✍🏻Control spaces , shinda mipambano yako , fanya runs nzuri , kuwa sharp uwanjani ni vitu ambavyo wamefanya kwa usahihi sana dhidi ya Newcastle leo na kuwafanya vijana wa Eddie Howe kucheza mdundo wao
✍🏻Distance : Hii kitu muhimu sana , jinsi Arsenal walivyohakikisha distance kutoka mstari mmoja mpaka mwingine na mchezaji kwa mchezaji kuwa ndogo sana , faida yake ?
1: Iliwanyima muda na nafasi kwenye mpira Newcastle na kushindwa kupita ndani . Matokeo yake wakalazimishwa kufanya makosa au kupiga mipira mirefu ambayo Arsenal ilikuwa rahisi kwao
2: Inasaidia sana kufanya pressinf nzuri haraka pale walipokuwa wanapoteza mpira
3: Inasaidia ku control mechi kwasababu inakupa options za pasi ambazo sio za umbali mrefu hivyo mpira kutembea vizuri
✍🏻Yes najua kuna namna makocha wanasisitiza timu kuanza nyuma lakini kama pasi haipo kwanini usianze mipira mirefu kwa mawinga halafu uanzie hapo ? Newcastle mara kadhaa walijipiga risasi mguuni kwa risk pasi zao hasa ukizingatia Arsenal walikuwa sharp sana
✍🏻Arsenal waliwaonesha Newcastle sura yao ya pili kwamba nini wanaweza kufanya wakiamua kukabia chini ... compact 4-4-2 ambayo inafunga spaces , ndani hakuna njia , Newcastle walipata tabu sana kuwafungua Arsenal hasa kwa kutumia ile silaha yao ya combination play ( Bruno - Trippier - Almiron )
NOTE
1: Jorginho ali control sana mchezo hasa kipindi cha kwanza , simple passing na humuoni akiliacha eneo lake tupu
2: Arsenal kwenye mipira iliyokufa 🔥 hakika Nicolas Jover anafanya kazi vizuri
3: Leo Arsenal walikuwa wanacheza kama vile wana hasira na Newcastle , mbinyo huo 🔥😀
4: Sifa ya Newcastle ya msimu uliopita ya kuzuia vizuri msimu huu imepotea ... wameruhusu magoli 4 mechi kadhaa mpaka sasa
5: Bukayo Saka sasa hivi ukijaa tu kwenye mfumo unaokota kambani
6: Licha ya kurusu magoli 4 lakini performance ya Karius huwezi amini kama alikuwa hachezi 🤝
7: Mbio za ubingwa bado za moto sana
FT: Arsenal 4-1 Newcastle