


Mkuu
Castr unachosema ni kweli haswa ila ni kwa hukohuko kwao Uingereza.
Ila kibongo bongo mashabiki wa Man Utd na Arsenal ni wengi kuliko mashabiki wa timu nyingine yoyote kwenye Epl.
Nenda kwenye kibanda umiza fanya research utagundua mashabiki wa Liverpool hawafiki hata nusu ya mashabiki wa Arsenal na Mashabiki wa City hawafiki hata robo ya mashabiki wa Arsenal.
Wingi wa mashabiki ndio unaoleta uhasimu katika mazingira husika.
Kibongo bongo hauwezi kuona uhasimu wowote kati ya Arsenal na Spurs sababu hapa kwetu mashabiki wa Spurs ni wa kuhesabu, hata uhasimu wa Arsenal na Chelsea hapa kwetu sio mkubwa ki vile kwa sababu hapa Bongo mashabiki wengi wameanza kuijua na kuishangilia Chelsea baada ya Chelsea kununuliwa na Abramovich.
Hivyo ni sahihi kibongo kuona uhasimu mkubwa zaidi kati ya Arsenal na Man Utd hata kama uhasimu huo sio mkubwa kivile kwa huko kwao Uingereza.
Kibongo bongo hauwezi kuona uhasimu kati ya Barcelona vs Espanyol, Real Madrid v Atletico Madrid, Bayern Munich vs Dortmund, Psg vs Marseille, Napoli vs Roma, Juventus vs Torino.