Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

DiMarzio kuhusu Rice:

Arsenal au Liverpool ndio mahali atakapoenda, Sidhani kama atahamia Chelsea kwani wana wachezaji wengi kwenye safu yao ya kiungo."

“Nina uhakika kwamba [Chelsea] watajaribu kumpata kama wanajua kwamba anakaribia kusaini Arsenal kwa sababu tu hawataki aende huko. Chelsea inanunua wachezaji kama mchezo na ni hali mbaya kwa sasa." View attachment 2564041
Di marzio anasema kweli kuwa Chelsea wanaweza act km ilivyokuwa kwa Mudryk, ni suala la Declan mwenyewe kuamua aende wapi, Chelsea sasa hawana natural #6 baada ya kumuuza Jorginho, lakini km tutamkosa Rice bado kuna kiungo mzuri tunaweza kumpata Moses Caicedo. Ila kwangu priority ni Declan Rice jamaa anajua.
 
Kwanza nimpe Happy birthday Willo Saliba, ndio Kwanza anatimiza miaka 22


Hivi majeraha ya Saliba mbona haisemwi au atakuwepo after international break?

Tomiyasu yeye kafanyiwa Upasuaji

Maana pale Nyuma bila Saliba hatuwezi kabisa kuanzia mpira nyuma kwa kujidai

Nimeangalia mechi mbili tatu kwa umakini alizocheza Holding ,pale Nyuma tunaanza mipira mara chache Sana ,mara nyingi Ni kubutua au buildup itaanzia mbele kwa mbele

Mchezaji mmoja kumbe anaweza haribu system nzima


Mechi na Fulham walikuwa Wana press na wachezaji Hadi 6 na tunawatoka vzr bila shida ,ila Kama yupo holding lazima tutachoma kibanda tu

Angalia hapa Vs Fulham , Marco Silva hakuamini ,Pass Moja ya Saliba inaenda kwa Xhaka tunawaweka Goli


View attachment 2564068
Saliba na hoding ni km Messi na Anthony.
 
Di marzio anasema kweli kuwa Chelsea wanaweza act km ilivyokuwa kwa Mudryk, ni suala la Declan mwenyewe kuamua aende wapi, Chelsea sasa hawana natural #6 baada ya kumuuza Jorginho, lakini km tutamkosa Rice bado kuna kiungo mzuri tunaweza kumpata Moses Caicedo. Ila kwangu priority ni Declan Rice jamaa anajua.

Caicedo ana pumzi kuliko Rice
 
Brother, Ahsante sana kwa kunikumbuka. Nipo japo nimepotea kiasi.

Nawamiss wanangu nyote, nitarudi kuja kusheherekea ubingwa nanyi hapa hapa jukwaani. Sijui kama kuna sherehe yoyote inaandaliwa ya kusheherekea ubingwa na kama ipo basi ntahudhuria kama itakuwa Dar.

Mwanangu isajorsergio upo?
Kaka nakumbuka ulisema msimu wetu ni 23/24 ila tupo ahead of schedule tayari
 
Di marzio anasema kweli kuwa Chelsea wanaweza act km ilivyokuwa kwa Mudryk, ni suala la Declan mwenyewe kuamua aende wapi, Chelsea sasa hawana natural #6 baada ya kumuuza Jorginho, lakini km tutamkosa Rice bado kuna kiungo mzuri tunaweza kumpata Moses Caicedo. Ila kwangu priority ni Declan Rice jamaa anajua.
Hivi hatuwezi wapata wote kisha tukaongeza RW?
 
Naona mjadala umehamia kwa Rash Vs Martinelli, ila ni matusi kumlinganisha mtu mzima yule na vijana wadogo hawa

Marcus Rashford Bukayo Saka in the Premier League this season:

Goals - 14 / 12
Assists - 3 / 10
Key passes - 18 / 61
Dribbles - 32 / 46
Shots - 69 / 69
WS Rating - 7.05 / 7.50
20230319_213642.jpg
 
Naona nimepiga kisu Cha mbavu wote mnatoka mafichoni kuja kutapatapa hapa mni jibu kwanini mjawai kubeba hata ueropa kwanza.

