Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Hivi vichekesho vyako hua unavifikiria?

Mwisho wa msimu timu yenye mpira haramu ina magoli ya kufunga 71.

Timu yenye mpira mzuri ina magoli ya kufunga 58.

Mnachokasirika ni kushuhudia timu inageuka kua nzuri mbele ya macho yenu. Na siyo peke yako, mpo wengi sana. Na wote hua wanatulia wakiletewa takwimu
Fainali mlikutana na PSG inayojua mpira wewe mwenyewe shahidi mliishia kudefend maana mlipelekewa moto ile mbaya
 
Fainali mlikutana na PSG inayojua mpira wewe mwenyewe shahidi mliishia kudefend maana mlipelekewa moto ile mbaya
PSG inayojua mpira msimu wa 25/26 imefunga magoli 74.

Arsenal isiyojua mpira imefunga magoli 71.

Fainali PSG walipata goli kwa penati.

Halafu chelsea akafunga magoli 50
 
Kuumia kwa Caicedo napo pamechangia anasaidia sana kufanya kazi zote chafu na kulinda defenders moja kati ya mchezaji muhimu sana kwetu
Huyu hana lolote alijualo kazi ni kujikusanyia Kadi nyekundu na ndo maana kitaalam anaitwa " sheen kicker"
 
Huwezi kunielewa ukiwa umebeba bendera ya ushabiki, Arteta kaichukua team yenu ikiwa haina mbele wala nyuma mpo nje ya top 4 lakini akaisuka na mkampa muda wa ujenzi ndio kaifanya iwe hii Leo mnacheza kwa identity yake kaona mpira mzuri hauwezi kuwalipa kwa sababu hamna wachezaji wenye viwango vikubwa wa kuwapa Mataji ndio maana akaamua acheze soka haramu. Huwezi kucheza mpira wa mzuri na hapo hapo unataka matokeo ukawategemea Kai, Madueke,Martinell, Jesus, Zubimend,Ben White, Eze n.k ndio maana akaamua kuchagua njia haramu kushinda taji utapinga lakini hiyo haibadilishi nyie mna wachezaji wengi wa kawaida wachezaji wengi kwenu wakija Chelsea namba hawapati na ndio maana tunawauziaga magarasa.
Arsenal ina wachezaji wa kawaida kulingana na mtazamo wako haya hebu tuambie ni lini mara ya mwisho Chelsea kuifunga Arsenal na kuondoka na point zote 3 ukizingatia Arsenal ina average players
20260622_201441.jpg
 
Ila wewe jamaa 😅

Hii timu ishakua na beki Maitland-Niles, Mari, Sokratis.

Ishakua na kiungo Guendouzi, ishakua na beki Soares, imeshacheza ikitegemea kiungo Ramsay ndiye afanye maajabu ya kufunga. Na siyo forwards.

Hii timu imeshakua na beki Luiz, imeshacheza ikimtegemea kipa Cech na Leno.

Hii timu imeshaingia uwanjani huku mpinzani akiwa amejiandaa kuchukua matokeo na anayachukua.

Hii timu imeshacheza huku inaanza kupata magoli mawili lakini mechi inaisha sare au tunafungwa.

Wewe huwezi kujua haya kwakua unaangalia livescore matokeo hauangalii mechi na unaangalia stats za mchezaji.

Mimi nisipoangalia mechi nasema ili mtu aelewe mtazamo wangu unapotokea, kama unaangalia takwimu na rekodi na unadai wachezaji wa Arsenal hawana viwango hakikisha na makocha wa timu za taifa wanapata huu ujumbe.

Saka kamuweka benchi Palmer, akamuweka benchi Madueke. This time around hata timu ya taifa hajaitwa, mnadai mna forward mzuri hata hiyo timu ya taifa hajagusa.

Unaongea sana broken mzee
Jamaa huwa anaongea pumba tupu tu anatumia akili za kulima matikiti kuchambua mpira.

Anadai Arsenal ina wachezaji wa kawaida na hata hakumbuki mara ya mwisho Chelsea kuifunga Arsenal 😂
 
Ila we jamaa haupo serious yaani unamfunga Aston villa mbovu kwa mbinde halafu unajitapa utafunga Chelsea 🤣
Kila mgonjwa anatibiwa kwa dawa yake huwezi ukampasua mtu kichwa kwa ugonjwa wa mguu
last time chelsea kuifunga arsenal ww hujaaanza kufanya mapenzi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom