Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Tunazungumzia ubora ama ? Usajili ni kitu kingine na matokeo ya huo usajili ni kitu kingine! Point yangu ni kuwa mnaona kama mmeshinda vita ya kumpata Victor kumbe mlikuwa wenyewe, hakuna timu kubwa iliyomhitaji ikamkosa ! Ni kama kujitekenya na kucheka mwenyewe !
Siyo kwamba tulikuwa wenyewe tunaomtaka. Tulimtaka wengi ila yeye alikomaa kuwa anataka kuja kwetu tu, hivyo wengine wote, mfano Manchester United, wakajikuta hawana nafasi ya kumchukua.
 
So sad ndio nini???
There is no single Arsenal fans with Brian.

Tofauti ya Arsenal na Real Sociedad alyotoka huyo Zubimendi ni different league tu lakini vingine vyote mpo sawa TROPHYLESS AURA.
Sawa lakini haibadili mtazamo wa kwamba Slot ni kilaza 😁
 
Kuna marekebisho kidogo. Hapana, hatujaongezewa bei kwa Viktor bali tumeshushiwa bei tena kiasi kikubwa tu.

Viktor ana release clause ya €100m. Sisi tumeuziwa kwa €63.5 + €10m kwa add-ons. Akitimiza hizo add-ons maana yake ni tutalipa €73.5m, ambayo ni chini ya 3/4 ya bei yake. Ni gharama nafuu kuliko Ekitike, Šeško, Isak, Mbeumo, Matheus Cunha na hata Eze, ikiwa tutampata.

Sioni kama ni usajili mbaya ukizingatia hayo. Hii imetuzewezesha pia kuwekeza kwenye kipa mpya, beki mpya na mido wawili wapya kusaidia timu kuwa na mbadala.
Yetu macho,,,, tuombe huu usajili uende vizuri apafom vyema !
 
Siyo kwamba tulikuwa wenyewe tunaomtaka. Tulimtaka wengi ila yeye alikomaa kuwa anataka kuja kwetu tu, hivyo wengine wote, mfano Manchester United, wakajikuta hawana nafasi ya kumchukua.
Utd usiihesabie, kwanza hawana michuano ya ulaya(hii inapunguza ushawishi kwa wachezaji ), pia wanajitafuta, kimsingi wana matatizo yao mengi tu ! Mm namaanisha timu kama Madrid, bayern, barca, juve, city , liver ,,, kuna tumu ilimtaka hapo ikamkosa ?
 
Utd usiihesabie, kwanza hawana michuano ya ulaya(hii inapunguza ushawishi kwa wachezaji ), pia wanajitafuta, kimsingi wana matatizo yao mengi tu ! Mm namaanisha timu kama Madrid, bayern, barca, juve, city , liver ,,, kuna tumu ilimtaka hapo ikamkosa ?
Hapo mpaka nipekue mitandaoni kwa kweli. Habari kubwa ni Manchester United na timu za Saudia.
Hizo timu kubwa zingine tayari zina akina Kane, Lewandowski, Mbappe...sidhani kama walikuwa wanatafuta strikers. Timu ninayofikiri ilikuwa inatafuta striker hapo ni Liverpool ambao wanamtaka Isak na wamemchukua Ekitike. Nafikiri sababu kuu pia ya kutaka striker kwao imekuja baada ya kuondokewa na Jota (RIP), la sivyo sidhani kama wangetaka striker mwingine msimu huu. Na bado wasingempata Gyokeres maana jamaa ameikubali project yetu kinoma.
 
Dogo ana upepo, kakubalika na mashabiki
IMG_20250723_185840.jpg
 
So sad ndio nini???
There is no single Arsenal fans with Brian.

Tofauti ya Arsenal na Real Sociedad alyotoka huyo Zubimendi ni different league tu lakini vingine vyote mpo sawa TROPHYLESS AURA.
Dah umetish sana 😁
 
Arsenal's summer so far:

Kepa Arrizabalaga: £5M.
Martin Zubimendi: £56M.
Christian Nørgaard: £12M.
Noni Madueke: £52M.
Viktor Gyökeres: £63.5M
Christian Mosquera: £17M
Eberechi Eze

Total: £205.5M and counting
View attachment 3415001
Huyu Madueke inaonekana kanunuliwa kwa upuuzi wa Arteta.

Ukimuangalia Berta anaonekana kichwani zimo na sio mtu wakupigwa.

Yule mjinga mpanga koni wetu anaweza kuwa ni dalili wa wachezaji pia.

Anachukua asilimia zake kama ile kipara iliyokuwepo nyumbu.Iliwapelekea garasa nyingi kwelikweli kwa bei ya hatari na majinga yakajaa.
 
So sad ndio nini???
There is no single Arsenal fans with Brian.

Tofauti ya Arsenal na Real Sociedad alyotoka huyo Zubimendi ni different league tu lakini vingine vyote mpo sawa TROPHYLESS AURA.
Andika tu kiswahili ndugu.

Brian ndio inamaanisha nini kwenye sentensi yako.

Unaandika pumba halafu unazikazia kwa kiingereza ili wajinga wenzio waone umeandika la maana wakupongeze au sio.
 
Zubimendi ananikumbusha Vitinha na Neves dhidi yetu na PSG, touches nyingi zinazoipa timu control ya kumkera mpinzani, kama kaishiwa pumzi afu bado unamkaba koo.

Hawa Man u mbona itakuwa aibu siku tukikutana, hapo bado EZE
 
Dogo ana upepo, kakubalika na mashabikiView attachment 3416074
Kakubali katoa sehemu ya mshahara wake ili dili litimie

Changuo lake namba 1 hadi namba 5 ni arsenal tu. Nyumbu akatia pua yake akakataliwa live. He only wants to play for arsenal

Ameshinikiza Sporting cp ili dili lake likamilike, aligoma kurudi kwenye club

Wakala wake nae kakubali kupunguza kamisheni yake kisa dili likamilike
 
Zubimendi ananikumbusha Vitinha na Neves dhidi yetu na PSG, touches nyingi zinazoipa timu control ya kumkera mpinzani, kama kaishiwa pumzi afu bado unamkaba koo.

Hawa Man u mbona itakuwa aibu siku tukikutana, hapo bado EZE
Zubimendi na merino ndio midfield engine ya hispain. Epl safari hii watatugea lawama tu
 
Back
Top Bottom