MalcolM XII
JF-Expert Member
- Mar 19, 2019
- 5,262
- 14,283
Ishu sio Solanke kumsukuma Raya, hakukuwa na msukumo wa namna hiyo.Ben white alikuwa anafanya vurugu kwa kipa mwanzoni mwanzoni na faulo zilikuwa zinatolewa hivyo tukawa hatupati faida yeyote. Baada ya hapo siku hizi anajitahidi kwenda tu kusimama mbele ya kipa ili kipa asimpite bila kumsukuma na mara nyingi anakubali kusukumwa tu au ile sekunde ya mwisho, mpira ukiaribia box, yeye anaondoka kabisa na kumpisha kipa maana anajua hata akianguka kwa kusukumwa na kipa hatutapewa penati. Hata hivyo, mpaka hapo anakuwa ameshamchanganya kipa na linabaki tu suala la Saliba, Gabriel au Kai kupiga vichwa magoli yaingie.
Kwa Bournemouth, Solanke alimsukuma kidogo Raya wakati anaenda kupambania mpira. Hiyo hairuhusiwi. Ajabu ni kwamba Gabriel ama Saliba alikuwa anavutana na akamvuta Billing na kumuangusha kabla tu ya Solanke kumsukuma Raya. Sijui kwa nini VAR hawakuangalia hilo na kuwapa Bournemouth penati.
Tatizo Solanke aliushika mkono wa kushoto wa Raya kabla hajafanya ile save, tena aliingiza mkono ndani kabisa. It's obvious ni foul. Nikipata video footage nitaileta hapa.