Dakika 90 zimekamilika Arsenal wakiwashughulikia waliowakosesha ubingwa 2023/24 kwa jumla ya magoli 2 kwa 0 yakifungwa na Leandro Trossard na Thomas Partey kipindi cha pili, Arsenal wakiwa ugenini Villa Park. Msimu uliopita Arsenal aligawa pointi zote 6 kwa Villa hivyo kumfanya ashindwe kupata alama za kutosha kutwaa ubingwa.
Baada ya mechi mbili kuchezwa leo Arsenal anasimama ktk nafasi ya 3 katika msimamo wa EPL akiwa na alama 6 na tofauti ya magoli 4 wakati vinara ni Man City wakiwa na alama 6 na tofauti ya magoli 5 huku Brighton akiwa na alama 6 na tofauti ya magoli 4 katika nafasi ya 2.
Ingawa mmeshinda kibahati bahati ila dogo Rogers fundi sana aisee,
Hii ni product ya West Bromwich Albion Academy, dogo anateleza kama kambale, kijana anakatisha katikati ya msitu utafikiri yupo kwenye lami, hakika hapa Aston Villa wameramba dume.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.