Wakuu wenzangu vipi tena mbona kuna malumbano?
Nimejitahidi hapa Beghazi nami niweze kuangalia kabumbu lakini bado nasikia kwa mbali cluster bombs za majeshi ya Gaddafi.
Mimi nimekuwa mpenzi wa Arsenal kwa muda mrefu sana na nina imani ipo siku Arsenal FC watachukua kikombe cha Premier League lakini kwa wakti huu inawezekana leo wamewapa Man United kombe tayari.
Tuna mechi zita zimebakia tena zote ngumu tukianzia na Jumatano na Tottenham, na ukiangalia kuna 18 points hapo. Pia tupo nyuma kwa 6 points na Man United jumanne wanacheza na Newcastle United, kwahio hali ni ngumu.
Lakini wa kulaumiwa na mzee Wenger mwenyewe na inawezekana huu ukawa ndio mwanzo wa kununua wachezaji kwasababu mzee Kroenke amekwishanunua timu.
Wachezaji wa Arsenal wana kitu kinaitwa kwa kiingereza" immaturity" yaani kutokuiva kisawasawa na kuwa tayari "ku-grind out results" -yaani kujitoa na kuhakikisha unapata matokeo katika mazingira magumu.
Jana Manchester City walionesha dhahiri nia ya kutaka kushinda mchezo wao na Man United na walikuwa makini kwenye idara zote kiungo, ulinzi na ushambulizi. Man United nao wana nature hio na tulishuhudia mechi yao na West Ham United tena ugenini pale Upton Park London.
Hata jana Real Madrid walipocheza na Barcelona, walipopunguzwa na kuwa na wachezaji kumi uwanjani walizidisha ungangari na mwisho wake walipata penalti na Ronaldo akafunga na kuna watki walikosakosa kufunga goli kama sio Mesut Ozil kukosea lengo Madrid wangeshinda 2-1.
Kushinda mechi yoyote ile kunatokana na mambo hayo niliyojaribu kuyaeleza yaani "maturity" na ungangari. Timu yetu ya Arsenal bado haina vitu hivyo kwa sasa kwa sababu Emanuel Ebue ni mmoja wa mabeki wazoefu na angeweza kumsindikiza Dirk Kuyt nje ya eneo la hatari na mpira ama ungetoka nje au ingekuwa kona lakini akaamua kumkwaa mwezie na Kuyt akiwa mchezaji mzoefu alifahamu kwamba Ebue alikuwa nyuma yake.
Arsenal inahitaji wachezaji wengi wapya kuanzia idara ya goal-keeping, ulinzi, kiungo na umaliziaji. Hata Fabregas kwa sasa hachezi kwa moyo kwahio hafai. Kuna mazungumzo kwamba mzee wenger atafanya "clear out" kubwa wakti wa kiangazi. Hapo tutaona wachezaji wengi wakiuzwa kama Arshavin, Bendtner, Ebue na wengine kama Gael Clichy.
Arsena ya sasa ikiwa mabingwa basi tutakuwa ni moja ya mastaajabu ya Ligi ya Uingereza.
Hata hivyo bado mimi ni mwanachama mwaminifu tupo na tunawakaribisha wale wote wapendao kujiunga na Arsenal Supporters Trust.
Tembelea tovuti yetu na upate mengi.
Welcome to the Arsenal Supporters' Trust