Nimewahi kusema hapa na narudia kusema,Arsenal tatizo si kocha
Arsenal Tatizo kubwa ni mmiliki .
Kuna mtu(Shabiki wa Arsenal) niliwahi kumuelewesha kipindi flani ambako Unai emery anatimuliwa na Nkamwambia Arsenal tatizo si Unai bali tatizo lipo kwa mmiliki!,hakutaka kunielewa bali alisema "Ngoja sasa Arteta apewe timu halafu uone kama Arsenal hajabeba ubingwa"
Nilijitahidi sana kumuelewesha namna ninavyoifahamu hii timu toka nilipokuwa Shabiki rasmi toka enzi za miaka ya 2000 lakini kijana aligoma katakata na kusema "Tatizo la Arsenal ni kocha"
Leo hii tena Arteta hafai!,najua mashabiki watapiga domo Arteta atimuliwe ili walete kocha mwingine huku wakiendelea kujifariji ya kwamba tumeleta kocha mpya na ubingwa tutachukua!
Huwezi kutaka kumuua nyoka halafu umpige kwenye mkia badala ya kupiga kichwa,HAIWEZEKANI!
NARUDIA TENA ,TATIZO LA ARSENAL SI KOCHA BALI NI MMILIKI BWANA KROENKE!
Ninaifahamu Arsenal ndani na nje hivyo watu huwa wakiongea eti tatizo ni makocha,huwa nabaki nawatizama tu!
Nina pointi nyingi za kuwatetea makocha na nina pointi nyingi za kuelezea kwanini Bawana Kroenke hafai!
USIKU MWEMA,LALENI KWA MAUMIVU