Laca alipungua makali msimu uliopita. Ilikua miyeyusho, mzito kwa kila kitu, kukaba, maamuzi, kushuti ilikua ni aibu kumtizama.
Msimu huu ameuanza same. Isipokua anascore ana uzito ule ule ila wakina Saka wanamforce katika baadhi ya mambo haswa maamuzi.
Laca wa msimu uliopita lile shuti alilopiga kwa Brighton ilikua ni mpira kupotea na asisogee kukaba. Hiki kitu nimeona kwa senior players wote.
Goli la Sala dhidi ya West Bromwich ni ushahidi.
Bellerin katoa pasi kwa Saka kisha hakufanya run kwenda mbele ingawa kulikua na nafasi badala yake akawa anarudi nyuma huku akiuomba tena. Means Saka angempa yangekua masihara ya siku zote.
Wakati Saka anapokea mpira pembeni unamuona Xhaka, Xhaka anaonyesha ishara ya kidole badala ya kutanuka na kusogea mbele ili agewe pasi.
Saka akatoa pasi kwa Emile na kufanya run ya kwenda mbele, hapo Xhaka bado kaganda na Bellerin yupo nyuma vilevile.
Emile akamrudishia Saka, kisha Emile akachomoka na kufanya run nyingine ya mbele.
Saka akampa Laca, Laca akatoa diagonal pasi ambayo ikakutana na Emile aliyekua amefanya hiyo run baada ya kumpa pasi Saka. Laca alivyotoa pasi akawa kama kasizi muda anasizi Saka akampita Laca fasta kwenda kwenye boks.
kisha Laca na yeye ndiyo akaanza kwenda mbele, hata hajafika mbali Emile alishatoa pasi kwa Saka na Saka akascore.
kubwa lao ni Auba. Hii movement yote inaendelea hata hakujaribu kujigusa kuingia kwenye box au kwenye 18 alikua mbali kabisa. A guy ameshangaa ile move ilivyokua goli limeingia akashangilia.
Yaani 4 seniors wameshindwa kubadilika. Kutofanya hizi runs ndiyo kumefanya Arsenal imiliki mpira ila scoreboard inatia aibu. Hizi runs za Emile ndiyo zilikosekana kikosi chetu.
Mimi nasema Guendouz arudi, akae pale mid game ambayo yeye, Saka, Tierney, Emile watakua pamoja halafu tuone fighting spirits zikiwa high kama kuna linaloshindikana