Arsenal (The Gunners) | Special Thread


Arsenal haimizi watu wala nini ila zile uharo wenu na matokeo yenu ya mezani ndiyo inafanya watu tunapiga kambi hapa
 
Yamekua hayo tena nyie kabla ya game si mlijidai mkisema itafikia kipindi hatagusa mpira kwa kiungo cha Ode,Mchele, na Babu
. Kwamba mpaka half time atakufa goli 5
Chelsea ni mid table team kama Aston villa na Fulham, kukamia game ndo kawaida ya mid table team
 
Hiki kitu nilikiona arsenal mara nyingi saana inatokea hivi, yote kwa yote draw sio mbaya, ukizingatia tayari ngoma ilikuwa imeinamia kwetu.

Kwanini partey hakucheza!? Naona mtiririko wa timu haukuwa mzuri, odergard akapotea, jesu huduma akaikosa.
Kai akaingia akajikaza, jana kai kajitahidi.
Saka atafutiwe mtu wa kumpa challenge
 
Achana na mambo ya Form bana, Jana Arsenal walikuwa Terrible vibaya mno lakini still waliweza ku managed to come back from 2 goals down .
Biggest rivals wako anachomoa goal 2 nyumbani kwako bado mnaona ni kitu cha kawaida.
Unajua boli kaka
 
Achana na mambo ya Form bana, Jana Arsenal walikuwa Terrible vibaya mno lakini still waliweza ku managed to come back from 2 goals down .
Biggest rivals wako anachomoa goal 2 nyumbani kwako bado mnaona ni kitu cha kawaida.
Kweli aisee arsenal Jana ilikuwa hovyo, Chelsea alistahili kushinda kulingana na nafasi walizotengeneza.. japo binafsi niwapongeze kwa droo walopata..
 
Hii nchi ndo maana inashindwa kupata maendeleo sababu kwenye bongo za watu kumejaa funza tu

Hivi anaeshangilia draw ya jana ni arsenal au kenge? Kwa arsenal draw tunahesabu tumeangusha alama ila kenge zinaona ni ushindi

Chelsea hajashangilia draw, Chelsea mpaka sasa wanajiuliza imekuwaje wamepoteza ile game na wakati ilikuwa game yao kabisa.

Arsenal humu ndo mnashangilia draw ambayo imekuja ki miujiza tu , chelsea mbovu mpaka dakika ya sabini alikuwa amewatawala kila kitu .
Nyinyi false hopers tumewazoea false hopes kibao
yaani before game mlijipa ushindi wa goli 3 lakini after match mnaunda hope nyingine et chelsea ameshangilia ku draw .

Mpaka kufika may mnaweza kuwa tayari vichaa si kwa matumaini bandia haya , kupeana false hope ni kitu endelevu ona hapa last season ulijitangazia ubingwa April.
 

Hii timu ni kichekesho yaani wanakuambia Partey hajaanza utafikiri partey ndo winning signal , siku partey anaanza watatafuta sababu zao nyingine
.

Yaani ni sawa na chelsea waanze kulalamika kutokuwepo kwa nkunku maana jackson kakosa goli la wazi kabisa, lakini huwezi kuona chelsea wanalalamika hii ndo sababu hii arsenal tunaita false hope team yaani huwa wanatafuta sababu kila siku.
 
Wewe sio mzima wa akili aisee,, hakuna beki wa kati wakumuweka nje Thiago Silva licha ya umri wake.
 
Kwani chelsea amekatazwa kua form

Au ni makosa ya Arsenal wewe pambana mbona Newcastle alianza kwa kusuasusa now anapambana kashakuacha parefu, achana na hoja mfu izo
 
Tutatafuta sababu nyingi sana ila Chelsea jana walikua bora kutuzidi basi ndo ukwel huo hakuna kingine mzee
 
Kwani chelsea amekatazwa kua form

Au ni makosa ya Arsenal wewe pambana mbona Newcastle alianza kwa kusuasusa now anapambana kashakuacha parefu, achana na hoja mfu izo
Ndani ya hiyo comment yako kuna mambo matatu umeyafanya wewe mwenyewe.
1. Mkurupuko
2. Swali
3. Umejijibu wewe mwenyewe
 
Kuhusu mudryk,
Sio mbaya sana ila kwa pesa signing fee yake ifike mahali tukubali kwamba huyu ni potential sio complete article.
Jana kafunga,trossard kafunga pia.

Binafsi najuta sana kumpata trossard at late age.jamaa ana almost kila kitu.impact yake kwa arsenal huwezi ilinganisha na impact mudryck kwa chelsea.
Naamini mudy ni mchezaji mzuri akipata striker mzuri na viungo wazuri.hawezi ile one man show anategemea team compactness kudeliver.
Mpeni muda,chini ya enzo na caisedo anaweza akawapa kitu ila sio more than imagination.
 
Kwangu mimi kuna wachezaji naona muda wao unakaribia within 2-4 years watalazimika kuondoka kadri tunavyopata quality players

ODEGARD. Jamaa anakosa nguvu,high intensity driving hasa tukikutana na team physical and pace natured.kwa aina ya team anayoijenga arteta ni suala la muda tu.LCM ni eneo ambalo anacheza constantly kwa kuwa hatujapata right player eneo hilo.
Kuna quality player siku akipatikana ambaye ana
Ball vision
Ball striking
Bird eye kwenye pasi ya mwisho
Ball dribbling
physical on and off ball
Kasi na uwezo wa kuzifungua low block team.
Siku akipatikana nawaambia Captain ode atakaa bench na atauzwa.

Arteta na Edu wanatafuta huyu mtu taratibu.

JESUS.Jamaa ni moja ya watu ambao ni very blessed.namfananisha na mtu anayemiliki AUDI ila haina staring.wote tunajua ubora wa AUDI ila ikikosa "steringi" value yake inapotea.Jamaa uwezo wake wa kufunga hata ile ball striking ni ya kawaida.ATAONDOKA hamalizi miaka miwili.

Kuna wachezaji sisi tunawaona permanent ila kwa arteta na kichaa wake edu ni wachezaji walioletwa kutengeneza reputation ya team ili kuvuta toptop quality players.ni kama trekta wanasafisha njia ila baadae wanabebwa na lowbed ili wasiharibu walichotengeneza.

Nketiah,nelson,Jog20 hata rowe wataondoka taratibu kadri quality players wanavyokuja.

Arteta anatafuta kwa nguvu mno mtu wa kumrithi partey hasa kutokana na majeruhi yake ila amegundua you don't get such a player coz you have money.
Kuna mengi kwenye kichwa cha arteta ambayo mashabiki na wachezaji hawayatarajii ila yapo.
RAMSDALE SAGA inapaswa iwe somo kwa kila mchezaji na shabiki kwamba kuna heights Arsenal inazitafuta na itamtoa sadaka yeyote ili kufikia malengo
 
We hujielewi kweli. Yani umeshindwa kumaliza mechi nyumbani kwako ukiwa mbele kwa mabao 2 halafu unategemea uje kuifunga Arsenal Emirates?

Ukitaka jibu nenda kawaulize Man City walichokutana nacho.
Hahahaha saivi munashanglia droo maana mulikuwa na matokeo yenu mfukoni 😀😀 sisi bado tunajitafuta. Ninyi mataito kontenda imekuwaje mumeshindwa kubeba point zote tatu?!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…