Flano
JF-Expert Member
- Aug 7, 2019
- 5,870
- 16,425
Mwisho wa siku pamoja na GD nyingi bado mtatoka trophyless mkijazana ujinga wa tupo false 4( phase 4) mara false 5 kutakuwa hamna tofauti kati ya position ya 2 na 10 then tutaangalia individual performance nadhan hamna aliyemzidi isak timu au trippier timu yako nzima.


Hawa Kima kila msimu wanatoka Mikono mitupu halafu kwa aibu wanatafuta vitu visivyo na faida yoyote vya kujivunia navyo, mwaka juzi yamemaliza ligi nafasi ya 5 Masingeli akawadanganya kua kwao nafasi ya 5 haina tofauti yoyote na ubingwa maana wao ndio wanaongoza kwa cleanshit


Msimu ulioisha wameongoza ligi kwa siku 258 halafu kombe wakabeba wengine, Masingeli akawaambia watembee vifua mbele maana timu yao ndio inayoongoza kwa Pressing & Overloading pamoja na Position Interchange



Msimu huu wakati unaanza Masingeli Akawadanganya tena kua Arsenyo ya msimu huu ndio ile Arsenyo ya Asali na Maziwa waliokua wakiisubiri kwa miaka 40 iliyopita na tayari wameshafika nchi ya ahadi hivyo msimu huu lazima Arsenyo itabeba treble



Mashabiki waliokua na wasiwasi juu uwezo ya timu yao kubeba Uefa Masingeli akawahakikishia kua hakuna kombe rahisi duniani kubeba kama hilo kombe la Uefa, tena akawatolea mfano wa Madrid ni timu mbovu ambayo haifikii hata robo ya ubora wa timu ya Arsenyo lakini wana Uefa 14



Msimu huu waliodanganyana wanabeba treble wanamaliza pia mikono mitupu halafu utawasikia kina mkorea na arsenal2004 wanawajaza ujinga wenzao kua wanapaswa wajivunie timu yao maana ndio timu yenye GD kubwa kuliko timu yoyote duniani







