Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Masingeli akijifanya kuibuka na kuanza kucomments humu kabla game kuisha basi goli zote zitarudi na nyingine zitaongezeka.
Daaaahhh ila hawa Newcastle walianza ligi kwa mbwembwe sana sijui hata kitu gani kimewakuta, ukiachana na ile nafasi aliyoipoteza Almiron sijui hata kama wamepata attempt nyingine.
Dakika 45 attempt moja, On target 0 hawa sio nyukesto ninaowajua mimi.
Hao hao wanamaliza juu yenu, Newcastle sio wabovu tatizo aliekutana nae ni wamoto zaidi
 
Masingeli akijifanya kuibuka na kuanza kucomments humu kabla game kuisha basi goli zote zitarudi na nyingine zitaongezeka.
Daaaahhh ila hawa Newcastle walianza ligi kwa mbwembwe sana sijui hata kitu gani kimewakuta, ukiachana na ile nafasi aliyoipoteza Almiron sijui hata kama wamepata attempt nyingine.
Dakika 45 attempt moja, On target 0 hawa sio nyukesto ninaowajua mimi.
Tunaomba radhi ndugu zetu leo kumekuwa na goli chache🤠🤠...tunaahidi tutalitatua hili tatizo mechi ijayo...asante kwa kuwa nasi usiku wa leo tukisheherekea kilele cha Tetaball
 
Look away, Man Utd fans
Snapinsta.app_429665001_853392483256138_4088046944134191133_n_1080.jpg
 
✍🏻Control spaces , shinda mipambano yako , fanya runs nzuri , kuwa sharp uwanjani ni vitu ambavyo wamefanya kwa usahihi sana dhidi ya Newcastle leo na kuwafanya vijana wa Eddie Howe kucheza mdundo wao

✍🏻Distance : Hii kitu muhimu sana , jinsi Arsenal walivyohakikisha distance kutoka mstari mmoja mpaka mwingine na mchezaji kwa mchezaji kuwa ndogo sana , faida yake ?

1: Iliwanyima muda na nafasi kwenye mpira Newcastle na kushindwa kupita ndani . Matokeo yake wakalazimishwa kufanya makosa au kupiga mipira mirefu ambayo Arsenal ilikuwa rahisi kwao

2: Inasaidia sana kufanya pressinf nzuri haraka pale walipokuwa wanapoteza mpira

3: Inasaidia ku control mechi kwasababu inakupa options za pasi ambazo sio za umbali mrefu hivyo mpira kutembea vizuri

✍🏻Yes najua kuna namna makocha wanasisitiza timu kuanza nyuma lakini kama pasi haipo kwanini usianze mipira mirefu kwa mawinga halafu uanzie hapo ? Newcastle mara kadhaa walijipiga risasi mguuni kwa risk pasi zao hasa ukizingatia Arsenal walikuwa sharp sana

✍🏻Arsenal waliwaonesha Newcastle sura yao ya pili kwamba nini wanaweza kufanya wakiamua kukabia chini ... compact 4-4-2 ambayo inafunga spaces , ndani hakuna njia , Newcastle walipata tabu sana kuwafungua Arsenal hasa kwa kutumia ile silaha yao ya combination play ( Bruno - Trippier - Almiron )

NOTE

1: Jorginho ali control sana mchezo hasa kipindi cha kwanza , simple passing na humuoni akiliacha eneo lake tupu

2: Arsenal kwenye mipira iliyokufa 🔥 hakika Nicolas Jover anafanya kazi vizuri

3: Leo Arsenal walikuwa wanacheza kama vile wana hasira na Newcastle , mbinyo huo 🔥😀

4: Sifa ya Newcastle ya msimu uliopita ya kuzuia vizuri msimu huu imepotea ... wameruhusu magoli 4 mechi kadhaa mpaka sasa

5: Bukayo Saka sasa hivi ukijaa tu kwenye mfumo unaokota kambani

6: Licha ya kurusu magoli 4 lakini performance ya Karius huwezi amini kama alikuwa hachezi 🤝

7: Mbio za ubingwa bado za moto sana

FT: Arsenal 4-1 Newcastle

FB_IMG_17088175049803353.jpg
 
Tunaomba radhi ndugu zetu leo kumekuwa na goli chache🤠🤠...tunaahidi tutalitatua hili tatizo mechi ijayo...asante kwa kuwa nasi usiku wa leo tukisheherekea kilele cha Tetaball
Mmefanya vizuri kutuomba radhi. Hatujafurahishwa kabisa na kitendo cha kuwapiga wale mijusi milia 4-1 badala ya 5-0, 6-0 na kuendelea.

Inakasirisha sana kuona tumepiga mtu 6-0, mwingine 5-0, halafu hiki kimjusi tunakipiga 4-1. Hii inamaana kiwango chetu kinashuka na tusipokuwa makini tutakuwa kama manyumbu.

Kurekebisha hili, Sheffield anatakiwa apigwe kuanzia 7-0 na kuendelea pale kwake ili mahesabu yetu yakae sawa.
 
Back
Top Bottom