Fabio Viera the DELIVERER, William SALIBA the FINISHER.
Assist ya 6 Kwa Fabio Viera msimu huu na inamfanya kuwa sawa na Martin Odegaard na Gabriel Jesus.Kinara ni Bukayo Saka na Assist 9 kwenye mashindano yote
Ukiiwekea Muktadha unaona ni msimu wa kwanza wenye mafanikio kwa Fabio Viera ikiwa ameanza kikosi Cha kwanza mechi 12 tu.
Leo akiwa amepewa Majukumu ya Martin Odegaard kikosini kama #8 ule upande wa kulia kwenye 4-3-3 ya Arteta. Kila pasi yake ilikuwa sumu.Kijana anaendelea kukua Kimwili,nguvu na akili.Mafanikio yake ndani ya Arsenal hayaepukiki
MIKEL ARTETA aliikabili vizuri sana 3-2-5 ya Sporting Lisbon kwenye kushambulia na 5-2-3 Bukayo Saka akishuka zaidi kwenye mstari wa Mwisho.Tatizo ilikuwa kupiga pasi ambazo hazina macho wakati team inatoka kuanzia nyuma.
JAKUB KIWIOR alipewa mechi yake ya kwanza tangu ametua kutoka Spezia.Haikuwa mechi nzuri sana lakini bado unaelewa kwa kijana.Baadae Aliingia Gabriel MAGALHAES na utulivu ukarejea.
Arsenal wanaonekana kuwa na Faida nyingi kimbinu na Kiufundi dhidi ya Sporting Lisbon Lakini Sporting Lisbon wamefanya mechi iwe ngumu na tamu.Kwanini?
Kwasababu kwanza ya Mabadiliko Makubwa ya kikosi ambayo Mikel Arteta ameyafanya kwenye kikosi Cha kwanza.Lakini pia Sporting Lisbon wana mafundi wa kuichukua na kuitawala mechi kutoka kwa Arsenal
Welcome to the Emirates SPORTING LISBON
FT

UEFA Europa league Sporting Lisbon 2-2 Arsenal