


Arsenyau mnataka mnipe rushwa ili na mimi niunge mkono juhudi?
Humu wakikosekana watu kama kina
Flano na
Mkohoti jukwaa litapoa sana hili, kila siku mtakua mnaishia kutukanana wenyewe kwa wenyewe humu ndio maana watu wenye busara tunakuja humu kuweka mambo sawa.
Ila jana mbona niliwapongeza kiroho safi tu mkuu, ingawa mliondoka na points3 lakini mlivuta pumzi za moto, tena bahati yenu sana hakuwepo Zaha na Olise la sivyo humu leo kungejaa matusi.
Baada ya kadi nyekundu ya Tomiyasu kwa mara ya kwanza jana nimeweza kuipongeza defence yenu, sikutarajia kama mngekua na ukuta imara kiasi kile aiseee kwa jinsi Palace walivyokua wanawapelekea moto.
Kingine kadi ya pili aliyopewa Tomiyasu ile ki ukweli kabisa alionewa maana mimi binafsi sijaona kosa lolote alilofanya pale.
Kingine ni penalt ya wazi walionyimwa Palace baada ya Rice kumvuta na kumsukuma Eze ndani ya box, inawezekana refa aliikaushia hio penalt makusudi kwa kufuta makosa aliyoyafanya kwa Tomiyasu.
Kikubwa nilichokiona kwa Arsenyo hii Man Utd tuna point zetu 6 za wazi kabisa msimu huu, pona yenu ni marefa watuletee figisufigisu.