Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Hivi huyu Timber ni beki kweli? Na kama ni beki je anajua kukaba? Maana kila compilation yake YouTube namuona anashambulia tu na kuwatoka wapinzani kwa spins na feints. Utani pembeni...Inaelekea atafaa kama Eboue flani kwenye attacking ila kwenye kakaba isije ikawa ni Trent Alexander-Arnold type. Kwa YouTube unaweza kudhani jamaa hakutani na attackers wa maana. EPL itamchallenge
Timber na Zinchenko watakuwa wakipanda kusaidia mashambulizi na kukaa sehemu ya kiungo.

Hio ndo sababu Arteta amtaka Timber.

Tomiyasu aweza lakini kuna kipindi hushindwa kusimamia mashambulizi.

Ben White ndo kabisa hawezi mara nyingi huwa weak point.

Hivyo kutafuta balance ya upande wa kulia na kushoto ndi Timber kapatikana acheze na Zinchenko.

Liverpool nao huwatumia Robertson na Trent Alexandra Anold kupanda kusaidia mashambulizi.

Man City huwatumia Kyle Walker (kulia) na Nathan Ake (kushoto) na kuna wakati beki wa kati John Stones huwa mchezaji wa kiungo.

Hiyo ndo system mpya ya uchezaji kwa kuwatumia mabeki wa pembeni na wa kati kuwa wachezaji wa viungo jinsi game linavyoenda.
 
Ana invert Sana kwenda kwenye midfield ,Anajua kukaba kuliko Zinny ndio utofauti wao

Ana accuracy kubwa ya pass , inamaana itakuwa rahisi kufanya buildup haraka na kwa usahihi
Erik alimtaka huyu Timber alivyokaziwa kwa Timber akamgeukia Martinez.

Hapo Arsenal tupo tunafanya donoa donoa Erik akaingia akaweka ofa nene kwa Ajax na mshahara kufuru Martinez akatua
 
Nauliza tena

Kwanini tukiongelea wachezaji wetu wa msimu ujao hua tunamsahau mno Trossard? Mfano tuliamini tunahitaji ST, viungo wawili na backup ya Saka. Trossard hashindwi kua ST na hashindwi kukaa RW

Moto upo kwenye kiungo
Hata Smith Rowe wanamsahau , Trossard alicheza mech za mwisho vibaya , kumbe alikuwa majeruhi, kafanyiwa surgery ndogo
 
Mwanzo United walimuambia De Gea ashushe mshahara kama anataka mkataba mpya.

Jamaa kakubali akasaini.

United wamerudi wamemuambia ashushe tena mshahara kama anataka kubaki
 
Watakuwa na mawazo ya kijinga Tu ata kama ni watu wa mpira,mfano mtu kama Garry Neville pamoja na kuwa mtu wa mpira unamuonaga ana Akili timamu?

Westham walitaka £100 tangu mwanzo kabisa na hilo kila club iliyotaka huduma ya Rice walilijua

Sasa kama unajua Westham wanataka £100 umuagize pep Abid ili iweje? itabadirisha nini akibid? ilhali ukifika hela inayotakiwa mchezaji anakuwa wako?
Ni maoni tu. Cha muhimu Arsenal wamepata mtu wao.
 
ARSENAL WIN UEFA FOOTBALL AWARD

Hii tuzo ya kutambua mchango wetu katika kupinga baguzi mbali mbali na kufanya mpira wa miguu kuwa rafiki kwa wanadamu wote tutapewa kesho.

Tumeipata hii kwa kampeni yetu ya 'NO MORE RED' inayopinga violence, hasa uchomaji visu kwa vijana wa mitaani London ili kufanya viwanja vya michezo kuwa sehemu salama kwa vijana kutembelea na kufanya mazoezi.

Pia tumekuwa timu ya kwanza kuweka mkalimani wa lugha ya alama kwene mechi za Emirates ili wenye ulemavu wa kusikia nao waweze kuenjoy zaidi mbwembwe za Saka na Martinelli na wenzao

Hongera kwetu
 
Haka katimu kanajitengenezea laana kenyewe baadae wakose ubingwa wamtukane kocha.
20230628_203012.jpg
 
Top 5 Journalists/ITKs for Arsenal news this transfer window.

Power Rankings

1 - @SamiMokbel81_DM
2 - @Teamnewsandtix
3 - @David_Ornstein
4 - @FabrizioRomano
5 - @AlexGoldberg_ (who is CFC but has been spot on with his takes)
 
Dahhh simu yangu haifungi picha za JF inaniuma sana kukosa fursa kama hizi

Anyway unaongelea katimi gani mkuu
Arsenal hao kwenye Twitter profile picture wameweka bendera ya LGBTQ ku-support Pride month halafu wame-post tweet ya "Eid Al-Adha Mubarak".
 
Nauliza tena

Kwanini tukiongelea wachezaji wetu wa msimu ujao hua tunamsahau mno Trossard? Mfano tuliamini tunahitaji ST, viungo wawili na backup ya Saka. Trossard hashindwi kua ST na hashindwi kukaa RW

Moto upo kwenye kiungo
Me mwenyewe nawashangaa wanaomchukulia poa. Alipokuwa Brighton alikuwa anafunga magoli mengi kwenye tight spaces. Hii system ya center forward kuungana na viungo, sometimes inawakoseshaga sana magoli
 
Za Ndani kabisa ,kumbe Arteta kapewa £300m

Anataka amalize usajili mapema aende nao wote pre season, asiowataka atakuwa anawaondoa akiwa Pre season

Bado anataka Kiungo mmoja ambaye ni Lavia ,personal term ameshakubaliana na Arsenal wiki 2 zilizopita ,


Pia anahitaji Winga mmoja wa kulia
 
Back
Top Bottom