Niliacha Bayern anaongozwa na Koln jana mpaka dakika ya 56.
Atletico kapigwa 2 mtungi na Madrid ambayo imebakwa na Shakhtar nje ndani na ikasuluhu na Monchengladbach.
Inter kashindwa kusonga mbele UCL na kashindwa hata kujitetea na kuja Europa. Man u kaja europa kwa kufungwa na timu ambayo mwanzo aliifunga tano bila na alipigwa na amateurs wa Uturuki.
Liva hali mbaya mpaka wanaomba VAR iache kutumiwa ni kama vile wamesahau jinsi ilivyowasaidia kuwapa kombe.
Jana Everton kaipiga chelsea watu wamesambaratika kwenye uzi wao.
Arsenal tunaenda kucheza na Burnley with all of our shortcomings. Ni game ngumu as tulipofikia sasa hivi ni kila game kwetu ni utata tutamiliki mpira ila kucreate na kuconvert chances into goals imekua mtihani.
Anyway, naamini tutapambana. Imeshakua dhahiri kwamba ukicheza na Arsenal, paki basi piga kaunta paki basi, kama Jose na Spurs so nafikiri ndiyo itakavyokua na Burnley.
Unless they got cocky na kuamua kwenda nasi ng'adu kwa ng'adu then hapo tutakua tumejipatia namna ya kusecure points tatu.
Huu ushindi tunauhitaji. Ili wanakondoo waliopotea warudi.