Arsenal ingekuwa Man city in the passed 10yrs, sisi wengine tungekua
Tumetoroka Tanzania
Wakati ukifika tutabeba
 
BEN WHITE

Msimu huu kwa " baadhi " ya mashabiki wa Arsenal wachezaji ambao wapo kwenye mawazo na midomo yao sana ni Saka, Odegaard , Martinelli , Partey , Zinchenko , Saliba , G.Jesus lakini kuna jina inawezekana ukakutana na wana " Gunners " kumi lakini wasilitaje : BEN WHITE

Binafsi naamini ukitaja wachezaji wanne muhimu wa Arsenal msimu huu nitataja jina la Ben White nikiambatanisha na sababu zangu ambazo ni :-

1: Upatikanaji wake uwanjani . Sikumbuki lini nilisikia Ben White atakuwa nje ya dimba kwa miezi kadhaa au wiki 3 . Moja ya sifa kubwa kwa mchezaji bora ni upatikanaji wake

2: Kutoka kuwa beki wa kati mpaka beki wa kulia na kucheza hiyo nafasi utasema ndio ulianzia huko maisha yako ya soka sio rahisi hata kidogo . Binafsi naamini ni nafuu kuwa beki wa pembeni kucheza beki wa kati kuliko wa kati kuwa fullback

3: Ben White amekuwa muhimu sana katika muundo wa uchezaji wa Arsenal na ana husika katika phase zote tatu . Kuna wachezaji ambao wanahusika :-

A : Kwenye phase ya kwanza pekee ( kuanzisha mpira nyuma ) build up

B: Phase ya pili pekee ( kwenye kiungo )

C: Phase ya tatu pekee : kwenye ushambuliaji

Lakini Ben White ndani ya Arsenal anatumika kwenye phase zote tatu ... kivipi ?

Arsenal wakiwa na mpira White anabaki nyuma kutengeneza BACK 3 ( White Saliba na Gabriel ) ili kumruhusu Zinchenko kuingia ndani kama kiungo karibu na Partey kwenye muundo wa 3-2-2-3

Arsenal wakisogea juu Ben White anakuwa kama msingi wa Bukayo Saka na Odegaard ule upande wa kulia wa Arsenal ( Odegaard kama namba 8 wa kulia , Saka winger na White anakuwa nyuma yao .

Wakifika eneo la wapinzani Ben White anakuwa mara nyingi mpishi wa Saka kwa kupiga pasi za ndani zaidi ni mara chache kumuona White anafanya overlaps

Kuna hili sasa la muhimu sana : waangalie Arsenal wakiwa na mpira na position ya White : kwenye ile " REST DEFENSE " ya Arsenal ( Yani namaanisha shape yao ya ulinzi wakiwa wanashambulia ) yeye anakuwa sambamba na Zincheno Partey na White katika mstari mmoja compact mbele ya Saliba na Gabriel wakiwa tayari kuzuia counter attacks lakini pia kupora mpira na kuurejesha kwa watu wa mbele ( recycle possession to sustain attacks )
Haongeze nguvu kweny kukaba yupo softi sana
 
Wakubwa tunaposema tutaidominate hii ligi kwa miaka 10+ tunamaanisha

Kuna balaa hili hapa dogo anaitwa Charlie Patino yupo Blackpool kwa mkopo

Anacheza CM(LCM) nafasi ya Granit Xhaka

Unyumbulifu

Tackling

One touch football

Press resistant

Tight spaces

Long balls

Interception

Kama atarudi msimu ujao sehemu ya kuimprove ni physicality tu

Naweza kum-rate huyu ahead of Vieira (Maoni yangu)

Kama tukimpata Caicedo/Rice tukaongeza RW na RB naona tutaenda kuchallenge UEFA next season

makaveli10 ukipata muda mfatilie huyu
0_GettyImages-1287222760.jpg
 
Wakubwa tunaposema tutaidominate hii ligi kwa miaka 10+ tunamaanisha

Kuna balaa hili hapa dogo anaitwa Charlie Patino yupo Blackpool kwa mkopo

Anacheza CM(LCM) nafasi ya Granit Xhaka

Unyumbulifu

Tackling

One touch football

Press resistant

Tight spaces

Long balls

Interception

Kama atarudi msimu ujao sehemu ya kuimprove ni physicality tu

Naweza kum-rate huyu ahead of Vieira (Maoni yangu)

Kama tukimpata Caicedo/Rice tukaongeza RW na RB naona tutaenda kuchallenge UEFA next season

makaveli10 ukipata muda mfatilie huyuView attachment 2564677

Ni ngumu kumpata Caicedo kuliko Rice, simpi nafasi ya kuja Arsenal kwa sababu price tag itakuwa kubwa mno
 
Back
Top Bottom