Arsenal (The Gunners) | Special Thread

£200k 🙄🤔 Chelsea hawataki masihara, wanatumbua tu pesa 😂
Ila akiingia kwenye mfumo si suala kumlipa mpunga huo akibuma sasa ndio changamoto.

Na nisiwe mnafiki naombea abume wakome 🤣
 
Liva hakuchukua point with 4 3 3 against 3 4 3 ya hawa hawa Spurs.

Tukiachilia mifumo ila tunahitaji wachezaji wa kuendana na mfumo, kwa 4 3 3 naona tunao ukimtoa Nketiah coz ni mgumu kurudi mid tofauti na Jesus.

Kwa maoni yangu Lloris anamuacha mbali Aaron. Naona mid wanaweza wasitukomalie nayo instead wakaitumia kudefend tu na mashambuliza yakapitishwa pembeni wakarely kwenye pace ya Son dhidi ya White na Kulusevski dhidi ya Zinny.
 
Shida kubwa wakiamua kucheza counter attacks, itakuwa shughuli pevu kwetu.
 
Mbona Zinny tulimnyakua kimya kimya tunashindwaje sasahivi kusaka mtu na kumaliza deal bila kelele?
Hata huyu sidhani kama ilikuwa ni dhamira ya Arsenal proposal yao iwe public, walichokifanya Shakhter ni kuweka hili deal public ili kuinvite bidding war; na kwa kiwango kikubwa wamefanikiwa kuexrtact as much cash as what they wanted.

Sent from my M2101K7AG using JamiiForums mobile app
 
Ffp haiwezi tumika hapa kwakua Roman wakati anaiuza timu madeni yote yalifutwa. Hivyo kwenye ffp Chelsea ilionekana iko 0.

Ffp inaangalia mapato yako na matumizi kila baada ya miaka 3. Na kwakua deni lilifutwa hii inamaanisha ffp inaona Chelsea katumia 500M na hana negative.

Ujanja mwingine ni amortization mfano dili la Mudryk ni 105M na mkataba ni miaka 7 ukiigawa hii 105 kwa miaka 7 utaona actually hii inamaanisha kila mwaka inalipwa 10.4M so bado wanakua hawajaiingilia FFP.

Swali hili liliwafaa Barca ambao tunajua wana deni la 1B ila walikua wanasajili non stop
 
Ndio muda wwa kukaza kubeba kombe, unadhani msimu ujao wwapinzani wetu watakuwa lonya lonya tena?
Hii umeandika kimihemko, kwani factor gani iludetermine msimu huu Liverpool/ Chelsea watacollapse, hata wao walichukua ubingwa miaka ya nyuma sababu Arsenal ilikuwa mbovu, united ilikuwa mbovu, tusiishi kwa kukariri. Regardless of anything, msimu ujao tena we are in for title.

Ajabu watu mliokuwa ooh Arteta hana uwezo ndio wa kwanza kulaumu uongozi umsupport ili Arsenal ichukue ubingwa.
 
Kivipi roho ituume kwa mchezaji ambaye hatujawahi kumuona?

Nilikunja kwa Locatelli na Vlahovic kwakua niliwaona na nilijua wakija watakua msaada lakini Mudryk hata sijawahi mjua kabla ya hili saga.

Na ofa yetu Arsenal bado ilikua kubwa kwaajili ya mchezaji anayekuja kua backup. Narudia tena kwa hapa tulipo tukisajili mid mkali na winger wa kawaida mi sina tatizo na mtu.

Odegaard namba ya Saka anacheza bila shida.
 
Muda ni msema ukweli, tuombe uzima tu, tukutane msimu ujao.
 
Hiyo NB nimeielewa sana
 
Kweli kabisa. Sisi utamaduni wetu ni kuapproach na kufanya maongezi kimya kimya maana hatupendi wenzetu wajue ili wasivamie. Fabio Vieira ilikuwa hivi hivi. Wakati Liverpool wanamfikiria tu wanakuta tushamchukua zamani. Sasa Shaktar wakamwaga radhi mbaya kabisa. Boss wao anatoka hadharani na kusema 'kwa anayemtaka Mudy, bei ni 100. Kama Antony kauzwa 100, basi Mudy naye 100'. Tukipeleka ofa, anatoka anasema 'Arsenal kaleta 50, jamani si nilishasema Mudy tunataka 100?' Mara aseme 'klabu kibao zinamtaka Mudy, na bei yake ni 100 kama Antony.' Hii tabia ya kuanika anika imewasaidia kupata bei waliyotaka.
 
Aisee kumpata kama yule ni kazi sana, hebu ngoja tuone Mudryk kama atafikia ata robo yake
nadhani tunapaswa kumpata mtu kama hazard wa kipindi kile. siyo huyu wa sasa. siipendi chelsea ila nilikuwa naanalia game zenu kwa sababu ya hazard tu. full entertainment jamaa alikuwa anajua aisee
 
Ukweli ni kwamba usajili wa Mudryk kwenda Chelsea unaweza kuaffect mbio za ubingwa kwa Arsenal msimu huu cuz naamini wachezaji pekee wa kusajiliwa Arsenal km rotation ya Saka/ Martinelli ni Mudryk ambaye kaenda Chelsea, waliyobaki ni Raphinha & Rafa leao.

Raphinha / Leoa ni vigumu kuwasajili kwa dirisha hili, hivyo binafsi nadhani kwa budget yetu ni bora tusubiri nxt window tupate winger mzuri zaidi but we should pay the price, tuwe tayari kuukosa ubingwa ikiwa long term injury itawapata wachezaji km Saka / Martinelli. Kumkosa Mudryk kunaweza kuaffect progress yetu msimu huu tu km injury itatokea kwa our natural wide players ila hakuwezi kuaffect project ya Arsenal kubang, kamwe.
 
Huu ni wakati vijana wa Arsenal kuonyesha uwanjani kwamba Edu na Arteta kwanini umlikua mnahangaika na huyo wakati sisi tupo?! Mashabiki tulieni. Kambini mambo ni shwari, leo spurs anakaa hamna namna.
Tuna miaka 10 hatujawahi kumfunga spurs away na katika game Kama 10 tumetoa draw only 2 times ,so anything can happen najua tutawazidi kwa kumiliki mpira but defenders wetu na wasiwasi nao sana kwenye counter attacks za spurs inabidi leo watulie mambo ya kukabia juu yanaweza yakatuumiza but tusubiri game muhimu ambayo itatoa direction season hii ukiachana na next game vs Manchester United lazima tupate 3 points leo ili next week tunaenda kumaliza mchezo tunakuwa juu zaidi ila leo ikitokea negative results tutaenda game ijayo vs Manchester United pressure ikiwa juu na watu wazima tukaanguka so game ya leo sio rahisi hata kidogo in my opinion
 
nadhani tunapaswa kumpata mtu kama hazard wa kipindi kile. siyo huyu wa sasa. siipendi chelsea ila nilikuwa naanalia game zenu kwa sababu ya hazard tu. full entertainment jamaa alikuwa anajua aisee
Nisahihishe kama nimekosea

Hazard hajawahi kufunga magoli zaidi ya 15 kwenye ligi akiwa Chelsea.

Alipofunga magoli zaidi ya 15 ndiyo Madrid wakamfuata.

Au haiko hivi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…