Standards are here.
Nyumbu wamefungwa roho inamuuma.
Anakuja kujifariji kua Arsenal siyo wa kwanza.
Wa kwanza ni nani? Liver.
Nyumbu na Liver ni mahasimu wakubwa. Ila watoto walioanza kushabikia mpira baada ya kucheza game la FIFA hawajui hilo.
Hawajui jinsi gani Ferguson inamkereketa anapoona liver inatawala mpira wa EPL, hawajui Erik alipata kazi baada ya kuahidi kumaliza utawala wa Liva.
Mahasimu wakubwa wengine ni City watoto wadogo hawajui Ferguson alitishia kumchania mkataba Evra kwakua alionekana matembezini na Tevez. Hawajui kila kombe la City ni tusi kwao, kila kombe la liva ni aibu yao imeongezwa juu ya aibu nyingine.
Shabiki mmoja wa nyumbu yupo Masaki anacheza ps 5 anazima anascreenshot msimamo wa ligi anatuma na emoji kufurahia liver au city kuongoza ligi.
WTF?
Ni sawa shabiki wa Arsenal nifurahie kenge au spurs kuongoza ligi. Ni haiwezekani. Na huyo ni average fan wa nyumbu humu JF, ndiyo sababu nawachukulia hawajui mpira, hawaijui klabu yao. Nadra sana unikute najibu komedi zao