Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Hii ni timu aliyorithi Mikel Arteta kutoka kwa Unai Emery afu unamfananisha na Slot aliyerithi timu ya klopp ikiwa na Van dijk, Trent, Konate na Mo salah, ukumbuke misimu miwili mbele mwamba akaingia kwenye title contention na monster Pep Guardiola akiwa na peak squad iliyochukua treble, ukisema Arteta mjuaji, ofcoz ni mjuaji sababu kweli anajua.
Hio hio timu aliyorithi Mikel Arteta kutoka kwa Unai Emery ndio iliyompatia Arteta the one and only trophy katika maisha yake ya ukocha, Kiwigi kabeba FA Cup 2020 kwa kikosi chote cha Unai Emery baada kumfunga Chelsea kwenye fainali.
Tukiwaambia shida yenu kubwa mashabiki wa Arsenyau ni Mentality mnao kama vile tunawaonea.
Sasa hio miaka yake 6 Arteta hapo Arsenyau ameongeza nini au wachezaji gani waliomsaidia hata kubeba Carabao?
Badala yake mnakaa na kushangilia title contender kwa misimu mitatu mfululizo pasi na kombe lolote, binafsi nina uhakika Unai Emery angeaminiwa na kupewa muda kama alivyopewa Tetea kiwigi sasa hivi Arsenyo ingekua na kati ya Epl au Uefa mkononi.
Hio nafasi ya pili mnayodanganyika nayo kila msimu hata Ole Gunnar Solskjær alitimuliwa akiwa kamaliza nafasi ya pili.
 
Ndio ujue kwamba sisi sio wa kupigwa Bali Brighton ndio chimbo letu zuri la bidhaa tunazohitaji
Huenda Maresca akabadili mambo zaidi. Tatizo lenu siyo kuwa na wachezaji wabovu. Mmekuwa na wachezaji wazuri tangu enzi za Potter. Nakumbuka mimi mwenywewe nilikuwa naamini Potter atafanya makubwa sana na kile kikosi ila hakuweza na mmeendelea hivyo mpaka kumpata Maresca. Pia mmekuwa na majeruhi kwa wachezaji wazuri kama Nkunku.

Sisi mmetupiga hela kizembe kwa kututupia wachezaji wenu hovyo, ila hao hao wachezaji, kwa miujiza flani, tumeweza kufanya nao mambo makubwa kuliko uwezo wao.
 
Huenda Maresca akabadili mambo zaidi. Tatizo lenu siyo kuwa na wachezaji wabovu. Mmekuwa na wachezaji wazuri tangu enzi za Potter. Nakumbuka mimi mwenywewe nilikuwa naamini Potter atafanya makubwa sana na kile kikosi ila hakuweza na mmeendelea hivyo mpaka kumpata Maresca. Pia mmekuwa na majeruhi kwa wachezaji wazuri kama Nkunku.

Sisi mmetupiga hela kizembe kwa kututupia wachezaji wenu hovyo, ila hao hao wachezaji, kwa miujiza flani, tumeweza kufanya nao mambo makubwa kuliko uwezo wao.
Mmefanya Mambo makubwa Kama yapi? Mbona unanichekesha
 
Mmefanya Mambo makubwa Kama yapi? Mbona unanichekesha
Nafasi ya 2 misimu 3 mfululizo. Msimu uliopita tumetolewa UCL kwenye hatua ya nusu fainali. Haya ni mafanikio makubwa kimpira kuliko UEFA Conference league na hata CWC. Asikudanyanye mtu yeyote kuwa Conference league title ni kubwa kuliko hizo za Arsenal.

Kijana wa miaka 16 aliye na Div 3 form 4 si sawa na kijana wa miaka 16 aliyefanya mitihani ya darasa la saba na kuwa kinara wa darasa hilo.
 
Tuna-test mitambo
1000444384.jpg
 
Nafasi ya 2 msismu 3 mfululizo. Msimu uliopita tumetolewa UCL kwenye hatua ya nusu fainali. Haya ni mafanikio makubwa kimpira kuliko UEFA Conference league na hata CWC, asikudanyanye mtu yeyote kuwa Conference league title ni kubwa kuliko hizo za Arsenal.

Kijana wa miaka 16 aliye na Div 3 form 4 si sawa na kijana wa miaka 16 aliyefanya mitihani ya darasa la saba na kuwa kinara wa darasa hilo.
Kwahiyo hayo kwenu ndio mafanikio kwa team ambayo mshajipata basi mnasafari ndefu sana
 
Madueke Efusiii tena? Yaani hata heshima ya jina hamtupi? Ligi ianze tu tuendelee kuwashushia vichapo ili muendelee kutamba na vikombe.
Usiishi kwa mazoea blaza, shauri yako! Jua mnaenda kukutana na Bingwa wa vitimu vyote vya hapa duniani. Usiseme sijakutahadharisha. Muulizeni mbabe wenu PSG
 
Back
Top Bottom