mujibu wa taarifa alizonazo, mashirika mengine yasiyo ya kiserikali yanakuja kwa mgongo wa kutoa elimu kwa wananchi kumbe malengo yake kuratibu masuala ya ushoga kupitia shule za awali na vituo vya taasisi zao.
Alisema Jeshi la Polisi linamshikilia mtu mmoja, ambaye alisajili shirika lisilo la kiserikali kwa nia ya kutoa elimu, lakini likawa linafundisha mapenzi ya jinsia moja.
Kwa mujibu wa Mtahengerwa, kuna fedha nyingí zinatolewa kwa shule binafsi na taasisi za kijamii kuratibu na kufundisha mapenzi ya jinsia moja kwa madai ya kuwaelimisha watu hao kutambua hali zao.
"Juzi kuna mtu moja alibainika kusaiili taasisi va kijamii tulipoifuatilia tumegundua kibali amedanganya, pia taasisi hivo inajihusisha na vitendo vya kuwafundisha vijana mapenzi ya jinsia moja," alisema.
Aidha, aliwaomba wazazi na walezi kutambua jukumu la malezi ni la kwao hivyo wana wajibu wa kufuatilia mienendo ya watoto kwa njia ya kuzungumza nao athari za mapenzi ya jinsia moja.
"Niwaombe wazazi fuatilieni mienendo ya watoto wenu wa kike na wa kiume na ikibidi muwakague hali ni mbaya haiwezekani mtoto anatoka hovyo bila kuaga na kurudi mzazi hujui mienendo yake hili hata sisi katika makuzi hatukulelewa hivyo," alionya.
Aliongeza: Wazazi wetu kipindi tunakua walikuwa wanafuatilia sana mienendo yetu ndiyo maana vitendo viovu havikuwepo kwa kasi, lakini hivi sasa malezi tumewaachia wasaidizi wetu wa nyumbani na kibaya zaidi kila siku tunapata ripoti ya watoto wawil kulawitiwa katika jiji la Arusha na wengine kubakwa." Alisema serikali wilayani.
Arusha imetangaza vita dhidi ya vitendo hivyo na kuwataka madiwani kutoa ushirikiano kwa sababu kuna taasisi nyingi zina fedha kwa lengo la kuhamasisha ukiukaji wa maadili.