Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Kai na arteta sijui wana ushemeji.

Timu inahitaji striker, ambae atashuka kuchukua mipira na kusogea nayo juu, striker ambae anasumbua mabeki akiwa na mpira, stiker sharp

Naandika haya, bwana kai kapiga pasi ya goli

Goli linachekiwa.....
Ni chumaaàaaa,
Chuma ya pili.

Ama kweli hakuna ng'ombe asiefaa, kai kasaidia chuma ya pili. Ila bado tunahitaji JESUS
Una chuki binafsi na kai... Kwani kuna shabiki wa arsenal ambae hajui kama arsenal inahitaji mshambuliaji mzuri wa kati. Mtu akikosea mkosoe akifanya vizuri mpe sifa zake. Kama siyo mtu wa boli mzer
 
I'd choose Jesus all day over Kai. Kai afunge au asifunge kwangu haibadili kitu.
Uchezaji wake kwa ujumla hawezi kumuweka level moja na Jesus.

Siwezi kukulaumu, magoli/matokeo mazuri ndio yanafika madhaifu yake huenda hujaliona hilo mpaka leo.
Jesus tukubali tukatae ila kwa sasa hatupaswi kumtegemea aanze kama CF, anaweza kuanza kama RW/LW
 
kai na jesus ni wachezaji wawili tofauti.. kwa jesus yeye namuona zaidi ni wide player ama acheze na twin striker mwenzie.

kwa hii system.. pamoja na jesus kuwa ni bora zaidi kwenye general play kuliko kai ila ataonekana ni mzururaji tu.
 
Hii turn aliyoifanya partey dk ya 9 ni moj kati ya vitu namisi toka kwake, timu yoyote inayoshambulia tokea chini inajitaji kiungo wa namna hii, anapokea mpira kwa kipa anaturn na kupiga pasi ya KUSHAMBULIA.

huyu tomiyasu huwa ana mawenge na game kubwa nini, atulize presha.
Anakua na mapepe anakosa sharpness, nakumbuka last season goli la kdb
 
Siku akianza mbona hatuoni impact yake, binafsi namkubali kwenye kuchezesha timu ila sio kutafuta magoli, he's not clinical hataaa.
Kwa kuaminiwa alikoaminiwa kai, nae angeaminiwa hivyo, nilikuwa naona makubwa mno toka kwake.

Kai kufika leo, kocha kamuonesha imani kubwa mnoo, wakati mashabiki wanamlalamikia kai yeye alikuwa kwake bega kwa bega.

Rudisha kumbukumbu msimu uliopita kabla jesus hajaumia, alikuwa na kiwango kikubwa mnooo, mpaka alipokuja kuumia, aliporudi hakuaminiwa tena, akawa mtu wa sub tu, msimu huu umeanza ni yale yale, binafsi kwa mpira aliokuwa nao jesus nina imani nae kubwa mnoo.
 
Ukitaka Kai afanye anayofanya Jesus, utaumia kila siku. Kai ana majukumu yake mengine kabisa yani.

Cesc Fabregas anasema hivi kumzungumzia Kai: "I don't like to talk about myself, but he reminds me a bit of me in Barcelona. I used to play the two roles that he plays as a false nine and a number eight. I know exactly how it feels. "
 
Ben White Kona zote anasimama mbele ya Kipa na bado VAR wanagoma ku intervene. Spazi kanyimwa tuta then against the run of play saka anafunga. Arsenali anaandaliwa ubingwa wa mezani.
Imeniuma sana ile, yaani rafu 2 ndani ya box halafu refa na VAR yao wanajifanya kupotezea.
Poleni sana ndugu zangu wa Spurs, leo marefa na VAR zao wapo kwa ajili ya kuwatoa mchezoni, tena kuna kila dalili ya kuwatafutia red card ili wawaandalie Arsenyo ubingwa wa mezani, lakini hata hilo pia halitawezekana maana dhuluma ya waziwazi mnayofanyiwa leo haina tofauti na ile sisi tuliyofanyiwa katika mechi ya kwanza pale Emirates, hivyo hii dhuluma nawaahidi tunaenda kuwalipia kwenye dimba la Trafford mtafurahi wenyewe na roho yenu.
 
Back
Top Bottom