Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Kumbukuka dk ya 76 wametoka kwa Villa Onana na Digne wakaingia Meaten na Barkley. Inaelekea kila wakitoka kubadili wanapigwa
 
Dakika 90 zimekamilika Arsenal wakiwashughulikia waliowakosesha ubingwa 2023/24 kwa jumla ya magoli 2 kwa 0 yakifungwa na Leandro Trossard na Thomas Partey kipindi cha pili, Arsenal wakiwa ugenini Villa Park. Msimu uliopita Arsenal aligawa pointi zote 6 kwa Villa hivyo kumfanya ashindwe kupata alama za kutosha kutwaa ubingwa.

Baada ya mechi mbili kuchezwa leo Arsenal anasimama ktk nafasi ya 3 katika msimamo wa EPL akiwa na alama 6 na tofauti ya magoli 4 wakati vinara ni Man City wakiwa na alama 6 na tofauti ya magoli 5 huku Brighton akiwa na alama 6 na tofauti ya magoli 4 katika nafasi ya 2.

Ni hayo tu kutoka Villa Park
 
Ingawa mmeshinda kibahati bahati ila dogo Rogers fundi sana aisee,
Hii ni product ya West Bromwich Albion Academy, dogo anateleza kama kambale, kijana anakatisha katikati ya msitu utafikiri yupo kwenye lami, hakika hapa Aston Villa wameramba dume.
images-8.jpg
 
Back
Top Bottom