Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Maddison hana ukali huo. Mimi binafsi naona Arsenal tunacheza kamari hapa ya kuwaridhisha mashabiki.

Arsenal ina shida na mtengeneza nafasi Maddison ana takwimu gani za kumfanya awe mtengeneza nafasi wa kumlilia? Na bahati mbaya sana mtengeneza nafasi kwa miaka hii wa kiingereza amekua Arnold, beki wa Liva, na Kane mshambuliaji.

Kwangu mimi huyu siyo mchezaji wa kuuzwa milioni 70 ila hapa ndiyo tunarudi palepale tunaposema "Ben White hana thamani ya milioni 50 ila Brighton wanaamini hiyo ndiyo thamani yake, Lukaku hana thamani ya milioni 150 ila inter wanaamini hiyo ndiyo thamani yake, Grealish hana thamani ya milioni 100 ila Villa wanaamini hiyo ndiyo thamani yake"

Arsenal ikipata winger mwenye speed, finnishing na skills hata za level ya Mahrez niamini mimi pengo la Maddison halitoonekana.
Kutokana na mfukoko wenu kutoboka, ni kheri mukamchukua japo thamani yake haifikii kiasi hicho cha pesa.

Napenda Arsenal irudi kwenye ushindani kama zamani.
 
Mkuu Maddison unamkataatu ila kwa Arsenal ilipo fikia inahitaji mtu kama yeye ili murudi kwenye ubora wenu.
Mpira wa siku hizi umebadilika.

Vitu vitatu vinampa namba mchezaji.
1) assisst 2) kufunga 3) kuzuia goli kufungwa

Timu zinasajili kiungo au forward kwa kufuata mfumo wa xg (expected goals) kama uwepo wako uwanjani unaweza sababisha chochote basi wewe namba utapata.

Ndiyo maana unaona pamoja na yote ila Arteta sub yake kubwa ilikua willian na beki mpendwa alikua luiz.
Kwa kufuatisha xg Willian ni wa muhimu na Luiz ni wa muhimu.

Sasa maddison kwenye hiyo system hajai sana na hivyo kuondoa uhalali wa kumlilia na kugawa pesa ndefu. White juzi tu kasajiliwa ila kuna blocks nne amezifanya ambazo zinaithibitishia timu kwamba huyu ni mtu sahihi.

Akija tutajionea
 
Maddison would be open to move to Arsenal, Sky Sports wanareport

Wanafki njooni tena muone ukubwa wa Arsenal, watu wanaacha European football kwa ajili ya Gunners.

Auba
Pepe
Partey
Now, Maddison & Lautaro
Deal la lukaku likikamilika, msahau deal la lautaro
 
uwezekano wa kumsajili Maddison ni mdogo kwa sasa, nadhani 1:5, jamaa wanataka Pound 70m cash. kitu ambacho ni kugumu
 
Leicester ni wajinga sana, hilo takataka thamani yake sio kubwa kiasi hicho.
uwezekano wa kumsajili Maddison ni mdogo kwa sasa, nadhani 1:5, jamaa wanataka Pound 70m cash. kitu ambacho ni kugumu
 
Matakataka ya London naona mnaenda kupigwa kwa Madison
Kuna kitu nafikiria, tunachoweza kutumia kwenye jukwaa letu la Arsenal, ambacho kitazifanya takataka kama huyu wasiwe wanaingia kwenye jukwaa letu kuonyesha ujinga wao. Stay put, naandaa modality.
 
We andaa tu, takataka kama ww ni buree kabisa.
Kuna kitu nafikiria, tunachoweza kutumia kwenye jukwaa letu la Arsenal, ambacho kitazifanya takataka kama huyu wasiwe wanaingia kwenye jukwaa letu kuonyesha ujinga wao. Stay put, naandaa modality.
 
Ukiwa unaandaa modality usisahau kuwa London is blue
IMG-20210601-WA0077.jpg


Sent from my CPH1923 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom