Ila asenali suala la kurusha mpira linaanza kuwa tatizo tena. Ni kama Wanaotakiwa kurushiwa wanakuwa wanajikabisha kwa maadui kimtindo
Kai sio mchezaji anayeonakana vizuri uwanjani labda anaonekana vizuri kwenye takwimu tu.
Na arteta kajiwekea kitanzi mwenyewe kwenye kumsajili kai kwa pesa ndefu,ni ngumu kwake kumuweka benchi,bodi itamhoji.
Ila kuna baadhi ya mechi itakuja kumgharimu sana,kwa sababu kai kwa sasa anakupa vitu vingi ambavyo ni nusu nusu kulingana na mfumo na kuna mechi unahitaji kitu kamili kutoka kwake au wachezaji wawili waliokaribu nae.
Arteta anajitahidi kuunda timu yake mdogo mdogo ila kwakuwa timu inauhitaji wa magoli na wafungaji wengi ni kuanzia eneo la kiungo kai atapata lawama nyingi za kuchelewesha pasi/kukosa goli (ufanisi wake ni wakawaida kwenye maeneo hayo).
Kai anakasumba ya kuchelewa kuamua nini cha kufanya akiwa na mpira na kwa mfumo wa arteta ukiwa ni mchezaji wa hivyo utakuwa unapishana na mashabiki.
Odegaard/Rice/Partey akikosa goli sio lawama sana ila kai akikosa sasa




itabidi avumilie kejeli

