Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal akishinda leo ana 90% ya ubingwa.
Leo ni fainali kwa Arsenal. Kwa nini? Mechi nyingine anapiga na Burnley ambayo ni wachovu walioshuka daraja, tena nyumbani. Mechi ya mwisho anakipiga na Palace kwao. Itakuwa ni siku ya Jumapili, na Jumatano itakayofuata Palace atacheza fainali za Europe, hivyo sidhani kama ataizingatia sana hiyo ya Arsenal. Hivyo mechi ya leo ni kama fainali kwao.
 
Kwenye mechi zenu zilizobaki mie nawekeza pesa ili kuvuna mamilioni maana mko kwenye ile moment hamtakiwi kutoa droo au kufungwa.
Msiniangushe kenge maji nyie
Come On You Gunners,
Arsenal kombe lao mwaka huu. Mechi ya leo sioni West Ham wakishinda japo ni ngumu sana. Yes, wanacheza kama fainali ili wasishuke daraja lakini Arsenal wakitulia watawapiga si chini ya goli 3. Hata wakitoa draw bado wana nafasi ya kushinda ligi kwa tofauti ya magoli kwa sababu mechi zake zilizobakia siyo ngumu sana. Burnley keshateremka na Gunners wanachezea nyumbani. Mechi ya mwisho na Palace, Palace watachezesha team B kwa sababu watakuwa wanajiandaa kwa fainali ya Europe siku mbili baadae. Hata kama atatoa draw leo, mechi nyingine akiweza kupata goals 3 na 4. City hawezi kumfikia kirahisi.
 
Leo ni fainali kwa Arsenal. Kwa nini? Mechi nyingine anapiga na Burnley ambayo ni wachovu walioshuka daraja, tena nyumbani. Mechi ya mwisho anakipiga na Palace kwao. Itakuwa ni siku ya Jumapili, na Jumatano itakayofuata Palace atacheza fainali za Europe, hivyo sidhani kama ataizingatia sana hiyo ya Arsenal. Hivyo mechi ya leo ni kama fainali kwao.
Hili liko wazi, leo arsenal akishinda ana ubingwa kwa 90%...
Hapa ndio muhimu arsenal akaze leo
 
Kimahesabu jana City asingeshinda Arsenal ilibidi kushinda leo na mechi ijayo tu.

Ya kufungia msimu ilikua haina haja tena. Na bado hizo hesabu zipo vilevile. City hajadrop points jana ila akipoteza mechi ijayo na Arsenal ikishinda leo means ashinde na game inayofuata tu
Sahihi... .wacha tuone ... Pep naona keshatupa taulo, mshindwe nyie sasa !

Game ya Leo mki_draw tu imekula kwenu
 
Huyo Burnley waliyesema mwepesi anamuongoza Villa chuma kimoja.

Matokeo yakibaki hivi itakua poa zaidi kwakua yatamtamanisha Bournemouth kupambana akishinda anamshusha Villa nafasi ya tano
 
Lineup ni ile ile, Raya, White, Gabi, Saliba na Calafiori kwenye ulinzi af skelly, Rice kwenye kiungo pamoja na Eze, Saka, Trossad na Gyokeres mbele, COYG!!!
 
Leo draw tuu, Ila Arsenyembo anakuja kuvunja huu utaratibu kwa kukazwa 😂
 
Hiki ndio kikos cha kumaliza nacho ligi, na uefa labda changes ya timber au hincpie

Westham leo inabidi afe kikatili sana ili pep akate tamaa mapema
Screenshot_20260510_175402_FotMob.jpg
 
Leo hii city anaomba watu wamfanyie kazi ili achukue ubingwa
Kauli za kila mtu ashinde mechi zake hazipo tena.

Kenge na nyumbu wapo sitaki nataka, wanataka arsenal achukue ubingwa ili pep na city yake yasifanye ligi kama ya ukoo wa waarabu.
Pia hao hao hawataki kuona arsenal ikifanikiwa, sijui wanahofia nini. PUMBAVU
 
Back
Top Bottom