Bushmamy
JF-Expert Member
- Aug 18, 2019
- 8,848
- 15,252
Stand ya magari madogo Kilombero Almaarufu kama stand ya Hiace ambazo daladala zote za mjini huanzia hapo haikidhi kabisa vigezo vya kuitwa stand ya daladala kutokana na sababu zifuatazo.
Hakuna vibao vinavyoonyesha kwamba hapa ndipo yanapopaki magari ya uswahili, Njiro au Usa, bali dereva anapaki popote pale ndani ya kituo hicho.
Sehemu ya kujikinga mvua na jua kwa abiria hakuna, mvua na jua vyote vyao.
Uzio, kituo hicho hakina Uzio unaoonyesha mwanzo na mwisho wa kituo,
Uboreshaji wa kituo chini hamna ni udongo tu hivyo wakati wa mvua ni matope na wakati wa jua ni vumbi tupu.
Uchafu, kituo ni kichafu kutokana na kukosekana kwa mapipa ya kuwekea taka, taka zinatupwa popote pale.
kituo hichi kipo katikati ya jiji
Hakuna vibao vinavyoonyesha kwamba hapa ndipo yanapopaki magari ya uswahili, Njiro au Usa, bali dereva anapaki popote pale ndani ya kituo hicho.
Sehemu ya kujikinga mvua na jua kwa abiria hakuna, mvua na jua vyote vyao.
Uzio, kituo hicho hakina Uzio unaoonyesha mwanzo na mwisho wa kituo,
Uboreshaji wa kituo chini hamna ni udongo tu hivyo wakati wa mvua ni matope na wakati wa jua ni vumbi tupu.
Uchafu, kituo ni kichafu kutokana na kukosekana kwa mapipa ya kuwekea taka, taka zinatupwa popote pale.