Arsenal sasa hivi tunacheza kama kipindi cha kwanza Arteta alivyotupokea.
Ni back passes na sideway passes.
Kama umeangalia mechi utagundua kila Martinelli akipata mpira Calafiori alikua anaoverlap kwa speed akitaka agewe thru ball Martinelli badala ya kupeleka mpira anachagua kupiga sideway pass.
Sehemu ambayo hakutakiwa kupeleka mpira ndiyo akampelekea Trossard, kwenye move ya 3 against 2.
Rice akipata mpira unaona Kai kule mbele anafanya run inayohitaji long ball, Rice anachofanya ni kupiga side way pass.
Jesus anapata mpira, Ben anaoverlap Jesus hapeleki mpira anapiga back pass.
Hii style ya mpira ilikua tunafungwa timu pinzani ikiamua ku-high press na intensity movements kuja mbele. Ndiyo hichi kipindi ilikua tuna possession kubwa ila tumefungwa 1 - 0 au 2 - 1.
Notice kwamba hata Shakhtar alivyorudi kipindi cha pili akaamua kua sasa nafanya msako alipata fursa nyingi tu mbele ya goli. Kilichotubeba ni defense hakuepo Mustafi, Luiz, Sokratis na kipa Cech.
Jambo jingine ni hili. Tuna kipa mzuri sana. Sitaelezea chochote ila tuna kipa mzuri sana.