Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Uko sahihi kabisa na Fabio Vieira leo ametoa pasi murua sana kwa Jesus kwenda kufunga, na hivyo ndivyo Zinchenko apaswa kuangalia analink vipi mchezo na mchezaji wake wa kiungo (Havertz).

Hata mchezaji akiwa mzuri kiasi gani akijiunga na timu ni lazima ajifunze kucheza na wachezaji wenzie wapya mifumo mbalimbali yaani formations.

Kuna kutoa pasi kutoka kwa beki iwe Zinchenko kwa Havertz au Ben White kwa Bukayo Saka na weye kama beki watakiwa ufanye timning ya ile pasi yako na ikiwa mbovu au umechelewa ndo utaona Saka au Havertz ashindwa kuumudu mpira (ball control) na huupoteza kwa adui.

Pia Martinelli na Saka wakiwa wachezaji wa pembeni kuna kujenga mashambulizi na mabeki au Odegaard na kama hakuna hiyo link Arsenal hupata taabu sana kufanya mashmbuliz ya maana.

Hivyo kulink mchezo na mashambulizi hasi kufunga ni lile goli la kusawazisha la Arsenal yaani mchezo umeunganishwa tangia mwanzo hadi mwisho kwa Onana.

Hivyo wenzetu hawa hawauchezi tu mpira na ndo maana Tierney na Tavarez au Lokonga na wamepewa tena muda wa kujifunza namna ya kulink mchezo bila kukimbia tu kama wafukuza sungura wa kitoweo.
 
Wadau humu hatupingi Kai kupata time. Everyone anahitaji kucheza.

Vieira alipata time akianzia nje. Na Kai iwe hivi.
Yote sawa mkuu, Hakuna anayelazimisha aanze ,tatizo wadau wanaweka chuki Sana

Ilifika hatua mtu anadai Partey anacheza RB ili Kai acheze

Leo Partey alikuwepo?

Mchezaji anahitaji muda azoee , Kuna mchezaji alichukua muda Kama Partey kuzoea lone 6

Arteta on Havertz:

"I said to him yesterday beginings are hard. When I met my wife at beginning it was hard to conquer her, I had to try and message and go and go...

At end when she said yes we want to be together, it's beautiful."
 
Nachokiona ni kwamba Kai siyo m bovu ila tu kwenye role ambayo anataka arteta acheze sana kuizoea kwa sababu yeye ni mshambuliaji . Xhaka ilikuwa rahisi kui master vizuri. Hata Fabio mwanzo alikuwa hivi hivi hasa lege lege Nashukuru sasa hivi Fabio anau wezo mzuri sana . Hata siku Ode akikosekana ntakuwa sina wasi wasi kutokana na uwepo wa Fabio. Ila leo naamin kama angeanza jorginho na rice game ilikuwa inaisha mapema sana
 
Nilikua naona Martinelli hamuamini Kai, akipata mpira Kai akitokea Martinelli anatafuta njia kwingine.

Katika games nne za points 12 tumepata 10. Siyo mwanzo mbaya hata kidogo. Kilichopo benchi lione ni kivipi tunaweza secure points nyingi zaidi
Nili Note hiki kitu na mimi, baada ya kupika pasi ya hovyo iliyoenda kuzaa bao la Man U.
 
Kwann asianze na jorginho na rice kipind hiki partey hayupo naona kam mchele utatupa faida san ukiwa juu kidogo sabb jamaa anatupa energy y kutosha kila angle y uwanja
 
Muda wote alochezea Chelsea Havertz alitumika kama mashambuliaji na ndipo alipopata shida ya kutofunga magoli mengi.

Kai Havertz ni deep lying Midfielder nafasi alokuwamakicheze atimu yake ya Borussia Dortmund.

Hiyo ndo nafasi ambayo Arsenal wataka awe akicheza.
 
Harvertz kachukua Nafasi ya Xhaka ???? How

May be kabadilishiwa majukumu ila kusema amechukua nafasi ya Xhaka ni uongo

Nafasi ya Xhaka ilikua inatoa Assist na Magoli

Kwa sasa kitu icho hakipo mpaka sasa

Nguvu ya kuzuia wakati hatuna mpira now zinazibwa nafasi ambapo kwenye hilo Kai anasaidia

Mtu naemuona anauwezo wa kuchangia Goals & Assist kwenye LCM alipokua anacheza Xhaka ni Fabio na Trousard ila kwa Kai naona Awe ST tu basi wawe wanaachiana nafasi na Nketia,Jesus
 
Alipokuwa akicheza Xhaka ndipo anapocheza Kai Harvetz na ndo maana Xhaka akaruhusiwa kuondoka.
 
Kwanini Trossard/Rowe/Vieira wasianze kwenye LCM kisha kama kocha ana mahaba na Kai amu-intergrate taratibu kwenye kikosi kwa kuingia sub? Mbona anafosi sana
 
Iyo game inaitaji mafundi tupu hasa LT19
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…